Faida na Hasara za Uwakala wa MaxMalipo na ButtonPay

Faida na Hasara za Uwakala wa MaxMalipo na ButtonPay

Sijatumia max malipo or hiyo nyingine kwangu natumia selcom mtaji ni laki 5
Faida yake unaipata papo kwa papo mfano..
Unapouza luku unapata faida ya asilimia 3 kila ufanyapo muamala so ukiuza umeme wa 10000 kwenye balance yako yani float itaongezeka kwa asilimia tatu yani mia 3 kwa hiyo ukiuza umeme wa 100000 unapata 3000 na inaenda hvyo...kwa commision luku ndio ina aslimia kubwa na huduma nyingine zina asilmia chache zaidi mfano vocha ni 1.5 dstv 1 na nyinginezo....uzuri wa hii uwe sehemu kwenye mzunguko wa hela ambapo una hakika itaisha haraka na pia ni kivutio kizuri kama una biashara nyingine unafanya eneo hilo yani ni kama vocha na soda....
Conclusion.
Kwangu biashara ya vocha inalipa kuliko hizi machine ingawa ni vizuri ukawa unavyo vyote sambamba....

Nawasilisha ....
Asante
 
Mimi nilifanya kwa kutumia mashine ya Selcom,kama alivyosema mdau hapo juu uitumie kama kivutio cha biashara nyingine na uwe sehem yenye mzunguko lasivyo faida yake utaona aibu hata kuiangalia,commission zao ni ndogo kiukweli,mi ilinishinda sahivi mashine ipo tu ndani.Hasara; Usipokuwa makini unaweza pata hasara sana tu,mfano ukikosea kuingiza namba ya simu wakati wa kurusha vocha ukamrushia mtu mwingine ndo imekula kwako.
Kweli mimi nawachaji 200 ya huduma ndo naona kafaida kidogo kwene luku otherwise ni kupoteza muda.zamani kweli ilikuwa na faida
 
Mkuu, ukishanunua hyo mashine huwa unaenda tena vodacom, hewatel, tigo, tanesco, dstv n.k ili kuuza bidhaa zao au hawa selcom wanakuunganisha 1 kwa 1?
Naomba kama wana chart yao ya commission. Je, malipo ya Serkali kama traffic notification yamekaaje?
 
Nasikia uko dsm unaweza kuunganishwa na huduma za selcom kupitia simu??
 
Back
Top Bottom