FASTJET: My first and last experience

Mimi nilikata return ticket KIA/MZA/KIA, nikasafiri vizuri kwenda MZA, wakafuta route ya MZA/KIA bila hata taarifa siku na kusafiri wanasema walifuta hiyo route na wala hawakupiga simu, Ikabidi na mimi niingie tena hasara ya kutafuta upya ticket ya precision. Hawa watu inabid wajipange upya.
 
:yell::yell::yell::yell::yell:

Nilikutana nao pale BAKITA majuzi......kumbe ndio ilikuwa barua yako ile? Wataalam wa BAKITA waliwashangaa sana!

:heh::heh::heh::heh::heh::heh:


Ofisi nyingi bongo ongea nao kwa kiingereza na hata mawasiliano fanya kwa kizungu lazima upate huduma wanababaika sana. Kuna siku niliwapigia CRDB kuulizia sim banking.....nikatema yai, walihangaika sana kupata walau wa kuelewa na kunielewesha.....jaribu sikumoja kuwapigia CCM makao makuu ongea kiingereza uone watakavyohangaika hata kukata simu yako.
 
Mkuu Masanilo,

Pole sana kumbe tungeweza kuwa kwenye flight moja siku hiyo. Hebu niambie hiyo ndege iliondoka saa ngapi kesho yake? Au na wewe uliamua kuwakimbia? Usitarajie wakujibu hata siku moja, hiyo imetoka.

Tiba

Nilikwea Bus (Dar Express Luxury) maana mimi na ujanja wangu wote niko Mwoga baada ya kuambiwa ndege inahitilafu nikaona maisha yangu siyaweki rehani. Kumbuka nililala pale KIA na usiku nilisikia nyundo zikigongwa nikaona kama ni matengenezo hayo wacha nitumie Bus, sikuwa na hela ya Precision maana waliniambia Tsh 240000 one way
 

Pole kwa yalio kukuta,lakini shirika gani la ndege unatakiwa ufike 40 min before dep? hiyo kali na wewe mwenyewe vile vile kama msafiri sidhani kama ulijitendea haki,zisinge kutoka hizo zote kama ungekwenda 90 minutes before ya flight yako
ungeweza kupita kila sehemu bila tatizo kuliko unakwenda last minute una rush,ungeweza pia kupata ufumbuzi wa ndege nyengine kama ingekuwepo, anyway sikunyengine jipange fika mapema.
 
Nilinuia hiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kujaribu kusafiri na Fastjet na ilikuwa mara ya mwisho pia. Sitakaa nithubutu kufanya makosa tena hata kama Fastjet wata improve huduma kwa wateja na kuajiri watu wanaoweza kuwasiliana kwa heshima na wateja.

Hapa unasukumwa na hasira tu, inawezekana usirudie kutumia Fastjet hivi karibuni lakini siyo hata waki-Improve kama ni hivyo utaacha kupanda ndege hapa Tanzania, binafsi Air Tanzania walishawahi kunisababishia usumbufu na hasara kubwa sana niliapa kutopanda tena ndege zao, lakini pia hata Precision Air walishawahi kunisababishia usumbu wa ajabu sana kwa hiyo nime conclude kwamba Usafiri wa anga kwa hapa Tanzania bado hauja 'seto' vizuri, mimi nitaendelea kuwatumia Fastjet, Precision Air na hata Air Tanzania kwasasa na hata watakapo improve huduma zao, kwasababu so far Air Tanzania na Precision wameshanikwaza kwa nyakati tofauti na hii haitanifanya niseme wao hawafai kuliko Fastjet ambao kwa route zangu zoote sijapata bahati mbaya nao
 

Mkuu Sikonge huna haja ya kuomba msamaha kwani hakuna lolote baya ulilolisema, tuna elimishana na kupeana maarifa tu. Kwanza naomba nifafanue kwamba sikuachwa na shuttle asubuhi ya tarehe 27 kama unavyodai. In fact nilifika mapema kabla shuttle haijafika pale na dereva taxi na mlinzi wakaniambia uongo kwamba shuttle tayari imeondoka ili nikodishe taxi yao. Shuttle ilifika KIA wakati namalizia kucheck in. Suala la muda wa kuripoti uwanjani unategemea airline na airline lakini in general local flight unatakiwa uwe uwanjani one hour before departure time na international flight ni two hours, lakini hawa wenzetu wa Fastjet wao wanatangaza 40 minutes before departure kitu ambacho nilitimiza.

Hakuna mahali ambapo nilikwenda kinyume na matakwa yao. Lakini kumbuka pamoja na kukataa kunicheck in, hiyo ndege bado haikuondoka usiku huo.

Masanilo ni shahidi alikuwa asafiri na ndege hiyo pia.

Tiba
 
Ndio tatizo letu wabongo..Tuna alegry na kutunza muda afu tuliambiwa utaratibu tunakuwa wakali.Wenzetu ngozi nyeupe ukikuta mlango umefungwa hakuna kubembeleza
 

Pole Tiba
Mimi bahati huna si mwepesi sana wa kufanya conclusion kwa mkasa/ tukio moja. Kwa jinsi ulivyojieleza unaonekana ni mtu mwenye mwenye elimu kubwa ambayo ingekusaidia katika kufanya conclusion ambazo ni 'objective'. Sikubaliani na wewe katika kurusha hizi shutuma as if kwamba kilichotokea hakiwezi kutokea katika shirika la ndege lolote hapa duniani.
Mimi niliachwa na precisionair pale JNIA nikielekea mwanza nikiwa kwenye mstari saa 1.20 kabla ndege haijaondoka. Tulikuwa kama wanne hivi na mtu mmoja ambaye alionekana ni mkubwa tu. Ningekuwa peke yangu ningesema labda wamenionea mimi msukuma wa watu. Tukapewa ndege ya kesho yake saa 2 asubuhi kupitia kilimanjaro. Kilimanjaro tuliondoka saa tisa mchana.
But toka kipindi hicho nasafiri kama kawaida tu
Mkuu hayo ni matukio tu ambayo yangeweza kukupata hata ukiwa na usafiri wowote ule iwe meli, gari binafsi n.k
Ila nikuachie semi mbili, ya kwanza " WAKATI MWINGINE KUKOSA HUWA NI BAHATI" ya pili " EVERYTHING HAPPEN FOR A REASON". Unaweza kubisha lakini ipo siku utayakumbuka haya maneno yangu
Bye, cheeerz
 

Mkuu Mvaa Tai,

Asante kwa mchango wako. Lakini take it from me, I will go for expensive ticket with other airlines ili angalau kama kuna shida nisikilizwe kwa heshima kama mteja na wala sio kuwa treated kama kichaa au mpumbavu fulani hivi. Kumbuka tukio hili limenitokea karibu mwezi mzima uliopita lakini leo ndio nimeamua kulileta hapa jamvini hivyo sijasukumwa na hasira bali uhalisia. Walinifanya vibaya sana na hasa majibu ya huyo mwakilishi wao.

Tiba
 
Tiba,

Jitahidi ufike siku zote walau dakika 80 kabla ya muda hata kama wanatangaza dakika 40.

Kumbuka maneno ya Dr Dr Dr Dr Kikwete....." akili za kuambiwa, changanya na kwako."
 

Mkuu Polisi, yumkini wewe ni kati ya wachache wenye busara. Nashukuru kwa kunishirikisha kisa chako na mimi ni mtu ninayesafiri mara kwa mara kwa hiyo matukio ya ndege kuchelewa au kuhairishwa ni ya kawaida sana. Tatizo langu kubwa hapa pamoja na kwamba niliingia gharama za ziada ni majibu ya huyo mwakilishi wa Fastjet pale uwanjani usiku ule. Kama angeweza kunishawishi kwa lugha ya staha ni kwa nini hawawezi kuniruhusu kucheck in kwa wakati ule inawezekana leo nisingeweka bandiko ili hapa. Yaani anatoa majibu as if nimeenda kwake kumuomba hela ya kula au nauli ya kunifikisha mjini? Wanapashwa wajue kwamba we are their customers and we need to be treated with dignity.

Tiba
 

Mkuu Promiseme, huo muda wa 40 minutes before sikuweka mimi, ni wao. Kama wangesema niwe pale 90 minutes before ningefanya hivyo. Hata hivyo hiyo ndege haukuweza kuruka usiku huo pamoja na majibu ya ovyo ya mwakilishi wao pale.

Tiba
 
Aisee ulikosea muda wa kureport kwa hili nawatetea 40minutes?!nawachukia precision lakini sitaacha kupanda ndege zao to settle for the less imewahi kunisubiri twice KIA yani napigiwa simu na naingia ndani nakuta captein anatangaza jina langu.na nikiwa na masunduku yangu sina presha ya kulipia mzigo wala kukataliwa ndoo ya samaki.wananiuzi tu wanavyotaka kuhodhi hii huduma
 
Mkuu inawezekana wewe sio mzoefu wa usafiri wa anga hapa Tanzania. Hao Precision unaowasifia ipo siku utakuja hapa kuwaanzishia uzi wa kuwaponda. Kifupi inategemea tu bahati ya safari ya siku hiyo.
 
Nimekupata vizuri sana mkuu hapo kwenye nyekundu. Kwa kweli hata mimi ndiyo kilichonipata, ilibidi niingie mfukoni na nikaspend zaidi ya nauli. Inasikitisha mno. Bahati mbaya sijawahi kusafiri na ndege za wenzetu kwenda nje ya nchi, ningeweza kulinganisha. Tena ingekuwa enzi zangu zile nizungumzia miaka ya 20+ walai ningenasa mtu kibao. Lakini ndo hivyo binadamu tumeumbwa kusahau
 

nahisi hapa nimekuelewa vizuri kuliko thread yako!

ukweli ni huu, customer care ya watanzania ni mbovu haina kifani, sio kwenye ndege peke yake bali katika kila sehemu, kila sector kwa ujumla wake!

ushauri:
ukiwa tanzania hasahasa mtu unaefanya deals mbalimbali za kufanya ukutane nao mara kwa mara KAMWE usitegemee huduma nzuri kwa namna yoyote ile, bali cha kufanya chukulia km kupata huduma nzuri ni bahati kwako, otherwise kila siku utakuwa unakuja na mikasa isiyoisha unayosababibishiwa na watz! mm pia ni mtanzania na haya nayaandika kwa niaba yao!

take it from me!
 
RedDevil, ungejua nilivyokuwa nimekasirika usiku huo baada ya majibu ya huyo mwakilishi wao, kwa kweli hilo sikulifikiria kabisa kuongea na mtu yeyote kutoka Fastjet na hata leo hii hamu sina kabisa.

Tiba
Pole sana Tiba, ila ni vyema, hata kama hutatumia usafiri wa FastJet tena, uende kwa top boss wao hapa nchini ueleze mkasa wote huo. Unajua sisi Waafrika mtu akiwa kwenye ofisi ya kutoa huduma anajiona sijui kama kitu au mtu gani! Ule wajibu wake anakuwa haujui; even if huwezi kumsaidia mtu kupata solution ya tatizo lake, hata namna unavyowasiliana na mteja wako inaweza kuwa msaada kwake! Aisee nenda Ofisi za FastJet utoe malalamiko haya labda itakua fundisho kwa wafanyakazi wengine wa kampuni hiyo, INAUMA SANA! POLE
 

Akili nyingine bana! Hivi wote mkifika 2 hours before mtaingia kwa wakati mmoja? 40 minutes before departure ndo wanafunga. Ina maana ukifika bado dakika 50 upo ndani ya muda
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…