Faida ya kuwa SINGLE

Bedui la bongo

JF-Expert Member
Aug 24, 2018
297
306
Katika sayari hii ya dunia kuna baadhi ya watu wanakwambia mapenzi ndiyo yanayoiendesha dunia, hii ni kwa sababu asilimia kubwa ya watu wengi wametawaliwa na mawazo ya kimapenzi.

Pamoja na kuwapo kwa kundi hilo la watu wanaoamini hivyo lakini pia wapo baadhi ya watu huamini ya kwamba mapenzi hayana faida yeyote ile.

Kundi hili la watu hao hujikuta wakitoka kwenye mahusiano, na sababu zinazopelepekea wao waamini hivyo mara nyingi huwa zinatokana na maumivu ya kutendwa na mtu ambaye alikuwa anamuamini na leo hii hayupo na mtu huyo tena kwenye mahusiano.



1. Mtu anapokuwa single anakuwa na uhuru wa muda wa kufanya mambo yako binafsi pasipo kupelekeshwa na mtu yeyote yule. Uhuru huu wa muda ni ule wa kufanya mambo yake na ya kijamii pia.

2. Mtu ambaye yupo single unakuwa na uhuru pia wa kufanya kile inachokitaka/ anachokipenda. Unapokuwa kwenye mahusiano kunakosekana uhuru wa kufanya vitu uvipendavyo hii ni kwa sababu unaweza ukawa unapenda kufanya jambo fulani ila kwa kuwa upo kwenye mahusiano ya kimapenzi huyo mpenzi wako akakuzuia kufanya jambo hilo kwa kuwa jambo hilo halimpendezi.



3. Unapikuwa single unakuwa hauna hisia mpelekesho, hisia mpelekesho ni zile hisia za kimapenzi ambazo zinakufanya ifikiri sana kuhusu mambo yanayohusu mapenzi, kwa mfano hivi hujawahi ona mtu anakurupuka usiku wa manane anampigia simu mpenziwe? bila shaka umewahi kuona, hii ni tabia inayokwenda sambamba na kitu kinachoitwa wivu. Hivyo unapokuwa single unakuwa hauna wivu kwa sababu unakuwa hauna mtu ambaye anakufanya uwe hivyo.

4. Unapokuwa single hakuna lawama zinazohusu mahusiano ambazo zitakuwa zinakuhusu wewe. Unapokuwa kwenye mahusiano yapo malalamiko mengi ambayo yatakuwa upande wako, vitu kama kwanini hupokei simu yangu na mambo mengine kama hayo yatakuwa mbali na wewe.

5. Utaishi maisha marefu yenye mjumuiko wa amani ya moyo pamoja usiokuwa na bugudha wala makwaluzano ya aina yeyote ile.

6. Kila siku Utalala usingizi mzuri.

7 Faida nyingine ya kuwa single utaongeza mwenyewe.
 
Mkuu inategemeana me naona wakati mwingine kuwa kwenye mahusiano kunaweza kuwa na faida nyingi kama ukiwa na mtu sahihi.
1+1 = 2
Kuna nguvu unaweza kuwa umeongeza.
Au ukikutana na kimeo ndio unakuta umeongeza tatizo.
 
Faida nyingine ya Kuwa Single ni kwamba huko MBELENI utakuwa na "SAFARI ZA DUBAI" maana kila zigo litakolokatiza mbele utataka kulipiga na sio kila mda "utamkumbuka mwewe" kuna siku nyingine lazima "UTAUZA MECHI".
 
Sasa tatizo ndo uipate hiyo bahati ya kupata mtu sahihi
Mkuu inategemeana me naona wakati mwingine kuwa kwenye mahusiano kunaweza kuwa na faida nyingi kama ukiwa na mtu sahihi.
1+1 = 2
Kuna nguvu unaweza kuwa umeongeza.
Au ukikutana na kimeo ndio unakuta umeongeza tatizo.
 
Ujanani faida kama zote kwakuwa una nguvu na una uwezo wa kufanya lolote ndani ya uwezo wako na kwenda popote... Lakini fainali uzeeni
Katika sayari hii ya dunia kuna baadhi ya watu wanakwambia mapenzi ndiyo yanayoiendesha dunia, hii ni kwa sababu asilimia kubwa ya watu wengi wametawaliwa na mawazo ya kimapenzi.

Pamoja na kuwapo kwa kundi hilo la watu wanaoamini hivyo lakini pia wapo baadhi ya watu huamini ya kwamba mapenzi hayana faida yeyote ile.

Kundi hili la watu hao hujikuta wakitoka kwenye mahusiano, na sababu zinazopelepekea wao waamini hivyo mara nyingi huwa zinatokana na maumivu ya kutendwa na mtu ambaye alikuwa anamuamini na leo hii hayupo na mtu huyo tena kwenye mahusiano.



1. Mtu anapokuwa single anakuwa na uhuru wa muda wa kufanya mambo yako binafsi pasipo kupelekeshwa na mtu yeyote yule. Uhuru huu wa muda ni ule wa kufanya mambo yake na ya kijamii pia.

2. Mtu ambaye yupo single unakuwa na uhuru pia wa kufanya kile inachokitaka/ anachokipenda. Unapokuwa kwenye mahusiano kunakosekana uhuru wa kufanya vitu uvipendavyo hii ni kwa sababu unaweza ukawa unapenda kufanya jambo fulani ila kwa kuwa upo kwenye mahusiano ya kimapenzi huyo mpenzi wako akakuzuia kufanya jambo hilo kwa kuwa jambo hilo halimpendezi.



3. Unapikuwa single unakuwa hauna hisia mpelekesho, hisia mpelekesho ni zile hisia za kimapenzi ambazo zinakufanya ifikiri sana kuhusu mambo yanayohusu mapenzi, kwa mfano hivi hujawahi ona mtu anakurupuka usiku wa manane anampigia simu mpenziwe? bila shaka umewahi kuona, hii ni tabia inayokwenda sambamba na kitu kinachoitwa wivu. Hivyo unapokuwa single unakuwa hauna wivu kwa sababu unakuwa hauna mtu ambaye anakufanya uwe hivyo.

4. Unapokuwa single hakuna lawama zinazohusu mahusiano ambazo zitakuwa zinakuhusu wewe. Unapokuwa kwenye mahusiano yapo malalamiko mengi ambayo yatakuwa upande wako, vitu kama kwanini hupokei simu yangu na mambo mengine kama hayo yatakuwa mbali na wewe.

5. Utaishi maisha marefu yenye mjumuiko wa amani ya moyo pamoja usiokuwa na bugudha wala makwaluzano ya aina yeyote ile.

6. Kila siku Utalala usingizi mzuri.

7 Faida nyingine ya kuwa single utaongeza mwenyewe.
 
Back
Top Bottom