Faida za mkojo wa sungura

Faida za mkojo wa sungura

Chifu mkuu

JF-Expert Member
Joined
Jan 6, 2025
Posts
846
Reaction score
884
FAIDA ZA MKOJO WA SUNGURA KWENYE
KILIMO
Sungura hufugwa kwa ajili ya kutupatia nyama
ambacho Ni kitoweo kizuri na muhimu Sana.
Hivyo wafugaji wengi Sana hujipatia kipato
kizuri kupitia ufugaji wa sungura.

Lakini sungura Wana umuhimu Sana kwenye
kilimo. Mkojo wa sungura una umhimu
mkubwa Sana kwenye kilimo. Hutumika Kama
MBOLEA na dawa pia. Matumizi ya MBOLEA za
viwandani Kama DAP, N.P.K pamoja na UREA
kwa muda mrefu huathiri rutuba ya udongo na
kuufanya udongo usifae kwa matumizi ya
kilimo.

Mkojo wa sungura huweza kutumika Kama
MBOLEA ya asili na rafiki kwa kilimo kwani
hudumisha na kuongeza rutuba ya udongo.
Mkojo wa sungura una virutubisho vingi vya
madini ya naitrojeni, phosforasi na kalsiamu na
potasiamu ambayo ndio mara nyingi huitajika
na mimea kwa ukuaji mzuri. Iwapo mkulima
atatumia Lita moja ya mkojo wa sungura kwa
Lita tano za maji asubuhi na jioni atapata
matokeo mazuri kwenye kilimo.

Mkojo wa sungura unatumika pia Kama dawa
ya kuua WADUDU waharibifu kwenye kilimo.
Iwapo mkulima atatumia Lita moja ya mkojo
wa sungura kwa Lita mbili au tatu za maji
ataweza kuua WADUDU waharibifu kwenye
kilimo. Hii Ni kwasababu mkojo wa sungura
una kiambata Cha ammonia ambacho huua
WADUDU Kama fangasi na bakteria. Hii pia
hutunza na kuhifadhi rutuba ya udongo.

Kwa mahitaji ya mkojo wa sungura tutafute:

0717 445411
0784 024 733

Pasua manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro.
 
Maelezo ni mzuri ila hizi taarifa zimekosekana:
  • Bei
  • Ujazo wa huo mkojo.

Kila lakheri Ndugu
Bei nitafute kwenye simu!
Ujazo nina madumu matano ya lita 20@ kwahiyo nina lita 100.
 
Maelezo ni mzuri ila hizi taarifa zimekosekana:
  • Bei
  • Ujazo wa huo mkojo.

Kila lakheri Ndugu
Ujazo nina lita 100 ( madumu 5 ya lita 20 @)
Bei kila lita ni tsh 20,000/= hadi 15,000/= inategemeana unataka Lita ngapi..Ukichukua nyingi unapunguziwa bei.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom