Fainali ya CAFCC hiiiiiyo inawasubiri Simba

Fainali ya CAFCC hiiiiiyo inawasubiri Simba

DELETED ACCOUNT

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
9,805
Reaction score
15,470
Baada ya mechi ya kwanza ya nusu fainali dhidi ya Al Masry, nilikumbushia kwamba Simba ina tatizo sugu la kuleta ugumu pale njia rahisi inapokuwa mbele yake.

Simba ndiyo wakali wa hizi kazi, inafuzu kwenda nusu fainali vizuri tu

Nilichokuwa nina uhakika nacho ni kuwa Simba ingeenda kusahihisha makosa nikiwa na uhakika wa kucheza nusu fainali. Na kweli hilo lilitimia, Simba ilicheza mpira mkubwa sana na kutawala mchezo ila hali ya uwanja na tatizo la kutotumia vizuri nafasi likapelekea ushindi usubiri hatua ya penati.

Simba inapoenda kurudiana na Stellenbosch baada ya kupata ushindi wa goli 1-0 ni kwamba nafasi ya Simba kufuzu ni kubwa sana. Hii ni kwa sababu matokeo mengi yanayowezekana siku hiyo yana faida kwa Simba. Matokeo ya South Africa ya 0-0, 1-1, 2-2, 2-1 Simba anavuka moja kwa moja. Hata Stellenbosch ikishinda 1-0 tunaenda kwenye matuta. Hapa utaona Simba ina nafasi zaidi ya kuvuka kuliko kutolewa.

Kwenda kwao na mtaji wa 2-0 ingekuwa bora zaidi ila pia ni kama nilivyosema kwa Al Masry, haya matokeo magumu kwa Simba yana faida zake za kuifanya timu isibweteke katika mechi ya marudiano.

Niliwahi pia kusema hawa Stellenbosch hawana mentality ya kutegemea sana uwanja wa nyumbani kama timu nyingi zenye uzoefu wa mpira wa Africa. Jinsi walivyocheza mechi ya kwanza ndiyo hivyo hivyo watacheza huko kwao. Hawa jamaa ni hatari zaidi wakiwa ugenini kuliko hata nyumbani kwao kama nikivyosema katika uzi huu.

Stellenbosch ni hatari zaidi wakiwa ugenini

Simba inahitaji kuwa na nidhamu kubwa eneo la ulinzi kama iliyoonyesha jana na kuwa na utulivu na ushirikiano kwenye kiungo na safu ya mbele. Kwa nafasi nyingi ambazo Simba inatengeneza, uhakika wa kupata goli kule kwao ni mkubwa na hawana timu ya kumfunga Simba goli 3 au zaidi ndani ya dakika 90.

Mziki tuliowachezea jana siyo wa kitoto. Ni vile tu tukio la mwisho la Ahoua limetuvuruga hadi tumesahau jinsi tulivyotawala mchezo na makanzu na matobo tuliyowapiga. Angalia sura zao baada ya mechi ya jana, wanajua ugumu wa mechi ya marudiano kule kwao.
 
Mpanzu akiwa na Mpira ndio unaona angalau Goli linaweza kutokea.
Lakini sio Mcezaji mwingine Yoyote yule.

Tatizo ni Quality kaka.
Quality inakataa, Tunatembea na Bahati tu.

Kila Level ina wachezaji wake kuanzia.
Mtoano.
Makundi.
Robo Fainali.
Nusu Fainali na
Fainali.

Wachezaji wengi wa Simba ni wachezaji wa makundi shirikisho CAFCC sio CAFCL.
 
Mimi roho inaniuma kwa kushinda goli moja nyumbani, nafasi tulizopata na tukashindwa kumalizia tu, zikichagizwa na ile ya mwisho ya Aohua sina amani moyoni mwangu pamoja tumeshinda goli moja.
 
Mimi roho inaniuma kwa kushinda goli moja nyumbani, nafasi tulizopata na tukashindwa kumalizia tu, zikichagizwa na ile ya mwisho ya Aohua sina amani moyoni mwangu pamoja tumeshinda goli moja.
Hilo tatizo la kupoteza nafasi inaonyesha inabidi tuishi nalo tu hadi mwishoni mwa msimu. Tukipata hata kidogo tushukuru ila usiwe na wasiwasi, tunaenda fainali vizuri tu.
 
Kupoteza nafasi za wazi ni tatizo sugu.
Inshallah kule south tukipata goli la mapema kabla yao tutawanyong'onyesha.
 
Simba bingwa? Pira biriani la Berkane mmeliona lakini?
 
Hilo tatizo la kupoteza nafasi inaonyesha inabidi tuishi nalo tu hadi mwishoni mwa msimu. Tukipata hata kidogo tushukuru ila usiwe na wasiwasi, tunaenda fainali vizuri tu.
Naona Berkane ana hasira vibaya mno, tuanze kumwangalia kwa jicho la ziada hiyo fainali
 
Naona Berkane ana hasira vibaya mno, tuanze kumwangalia kwa jicho la ziada hiyo fainali
Wana timu nzuri ila naona tunawamudu. Tuzingatie fitness ya wachezaji na tuepuke au kupona majeraha. Zitakuwa mechi mbili za kupishana sana.

Tukivuka, tusikubali TFF watujazie mechi za mfululizo kipindi hiki kabla ya fainali. Zitatugharimu.
 
Mimi ni mpenda soka Africa Sina timu nashabikia Liverpool na Barcelona tu Kwa nilivyoangalia ule mpira wa Jana simba hafiki fainali anaenda kutolewa south Africa
 
Mpanzu akiwa na Mpira ndio unaona angalau Goli linaweza kutokea.
Lakini sio Mcezaji mwingine Yoyote yule.

Tatizo ni Quality kaka.
Quality inakataa, Tunatembea na Bahati tu.

Kila Level ina wachezaji wake kuanzia.
Mtoano.
Makundi.
Robo Fainali.
Nusu Fainali na
Fainali.

Wachezaji wengi wa Simba ni wachezaji wa makundi shirikisho CAFCC sio CAFCL.
Mpunguzieni Mpanzu sifa, mpira wa anao anao hauisaidii Simba. Mpanzu ni Kibu asiye na nguvu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom