FASTJET has taken over FLY 540 shares!

FASTJET has taken over FLY 540 shares!

kwa bei yao hiyo mpaka wamachinga wataweza kupanda ndege sasa...mbona airport itakua ni kazi kutakavokua kumejaa kila siku..
 
bana wee kuna wafanyabiashara wangapi hapa bongo hawalipi kodi? bora hawa wasilipe lakini watupe huduma rahisi kuliko wakimbie na hela yetu hivi hivi
 
TRA wamelala sana
kodi wanajua kuzikata kwenye mishahara ya wafanyakazi tu serikalinilakini wafanyakazi wa kigeni kwenye migodi au blokcs za gesi kule songosongo na mtwara hawaguswi.
pia wageni kwenye mahotel na mbuga hawaguswi mishahara yao
vyanzo vya mapato viko vingi sana kutoka kwa wageni na pato lingeongezeka
ni nani mfanyakazi wa TRA alie maskini? asie na vitega uchumi vya kumwaga?
we have to do something 2015 watakosa pa kukimbilia
sina shaka ile jet ya 540 ni mali ya fastjet tangu mwanzo kuna chezo umechezwa hapa kati ya serkali na wamiliki
 
watadumu sana kwanini wasidumu? wanatoa affordable price kwa consumers
sheria za ushindani haziruhusu usafiri wa anga kuungana kuwa na bei moja wanaita cartels is prohibited
ni kila kampuni na bei yake ili kumnufasha msafiri
watapata more customers, wataongeza idadi ya safari
na pia wataongeza ndege zingine kwa ajili ya mikoa kama kigoma,tabora,bukoba,mtwara na mbeya lets wait and see.
precission imekula kwao
nashauri makampuni mengine walete ndege zao zifanye kazi tz
mabasi yanachosha bwana,tren nayo iboreshwe za kwenda mikoani
itasaida bei za bidhaa kushuka. viva tz
 
Itasaidia sana kupunguza vifo vya kisharobaro..
 
Ni zile zilizokuwa 540 nipo uwanja wa mwanza airport najiandaa kuja dar kwa nje ni nzuri ngoja tusubiri huduma zao ndani tutawajuza.

mkuu hizo ndege zinabadili majina kama serena vile..
 
ngoja na si wengine tuonje radha ya ndege teh teh teh
 
Low cost African airline FastJet has confirmed it will have its first airbase in Tanzania.
fast.png

The airline will commence flying in November with seats going on sale online a few weeks earlier. Fares will be available from $20 one-way excluding taxes and charges.


The lease for FastJet’s first Airbus A319 aircraft has been signed with lessor BBAM and will arrive in Dar es Salaam next month. Recruitment for crew and ground staff is already well advanced, according to a statement released by the company.


FastJet Chief Executive Ed Winter said: “Our initial focus will be on East Africa with the airline’s first base at Dar es Salaam, Tanzania, where the A319 aircraft has already been approved by the Tanzania Civil Aviation Authority.

This will be followed by a second base in Nairobi, Kenya, once the A319 is approved there. We look forward to bringing a great, reliable and affordable service to the people of East Africa.”
Once established in East Africa, Fast Jet revealed it plans to launch in Accra, Ghana and Luanda Angola
 
Has made its first commercial maiden flight today.
We are hopeful!
 
hii itatusaidia kupunguza madereva wa mabasi wanaosababisha vifo vya abiria kwa makusudi!!!
watarudi mitaani tu kama hiyo offer ikiendelea hivyo hivyo kwa miaka mi 3 mbele
 
"Serikali corrupt haikusanyi kodi itabaki kukumbatia wenye mali na kufukuzana na wamachinga barabarani"--J.K Nyerere
 
Ni kweli ndiyo hao hao fly540, na ofisi ni zilezile. Huu utaratibu wa kubadilisha majina baada ya miaka mitano ili kukwepa kodi kuna vigogo serikali wanaofaidika nao. Ni baadhi ya matokeo ya sheria mbovu tulizonazo, na wabunge wetu wanafumba macho kama hawaoni. Jamani tunahitaji serikali za majimbo katika katiba mpya.

Hafadhari hao wameokoa wananchi hata sie wakinakaj**ba nani tutafaidi hizo fastjet otherwise tungeziona kwenye tv tu ndege.
 
Kama 540 imeshindwa kulipa kodi, hii ni dalili ya profitability crisis. Na kama ndivyo hivyo ni maarifa gani hawa wajanja wametumia kuona kwamba wakiingia sokoni kwa mitambo ya airbus na bei ya daladala wataondokana na tishio la lililowasumbua kwanza? Wakuu wenye utaalam nisaidieni. Ni kwa namna gani hizi ndege zitaweza kujiendesha kwa nauli za mabus? Ndege hizi zinauwezo wa kuzunguka Mwanza Dar mara ngapi kwa siku bila kuhitaji service na ili kuhakikisha zinasafirisha abiria wengi kukidhi gharama za uendeshaji na hata kuacha kafada japo kadogo? Wajuzi naomba mnijuvye na wasioelewa kama mimi. Hivi kama gharama za uendeshaji ndege zinaweza kuwa reasonable kiwango hiki kinachoelelezwa na fast jet, kwa nini makampuni ya ndege mengine ikiwemo ATC na Precission wanacharge nauli za kiyama? Naona mambo mengi ni kiini macho macho vile!
 
Back
Top Bottom