ZionTZ
JF-Expert Member
- Oct 6, 2009
- 1,282
- 541
Chukueni taadhari wakuu mnapoenda kula pale fastfood Sinza kwa Remmy. Yaani wale wahudumu ni wezi wote kasoro mzee mmoja wa makamo hivi nahisi atakua Mhaya kutokana na lafudhi yake.
Wanaibaje?
Wewe ukienda wanakupokea pale counter alafu unatoa oda yako afu unaenda kukaa baadae wanakuletea. Ukimaliza anakuja anajifanya anaandika andika kwenye kikaratasi flani kwa mwandiko wa mcharango hivi afu anakutajia bill kubwa kuliko uhalisia.
Mimi nligundua baada ya kuwa nakula chakula kimoja kwa siku tatu mfululizo na wahudumu tofaut kila siku napata bill tofaut. Alafu ukitaka kujua bei halisi wewe ulizia palepale counter wale hawana cha kukuibia kwa sababu kazi yao ni kupakua chakula tu.
Kuna kadada pale kanaitwa Aisha na jamaa mwingine mweusi hivi kama Mkurya hao ndo wezi hatari. Hili swala lina baraka kabisa kwa uongozi wao kwa sababu kila mara nauliza Menu hawanipi wala ubao wa bei hamna.
Mi naomba kwa yeyote mwenye connection na uongozi wao awafikishie hii habari, wengi wanalalama sana. Tena wakikuona umekuja na wife ndo balaa!
Sio tabia nzuri kabisa.
Wanaibaje?
Wewe ukienda wanakupokea pale counter alafu unatoa oda yako afu unaenda kukaa baadae wanakuletea. Ukimaliza anakuja anajifanya anaandika andika kwenye kikaratasi flani kwa mwandiko wa mcharango hivi afu anakutajia bill kubwa kuliko uhalisia.
Mimi nligundua baada ya kuwa nakula chakula kimoja kwa siku tatu mfululizo na wahudumu tofaut kila siku napata bill tofaut. Alafu ukitaka kujua bei halisi wewe ulizia palepale counter wale hawana cha kukuibia kwa sababu kazi yao ni kupakua chakula tu.
Kuna kadada pale kanaitwa Aisha na jamaa mwingine mweusi hivi kama Mkurya hao ndo wezi hatari. Hili swala lina baraka kabisa kwa uongozi wao kwa sababu kila mara nauliza Menu hawanipi wala ubao wa bei hamna.
Mi naomba kwa yeyote mwenye connection na uongozi wao awafikishie hii habari, wengi wanalalama sana. Tena wakikuona umekuja na wife ndo balaa!
Sio tabia nzuri kabisa.