Fainali ya CAF Simba na Serikali wamefeli

Fainali ya CAF Simba na Serikali wamefeli

Username 20

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2017
Posts
741
Reaction score
1,513
Hii mechi imekuwa na sintofahamu nyingi ni wapi itafanyika, Caf walishatoa ratiba Simba wanalijua hilo na TFF wanayo taarifa kamili ni wapi mchezo huo utafanyika

Maajabu ni kwamba Simba na TFF ni kama wanaisaidia serikali kupoteza ukweli kuwa uwanja wa Benjamin Mkapa ni mbovu sehemu ya kuchezea (pitch) kwa ubovu ule uliooneka siku ya mechi ya marudio ya robo fainali kati ya Simba dhidi ya Al Masry haingekuwa rahisi hivyo kufanya marekebisho ndani ya mwezi mmoja

Simba imewakosea sana mashabiki zake, imekubali kutumika kupoteza uchafu wa serikali,
Caf waliufanyia marekebisho makubwa uwanja wa Mkapa kwa ajiri ya African Footbali League, ajabu eti serikali tena ikatoa bilioni 30 kwa ajili ya marekebisho na ukiangalia hakuna kilichofanyika zaidi ya kurekebisha mfumo wa umeme, wifi (haifanyi kazi yoyote mpaka sasa) na kubadili viti(wametoa vya zamani ambavyo vingeweza kuendelea kutumika bado) na hapo bil. 30 ndo ikawa imeishia

Narudia tena kusema Simba imewakosea sana mashabiki wake wanajua ratiba kamili ya wapi mchezo utafanyika wamekubari kuwa sehemu ya ulaghai wa serikali na mbaya zaidi wamekuwa wakiendelea kusisitiza watu wanunue tiketi, kivyovyote vile hakuna uwezekano wa mchezo kufanyika Benjamin Mkapa na wao wanajua kwanini wameruhusu hili?
Kwa mazingira yale ya mchezo wa robo fainali mnadhani ndani ya mwezi mmoja ingewezekana uwanja kufanyia warekebisho? Uwanja ule unatakiwa kuondolewa tabaka la juu (udongo) isingewezekana ndani ya mwezi mmoja hizi ni propaganda za serikali na Simba imetumka kwenye hili, uwanja wa mkapa ni mbovu na hauna vigezo vya kuandaa mchezo wa fainali

Wacha tusubiri mda ufike Simba kwa unyonge wajifanye kama wamezulumiwa na Caf (wakati walijua mapema na ukweli wanaujua kuhusu uwanja wa Benjamin Mkapa)
 
Fainali itafanyika Zanzibar.
NEW AMANI COMPLEX.

Watanganyika tumenyimwa Fursa ya kuangalia Fainali.

RIP MWALIMU JK NYERERE.
JPM, SOKOINE.
MKAPA.
 
Fainali itafanyika Zanzibar.
NEW AMANI COMPLEX.

Watanganyika tumenyimwa Fursa ya kuangalia Fainali.

RIP MWALIMU JK NYERERE.
JPM, SOKOINE.
MKAPA.
Zanzibar pia ni sehem ya Tanzania lkn kwann serikali imetenga kiasi cha bil. 30 na bado uwanja ukawa na ubovu ule
 
Inatia hasira sana, Caf walitoa taarifa mapema sana na Simba walikuwa wanajua hilo lkn wakaendwlea kusisitiza watu wakate tiketi, ule uwanja ni mbovu
Na mashabiki WA Simba wanaendelea kudanganywa kwa barua feki nk. Lkn hawastuki 😎
 
Fainali itafanyika Zanzibar.
NEW AMANI COMPLEX.

Watanganyika tumenyimwa Fursa ya kuangalia Fainali.

RIP MWALIMU JK NYERERE.
JPM, SOKOINE.
MKAPA.
Kwan kuna umbali gani hapo wa watu kushindwa kwenda kuangalia mechi? Watu wanatoka hadi Sumbawanga hadi Dar kwenda kuangalia mechi sembuse hapo Zanzibar.

Pitch imeonekana ina kasoro ikinyesha mvua tokea mechi dhidi ya Al Masry kwa mpira kukosa radha kwa matope leo mnataka CAF wawafate ujinga wa Watanzania ili fainali ionekane ya hovyo

Kwa jinsi akili za viongozi, wachezaji na mashabiki wanavyolilia huo uwanja inatoa picha kamili kuwa kuna siri nzito sana ya mambo ya nje ya uwanja hutumiwa na klabu ya Simba kwaajili ya kupata matokeo.
 
Hivi bil 30 haiwezi jenga uwanja wa kawaida wenye kuingiza walau mashabiki 10,000 hadi 15,000?
 
Hatucheziii
 

Attachments

  • 1747676924248.jpg
    1747676924248.jpg
    318.1 KB · Views: 16
Tff ni majangili, Mechi wanafahamu haitachezwa Ben Mkapa, Mashabiki wanatangaziwa wanunue tiketi na wao kama wasimamizi wa mpira Wana angalia uo upuuzi.
Uu puuzi na wizi wa wazi unaendelea kufanyika na Tff imekua ikifumbia macho upuuzi wa aina hii kwa muda mrefu.
Mechi zina ghairishwa bila sababu za msingi mashabiki hawaombwi radhi, viingilio havirudishwi na wanaona jambo la kawaida kabisa.

Inatakiwa washitakiwe kwenye mahakama za kiraia kwa wizi wa fedha za umma labda watajua wajibu wao.
 
Inshu sio kuwa na uwanja wao tatizo hapa ni kwanini serikali imeruhusu uwanja ukawa na ubovu kiasi kile? Na kwa gharama ya bil. 30 ni hela yetu walipa kodi kwanini tusihoj

Inshu sio kuwa na uwanja wao tatizo hapa ni kwanini serikali imeruhusu uwanja ukawa na ubovu kiasi kile? Na kwa gharama ya bil. 30 ni hela yetu walipa kodi kwanini tusihoji hili?
Nikuambie kitu Serikali ilikuwa sahihi kufanya kufunga uwanja,,ila simba ndo walikuwa wanaforce ,,wacha ukarabati uendeleeee
 
Kuna wapuuzi wanaisingizia CAF bure, wakati uwanja wa Taifa unafanyiwa Siasa na Msigwa, kabla ya mechi ya nusu fainali, Msigwa alifanya propaganda nyiiingi lakini mvua ikamuumbua saizi pamoja na waziri wake plus PM naye naona kaingia kwenye mtego wanashinda Temeke.
 
Back
Top Bottom