Familia yakamatwa kwa kuozesha watoto wa miaka 12 na 16

BigTall

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
422
1,049
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara linawashikilia watu saba, wakiwamo wanafunzi wawili wa Shule ya Msingi Kitarungu Wilayani Sereni kwa tuhuma za kuhusika kufanikisha ndoa ya wanafunzi hao wenye umri wa miaka 12 na 16 kinyume cha sheria.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Longinus Tibushubwamu alisema watu hao wamekamatwa cha Getarungu baada ya polisi kupata taarifa za kiintelijensia.

Alisema nyumbani kwa wazazi wa bwana harusi' kulikokuwa na sherehe za ndoa. Aliwataja katika tukio hilo lililotokea wilayani Seren katika Kijiji polisi walifika wanaoshikiliwa Aprili 2 kuwa ni Nyang'ombe Magere (50) na Ghati Masero (38) ambao ni wazazi wa mtoto wa kiume aliyekuwa anaozwa.

Mwingine anayeshikiliwa ni Kibaki Rioba (23) mkazi wa Sirari Wilaya ya Tarime pamoja na watoto wenye umri wa miaka 12 na 16 waliokuwa wanaoana.

Polisi pia inamshikilia msimamizi wa ndoa hiyo batili kwa upande wa mwanamume ambaye pia ni mtoto mwenye umri wa miaka 10 (jina limahifadhiwa), darasa la pili Shule ya Msinggi Kitarungu," alisema Kamanda Tibushubwamu.

Akizungumza kwa sharti la kuhifadhiwa jina lake, mkazi mwanafunzi wa Kijiji cha Kitarungu alisema wazazi wa mtoto wa kike (16) anayesoma darasa la saba walipokea mahari ya ng'ombe Sita kutoka upande wa mwanamume ambaye ni mwanafunzi (12) wa darasa la nne.

Alisema baada ya wazazi wa mtoto wa kike kupokea mahari, walimkabidhi binti yao kwa mume wake mtarajiwa, maandalizi ya sherehe yakaanza nyumbami kwao mwanamume.

"Baada ya taarifa hizo kufika polisi, askari walivamia sherehe hiyo na kuwatia mbaroni watuhumiwa," alisema mtopa taarifa huyo.

Juliana Kobiro ambaye ni mdau wa haki za watoto mjini Musoma alilipongeza Jeshi la Polisi kwa kuchukua hatua za haraka kudhibiti uvunjifu wa sheria na haki za watoto ulio karibia kufanyika, huku akiomba wahusika wote wachukuliwe hatua za kisheria ili iwe fundisho kwa wengine.

Chanzo: Mwananchi
 
Mtoto wa std 4 anataka kumkula mdada wa std 7 tena kihalali,
Dunia simama nishuke, hivi huyo mtoto hata shahawa anazo kweli? Au alikua anataka kumjaza mwenzie mikojo yake.
Hatari na nusu.
 
Mtoto wa std 4 anataka kumkula mdada wa std 7 tena kihalali,
Dunia simama nishuke, hivi huyo mtoto hata shahawa anazo kweli? Au alikua anataka kumjaza mwenzie mikojo yake.
Wavulana wngine wanakua wamebalehe kwa umri huo.
Huko England kuna mwalimu alipewa mimba na mwanafunzi wa kiume mwenye miaka 12,.... hii kesi ilishtua watu sana. Ila.kumbe walikua na mahusiano na ikawa hivyo
 
Wavulana wngine wanakua wamebalehe kwa umri huo.
Huko England kuna mwalimu alipewa mimba na mwanafunzi wa kiume mwenye miaka 12,.... hii kesi ilishtua watu sana. Ila.kumbe walikua na mahusiano na ikawa hivyo
Sasa huko ulaya n sawa, sio huku kwa wamatumbi lol.
 
Hivi huko Sereni bado wapo zama za giza hivyo jamani watu tunaenda mbele wao wanarudi nyuma
 
Hawa ndio wale kina Vita ni Vita Muraaaa.Jaman kuna mura mmoja hapa mjin nishaingia mkenge nina mimba yake basi km mambo yenyewe ndio haya nijipange tu.
 
Sheria ifuate mkondo wake. Wasukumizwe ndani wote waliohusika.
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara linawashikilia watu saba, wakiwamo wanafunzi wawili wa Shule ya Msingi Kitarungu Wilayani Sereni kwa tuhuma za kuhusika kufanikisha ndoa ya wanafunzi hao wenye umri wa miaka 12 na 16 kinyume cha sheria.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Longinus Tibushubwamu alisema watu hao wamekamatwa cha Getarungu baada ya polisi kupata taarifa za kiintelijensia.

Alisema nyumbani kwa wazazi wa bwana harusi' kulikokuwa na sherehe za ndoa. Aliwataja katika tukio hilo lililotokea wilayani Seren katika Kijiji polisi walifika wanaoshikiliwa Aprili 2 kuwa ni Nyang'ombe Magere (50) na Ghati Masero (38) ambao ni wazazi wa mtoto wa kiume aliyekuwa anaozwa.

Mwingine anayeshikiliwa ni Kibaki Rioba (23) mkazi wa Sirari Wilaya ya Tarime pamoja na watoto wenye umri wa miaka 12 na 16 waliokuwa wanaoana.

Polisi pia inamshikilia msimamizi wa ndoa hiyo batili kwa upande wa mwanamume ambaye pia ni mtoto mwenye umri wa miaka 10 (jina limahifadhiwa), darasa la pili Shule ya Msinggi Kitarungu," alisema Kamanda Tibushubwamu.

Akizungumza kwa sharti la kuhifadhiwa jina lake, mkazi mwanafunzi wa Kijiji cha Kitarungu alisema wazazi wa mtoto wa kike (16) anayesoma darasa la saba walipokea mahari ya ng'ombe Sita kutoka upande wa mwanamume ambaye ni mwanafunzi (12) wa darasa la nne.

Alisema baada ya wazazi wa mtoto wa kike kupokea mahari, walimkabidhi binti yao kwa mume wake mtarajiwa, maandalizi ya sherehe yakaanza nyumbami kwao mwanamume.

"Baada ya taarifa hizo kufika polisi, askari walivamia sherehe hiyo na kuwatia mbaroni watuhumiwa," alisema mtopa taarifa huyo.

Juliana Kobiro ambaye ni mdau wa haki za watoto mjini Musoma alilipongeza Jeshi la Polisi kwa kuchukua hatua za haraka kudhibiti uvunjifu wa sheria na haki za watoto ulio karibia kufanyika, huku akiomba wahusika wote wachukuliwe hatua za kisheria ili iwe fundisho kwa wengine.

Chanzo: Mwananchi
Hivi mkoa wa Mara umelaaniwa kuwa na matukio ya hajabu hajabu tu kila uchwao?
 
Nafikiri sheria tu haitoshi , jamii ipewe elimu na wajue madhara ya ndoa changa. Hiyo imeshikwa jamii imejua. Tunafikiri ni ndoa ngapi za namna hiyo zimefanyika kimya kimya ?
 
Back
Top Bottom