Familia John Heche yasema, haiko tayari kuona ndugu yao akipoteza maisha bila sababu ya msingi kwa sababu ndugu yao hana makosa

Familia John Heche yasema, haiko tayari kuona ndugu yao akipoteza maisha bila sababu ya msingi kwa sababu ndugu yao hana makosa

Mafyangula

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2025
Posts
505
Reaction score
887
Polisi polisi na Serikali ya Samia mbona mnazidi kutengeneza chuki zaidi kwa Watanzania, Hivi hivi utasikia Heche haonekani tena au kafungulia kesi nzito ilimradi tu wahodhfishe CHADEMA. Hii si sawa.
==================
Wakati Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kikihoji alipo Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Bara, John Heche, familia ya kiongozi huyo imetoa muda wa siku moja kwa Jeshi la Polisi kueleza alipo ndugu yao kabla hawajaamua kumtafuta wao wenyewe kwa kushirikiana na wananchi.

Uamuzi huo umefanywa na familia hiyo kufuatia kuwepo wa taarifa kuwa Heche alisafirishwa kutoka Dar es Salaam kwenda Tarime lakini hadi sasa bado hajafikishwa na wala hawana taarifa kuhusu ndugu yao huku wakidai kuwepo kwa danadana kutoka mamlaka mbalimbali.

Soma Pia: John Heche akamatwa akiwa Mahakama Kuu akijiandaa kuhudhuria kesi ya Tundu Lissu

Heche alikamatwa jana Oktoba 22, 2025 jijini Dar es Salaam katika viunga vya Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, alipokwenda kusikiliza kesi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu.

Kabla ya kukamatwa, Idara ya Uhamiaji Makao Makuu, ilitoa taarifa ikidai kwamba Heche alivuka mpaka kinyume cha sheria, madai ambayo Heche mwenyewe alikanusha na kudai kwamba alikuwa nyumbani kwake Tarime mkoani Mara.

Leo, Oktoba 23, 2025, familia ya Heche iliyopo Kijiji cha Ketagasembe wilayani Tarime, imesema wameamua kutoa muda huo ili kuonyesha namna gani walivyo wavumilivu na kwamba hawataki kuzua taharuki yoyote.

Mdogo wa Heche, Chacha Heche amesema familia haiko tayari kuona ndugu yao akipoteza maisha bila sababu ya msingi kwani wanaamini kuwa ndugu yao hana makosa ya aina yoyote, zaidi amekuwa mstari wa mbele kudai haki na demokrasia kwa ustawi wa nchi na watu wake.
 
Kama Samia na Genge wamedhamiria kuitawala Tanzania kwa njia hii; basi kuna mawili.

Moja ni kwa waTanzania wakubali tu kuvumilia kila uonevu wanaofanyiwa, au waTanzania sasa waamue kwa dhati kabisa kupambana na udhalimu wa namna hii.

Inaweza kuchukuwa muda na maumivu mengi, lakini na wao hawatatawala kwa raha. Kuna njia nyingi sana za kuwafanya watawale kwa shida kubwa sana.
 
Watanzania sisi ni wagumu sana wa kuelewa! Hizi kadhia zote zinazofanywa na mapolisi ni ku-provoke wananchi ili waamue liwe na liwalo! Sasa na Sisi tumebaki tunapiga ngonjera tu! Mapolisi wanatamani nchi iingie kwenye machafuko!
 
familia ya kiongozi huyo imetoa muda wa siku moja kwa Jeshi la Polisi kueleza alipo ndugu yao kabla hawajaamua kumtafuta wao wenyewe kwa kushirikiana na wananchi.
Siku 1 watawapa wanachosubiria wao ni kuwaona mtafanya nini baada ya hio siku 1 mtachoma vituo vya polisi? Na kuwakaanga polisi mmoja mmoja na risasi zao wenyewe au mtaenda kuchoma Ikulu?
 
Kama Samia na Genge wamedhamiria kuitawala Tanzania kwa njia hii; basi kuna mawili.
Moja ni kwa waTanzania wakubali tu kuvumilia kila uonevu wanaofanyiwa, au waTanzania sasa waamue kwa dhati kabisa kupambana na udhalimu wa namna hii.
Inaweza kuchukuwa muda na maumivu mengi, lakini na wao hawatatawala kwa raha. Kuna njia nyingi sana za kuwafanya watawale kwa shida kubwa sana.
Sisi watanzania ni mafala! Wewe nchi imejaza mataahira kama Clemence Mwandambo unafikri tutatoka?
 
Polisi polisi na Serikali ya Samia mbona mnazidi kutengeneza chuki zaidi kwa Watanzania, Hivi hivi utasikia Heche haonekani tena au kafungulia kesi nzito ilimradi tu wahodhfishe CHADEMA. Hii si sawa.
==================
Wakati Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kikihoji alipo Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Bara, John Heche, familia ya kiongozi huyo imetoa muda wa siku moja kwa Jeshi la Polisi kueleza alipo ndugu yao kabla hawajaamua kumtafuta wao wenyewe kwa kushirikiana na wananchi.

Uamuzi huo umefanywa na familia hiyo kufuatia kuwepo wa taarifa kuwa Heche alisafirishwa kutoka Dar es Salaam kwenda Tarime lakini hadi sasa bado hajafikishwa na wala hawana taarifa kuhusu ndugu yao huku wakidai kuwepo kwa danadana kutoka mamlaka mbalimbali.

Soma Pia: John Heche akamatwa akiwa Mahakama Kuu akijiandaa kuhudhuria kesi ya Tundu Lissu

Heche alikamatwa jana Oktoba 22, 2025 jijini Dar es Salaam katika viunga vya Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, alipokwenda kusikiliza kesi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu.

Kabla ya kukamatwa, Idara ya Uhamiaji Makao Makuu, ilitoa taarifa ikidai kwamba Heche alivuka mpaka kinyume cha sheria, madai ambayo Heche mwenyewe alikanusha na kudai kwamba alikuwa nyumbani kwake Tarime mkoani Mara.

Leo, Oktoba 23, 2025, familia ya Heche iliyopo Kijiji cha Ketagasembe wilayani Tarime, imesema wameamua kutoa muda huo ili kuonyesha namna gani walivyo wavumilivu na kwamba hawataki kuzua taharuki yoyote.

Mdogo wa Heche, Chacha Heche amesema familia haiko tayari kuona ndugu yao akipoteza maisha bila sababu ya msingi kwani wanaamini kuwa ndugu yao hana makosa ya aina yoyote, zaidi amekuwa mstari wa mbele kudai haki na demokrasia kwa ustawi wa nchi na watu wake.

Short and clear:

"imetoa muda wa siku moja kwa Jeshi la Polisi kueleza alipo ndugu yao kabla hawajaamua kumtafuta wao wenyewe kwa kushirikiana na wananchi."

Mwarobaini pekee wa kumaliza tatizo la utekwaji na kumrejesha mateka awaye yote!
 
Nchi inaongozwa na genge la Mafia. Polisi hawafuati sheria, taratibu, miongozo yao. Hawajali kabisa haki za msingi za raia.

Mtu maarufu, high profile kama Heche unamchukua hadharani zaidi ya masaa 24 chama chake, mawakili wake, ndugu zake bado hawajapewa taarifa alipo, hali yake ikoje na kosa lake ni lipi.
 
Watanzania sisi ni wagumu sana wa kuelewa! Hizi kadhia zote zinazofanywa na mapolisi ni ku-provoke wananchi ili waamue liwe na liwalo! Sasa na Sisi tumebaki tunapiga ngonjera tu! Mapolisi wanatamani nchi iingie kwenye machafuko!
Hayaelewi acha tuyafinye
 
Kwahaya Jeshi La Polisi Linaweza Kuwa Linafanyakazi Zake Kwa Uweredi?

Nabado Watu Wakawa Wanaamin Hivyo Wanatoa Huduma Nzuri Kwa Wananchi?

Mambo Mengine Wanaleta Wenyewe Kuleta Taharuki Tuu Kwan Kunattz Gan Kutoa Taarifa Sehemu Alipo
 
Nchi inaongozwa na genge la Mafia. Polisi hawafuati sheria, taratibu, miongozo yao. Hawajali kabisa haki za msingi za raia.

Mtu maarufu, high profile kama Heche unamchukua hadharani zaidi ya masaa 24 chama chake, mawakili wake, ndugu zake bado hawajapewa taarifa alipo, hali yake ikoje na kosa lake ni lipi.
Vuta picha ungeshikwa wewe au Mimi? Kwa Sasa polisi ndio wamekua hatari zaidi ya majambazi
 
Ila wanaume wa Dar makunguru sana mnaruhusu vipi mtu kukamatwa kiboyaboya mpo mnaangalia

Wanasubiri kukombolewa. Vipigo vya kionevu mahakamani ilithibitika. Ni heri wanawake kuliko hata kina Lema!

Bure kabisa!
 
Vuta picha ungeshikwa wewe au Mimi? Kwa Sasa polisi ndio wamekua hatari zaidi ya majambazi
Mtu wa kawaida inawezekana usionekane tena. Samia anasema nchi ina amani. Tusivuruge amani ya nchi.

Ukitekwa kama hivi usipige kelele kudai haki yako. Familia, ndugu, jamaa, marafiki, raia wakipiga kelele kudai haki itendeke Samia atakwambia kufanya hivyo kuvunja amani.
 
Sasa mtu anachukuliwa mahakama kuu kumepambazuka kabisa halafu wanaomchukua mnawaangalia tu halafu tunakuja kwenye mitandao kulalamika huu ujinga
Wa sirari walipambana juzi kuzuia mtu asichukuliwe na walifanikiwa kuhakikisha anapelekwa kituoni na taarifa ikatolewa, hata hivyo matokeo yake baadhi yao wapo rumande hadi leo. Mambo sio mepesi kama unavyoeleza hapa.
 
Heche atasahaulika kama polepole

Siyo kwa msimamo wa wanaume wa ukweli huu:

"imetoa muda wa siku moja kwa Jeshi la Polisi kueleza alipo ndugu yao kabla hawajaamua kumtafuta wao wenyewe kwa kushirikiana na wananchi."

Uanaume, si suruali!
 
Back
Top Bottom