Faida za tiketi za kielektroniki kwa wamiliki wa mabasi

Nonchalant

JF-Expert Member
May 10, 2015
293
388
Baadhi ya Malengo na faida mfumo wa ukataji wa tiketi za bus kielektroniki nchini



▪️Kuwa na udhibiti katika sekta ya usafirishaji.
Wasafirishaji kuwa na ushindani wenye tija, Mfano kwa sasa nauli zinazowaongoza ni za mwaka 2013 lakini hawazitumii. Basi la daraja la juu (luxury) anauza bei ya daraja la kati (semi luxury). Basi la daraja la kati (semi luxury) kuuza bei ya daraja la chini (ordinary)
Mfano. DAR-MWANZA semi luxury ni TZS 61400, Ordinary 42600. Kwa sasa mpiga debe/ wakala anauza semi luxury kwa nauli ya 45000 mmiliki anapewa 25000-35,000. Ordinary auze bei gani?

Mawakala na wapiga debe wanachukua fedha nyingi sana tena isiyolipiwa kodi ambayo alistahili kuipata mmiliki wa basi/mwekezaji.
NAULI

▪️Kwa sasa mpiga debe ni kama share holder wa mwekezaji. Ili hali halipi kodi, haweki mafuta, hanunui tairi, hanunui vipuli, na hana msaada wowote kwa mmiliki zaidi ya kukamata abiria wanaosafiri na kusema ni abiria wake.


▪️Kuwa na Udhibiti wa sekta pia, nauli zitadhibitiwa kutopandishwa hovyo au kushushwa kupita kiasi.
Nauli zinapopandishwa kupita viwango elekezi ni kosa kisheria na huumiza wananchi.


Pia zinaposhushwa kupita viwango elekezi humtia hasara mwekezaji kupelekea kufilisika na kufungwa kwa biashara. Wengi tumeona kampuni nyingi zinaanzishwa na kufa kutokana na kukosa udhibiti na kuwepo kwa ushindani usio kuwa na tija kwa wamiliki wa mabasi.
Ajabu ni kwamba wamiliki hawa nauli elekezi zinazotumika ni za mwaka 2013 na hazitumiki, wanatumia robo ya nauli mpaka nusu ya nauli elekezi kisha wanalalama kwa nini mafuta yanapanda nauli hazipandi! Fedha nyingi zinapotea kwa kukosa udhibiti hasa kwa wapiga debe na mawakala.

FLOAT:
▪️Hii inamwezesha mmiliki kupokea fedha yake kwa wakati. Tiketi yoyote itakayouzwa katika kituo chochote kwa wakala/mpiga debe/ofisi yoyote, pesa yote itakwenda kwa akaunti ya mmiliki bank muda huohuo.
Mmiliki ataidhibiti pesa yake wakati wote tofauti na ilivyo sasa

▪️Wakala atabaki na cash ambayo atapaswa kuirudisha kwenye float ili aweze kuendelea kuuza tiketi. Itawasaidia sana wamiliki kupata fedha zao kwa wakati kuondoa wizi na ubadhirifu unaofanywa na mawakala/wapiga debe.

▪️Lakini pia pesa zinapoenda bank cash flow yote ya mmiliki bank yake itatambua hivyo kumwezesha mmiliki kukopeshwa kwa urahisi.

▪️Kwa njia hii itafungua milango ya ajira kwa mawakala, madereva, makondakta, waasibu, mafundi n.k tena ajira zenye tija kuliko kuendelea kufanya udalali, na wizi wa kuwaibia wamiliki. Fedha yote ataipokea mmiliki na kuidhinisha ifanye kupanga matumizi kwa ajili ya kampuni yake.
Ajabu jingine kwa sasa wakala ndiye anayepokea fedha yote ya mmiliki, kuipangia matumizi kisha kuamua utume kiasi gani kwa mmiliki.

▪️Mmiliki wa basi au mwekezaji atakapotoa ajira rasmi, atawezesha wafanyakazi wake wote kulipa kodi (PAYE) ya serkali, hifadhi zao katika mifuko ya hifadhi ya jamii, na Mmiliki wa bus atalipa kodi stahiki pasipo kukadiriwa wala kuiibia serikali kwa sababu mapato yake yote yatajulikana

▪️Mmiliki hana ulazima wa kuweka float ya gari zima kama inavyosemekana yaani siti zote za bus. Kwani abiria watajinunulia tiketi wenyewe waapo nyumbani, kazini au mahala popote hivyo kiasi cha float kitakua ni kidogo sana baada siti kadhaa kununuliwa mtandaoni.

▪️Lakini pia sio lazima kuweka float ya siti zote. Wakala wa mmiliki anaweza kupewa kiasi kidogo cha float. Mfano kwa gari ya nauli ya tzs 30,000 wakala apewe Tzs 300,000 kwa masharti, mfano kila atakapouza siti 7 ambazo ni Tzs 210,000
arudishe cash aliyoipata katika namba yake ya float. Hii itarahisha sana badala kuweka mamilioni katika float kama wanavyodhani.

Suala la float ni la muda tu kwani litaondoka kabisa pale wananchi watakapofahamu namna kununua tiketi online wenyewe.

▪️NJIA NYINGINE ZISIZOMTAKA MMLIKI KUTUMIA FLOAT, ni kutoa bili kwa abiria anapokuja ofisini/kwa wakala atapewa bili ya tiketi yake alipe mwenyewe kwa kutumia mitandao ya MPESA, TIGOPESA, kwa control number/reference number/kumbukumbu namba. Baada ya malipo atapewa tiketi yake kwa kuprintiwa au sms.
Tasisi nyingi za kiserikali na binafsi zinatumia njia hizi kwa sasa mfano TRA, TANESCO, Bill za maji, Hospitali, bank, TANAPA, Maduka ya online n.k


Tunapomaswa sisi kama nchi kuondoa mifumo ya cash inayoleta na inayoendeleza urasimu, wizi katika maofisi na biashara zetu. Wananchi/wahitaji huduma wajilipie wenyewe kwa kutumia mitandao badala ya kwenda kupanga foleni kupata huduma.

TAKWIMU
▪️Serikali yetu itapata takwimu halisi katika seka ya usafirishaji, adadi ya bus zinazosafiri katika ruti fulani, idadi ya abiria wanaosafiri kwa siku/mwezi/mwaka hivyo kuweza kutoa kipaumbele katika utoaji wa huduma. Mfano kuongeza kuruhusu wawekezahi zaidi katika ruti/njia nyenye upungufu. Kipaumbele cha matengezo ya barabara au hata kuziboresha zaidi n.k


NJIA ZA KUNUNUA TIKETI YA BASI
▪️Namna mwananchi anavyoweza kujinunulia teketi awapo nyumbani/ofisini n.k


Bonyeza link
Tiketi Mtandao - Apps on Google Play


Pakua application ya tiketi mtandao kutoka playstore kisha tafuta unapotoka, unapokwenda na tarehe ya safari. utachagua basi, siti uipendayo na kufanya malipo.


Nitaonyesha njia nyingine hapo badaee


Baadhi ya route zinazopatikana katika tiketi mtandao kwa sasa
DAR ES SALAAM-DODOMA
DODOMA-DAR ES SALAAM
DAR ES SALAAM-MBEYA
DAR ES SALAAM-TANGA
DAR ES SALAAM-MTWARA
DAR-LINDI
TANGA-DAR ES SALAAM
TANGA-ARUSHA
TANGA-MOSHI
DODOMA-MOSHI
DODOMA-ARUSHA


Hizi ni baadhi tu,
Njia nyingine zitaongezwa hivi karibuni.


Wamiliki wengi wangependa kuona mfumo huu unafanya kazi ili waweze kupata udhibiti wa biashara zao na faida, kwachache wenye maslahi ya wizi, tena wasio na kampuni ya bus ndio wenye kukwamisha jambo hili lenye tija kwa taifa letu na wafanyabiashara wenyewe na wananchi.


Changamoto hutatuliwa....


TUIJENGE NCHI YETU.


Tutaendelea kuelimishana.......
 
Ifike mahali tuache nguvu ya soko/mahitaji yaongoze ubunifu.

Wamiliki wa mabasi hawataki huo utaratibu, wewe kuanza kuwapiga shule ya unazoziita 'faida' ni kama dhihaka kwao.

Muda ukifika, nguvu ya soko itawasukuma waanze kutumia utaratibu huo, kama tu vile baadhi ya mabasi yavyofanya sasa. Mf. Kimbinyiko
 
Nimepitia haraka haraka hapo umeweka taarifa nyingi kwamba mmiliki anapata faida maradufu (kama ni kweli kwanini mmiliki anakataa )?

Ukweli ni kwamba mwenye advantage kubwa hapa ni Serikali Mapato (na sababu hapa TRA tayari alikuwa anachukua, nadhani wamiliki maswali yao ni yafuatayo:-

Ubora wa system / mtandao (nadhani wote tunajua efficiency ya vitu vya serikali)

Pili kwenye hii system nadhani kuna players wanaongezeka (platform managers), huenda Latra pia wakataka fungu (per tickect) kwahio hizo percentages zitkazoongezeka per ticket nani atalipia ? (abiria ua mmiliki)

Na haya mambo ya bei elekezi kwamba luxury iwe ya juu alafu Luxury inauzwa chini (si ni kwa faida ya msafiri kupata cheaper rates ) na ndio hizo nyimbo tunaambiwa kila siku faida ya ushindani ni bei kushuka (au imebadilika)?

In short mkiwabana watu na hizi bei elekezi huenda quality ikashuka, kwanini mtu afanye investment ya kuvutia watu wakati hata bila kufanya wateja watakuja tu...
 
Maelezo mengiii lakini kaa ukijua huo mfumo watanufaika wale wenye abiria wa uhakika ambao kwa kiasi kikubwa hawahitaji wapiga debe kumbuka wamiliki hawalingani vipato na ulaxury wa magari so wale waliozoea kutegemea wapiga debe ndio unakuwa mwisho wao pili nauli hakuna atakae katisha 61000 mwanza utaona wote wanasajili gari zao kama ordinary ili waende sawa na vipato vya abiria wao sasa hawa ambao ndio ordinary wenyewe watampakia nani???
 
Nimepitia haraka haraka hapo umeweka taarifa nyingi kwamba mmiliki anapata faida maradufu (kama ni kweli kwanini mmiliki anakataa )?

Ukweli ni kwamba mwenye advantage kubwa hapa ni Serikali Mapato (na sababu hapa TRA tayari alikuwa anachukua, nadhani wamiliki maswali yao ni yafuatayo:-

Ubora wa system / mtandao (nadhani wote tunajua efficiency ya vitu vya serikali)

Pili kwenye hii system nadhani kuna players wanaongezeka (platform managers), huenda Latra pia wakataka fungu (per tickect) kwahio hizo percentages zitkazoongezeka per ticket nani atalipia ? (abiria ua mmiliki)

Na haya mambo ya bei elekezi kwamba luxury iwe ya juu alafu Luxury inauzwa chini (si ni kwa faida ya msafiri kupata cheaper rates ) na ndio hizo nyimbo tunaambiwa kila siku faida ya ushindani ni bei kushuka (au imebadilika)?

In short mkiwabana watu na hizi bei elekezi huenda quality ikashuka, kwanini mtu afanye investment ya kuvutia watu wakati hata bila kufanya wateja watakuja tu...
▪️TRA huchukua kodi yake mwisho mwaka, mapato-matumizi=Faida, kwenye faida Tra anachukua kodi yake hivyo hii ni win win kwa wote endapo watafanya biashara kubwa.
▪️system iko timamu, changamoto zinaweza kijitokeza na kutatuliwa kwa wakati
▪️Tozo zipo katika sekta zote nchini hivyo latra atachukua tozo yake kama ewura na wadhibiti wa sekta nyingine wanavyofanya
▪️sio lazima kutumia bei elekezi ila mmiliki atapaswa acheze na bei za daraja lake pasipo kuathiri bei ya daraja jingine. Hivyo punguzo la bei lipo kama kawaida.
 
Maelezo mengiii lakini kaa ukijua huo mfumo watanufaika wale wenye abiria wa uhakika ambao kwa kiasi kikubwa hawahitaji wapiga debe kumbuka wamiliki hawalingani vipato na ulaxury wa magari so wale waliozoea kutegemea wapiga debe ndio unakuwa mwisho wao pili nauli hakuna atakae katisha 61000 mwanza utaona wote wanasajili gari zao kama ordinary ili waende sawa na vipato vya abiria wao sasa hawa ambao ndio ordinary wenyewe watampakia nani???
Hapana hii itaongeza chachu ya wengi kuboresha na kufanya vizuri katika kutoa huduma zao.
Abiria wa gari za ordinary wapo watanunua kwa bei zao na kama mmiliki ataamu kutoa punguzo atafanya hivyo bila kuathiri biashara yake. Abiria wa semi luxury wapo mmiliki anaweza kutoa punguzo bila kuathiri biashara ya mwenye bus za ordinary.

Bus kuwa ordinary na jingine kuwa semi luxury vipo vigezo vya kuzingatia katika utoaji wa leseni
 
▪️TRA huchukua kodi yake mwisho mwaka, mapato-matumizi=Faida, kwenye faida Tra anachukua kodi yake hivyo hii ni win win kwa wote endapo watafanya biashara kubwa.
▪️system iko timamu, changamoto zinaweza kijitokeza na kutatuliwa kwa wakati
▪️Tozo zipo katika sekta zote nchini hivyo latra atachukua tozo yake kama ewura na wadhibiti wa sekta nyingine wanavyofanya
▪️sio lazima kutumia bei elekezi ila mmiliki atapaswa acheze na bei za daraja lake pasipo kuathiri bei ya daraja jingine. Hivyo punguzo la bei lipo kama kawaida.
Hakuna Player atakayeongezeka kwenye huu mfumo ?
System ipo vizuri kwa mujibu wako wewe (ni mara ngapi Bongo Sever zinakuwa down kuzidiwa na matumizi) ?

Au ndio haya mambo ya luku unanunua leo Units zinakuja keshokutwa ? (Au hio Haitokei)? Plan B ipo wapi ?

Kwa ufupi labda nikuulize hivi, baada ya huu mfumo wamiliki kulazimishwa kutumia, hakuna costs percentagewise zitaongezeka ?

Umesema wamiliki wanaukubali mfumo ni madalali na vishoka ndio hawataki (huenda ni kweli kwa sehemu kubwa) ila nimesikia TABOA wameonekana kuja juu (mimi nilidhani hiki ni chama cha wamiliki, au kina members vishoka na madalali)?

Hakuna anayepinga teknolojia (its the way forward) issue ni nani anahodhi that technology na kwa faida ya nani?
 
▪️Kwa sasa mpiga debe ni kama share holder wa mwekezaji. Ili hali halipi kodi, haweki mafuta, hanunui tairi, hanunui vipuli, na hana msaada wowote kwa mmiliki zaidi ya kukamata abiria wanaosafiri na kusema ni abiria wake.
😂
 
Dosari zake ni zipi?

Mimi nimeona wale wenye kipato duni hawatakuwa na nafasi ya ku negotiate wakapewa discount
 
Unasema mfumo mama ni wa Serikali (Why is it Necessary ) huenda tatizo linaanzia hapo..., Don't get me wrong mimi ni mjamaa and am all for Nationalization lakini inabidi tuamua moja either Privatisation au Nationalization sio tunakuwa vuguvugu (serikali inachukua vitu vinakuwa sub-par havina ufanisi / au inachukua vitu alafu inatoa tender kwahio mwisho wa siku ni kupeana shavu na kuongeza gharama za uendeshaji...

Pili umesema 2% inaongezeka (ataibeba nani ?) kama ni mmiliki huoni kwamba ataumia ?, kama ni mwananchi hapo anasaidiwaje kwa kumuongezea gharama ?

Tatu umesema technical errors huwa zipo (No kwenye dunia ya sasa hatuwezi tukakubali sub-par service kwamba ni kawaida..., Yaani inabidi hata tukiangalia ufanisi wa miaka kumi labda system ikiwa down labda ni sekunde mbili au dakika chache kwa miaka kumi...

Unadhani American Stock Exchange ingekuwa na mentality ya technical errors huwa zipo ingekuwa inapoteza ma-trillions mangapi?
 
Back
Top Bottom