Lekanjobe Kubinika
JF-Expert Member
- Dec 6, 2006
- 3,020
- 577
Waganga wanavaa makoti marefu meupe, mashehe na wachungaji na mapadre wanavaa majoho meupe na marefu. Nini faida na hasara zake?
- Padri, shehe wanapohubiri wanahifadhiwa na mavazi yao wasiaibike pale mambo yanapobadilika wakihubiri, hasa mabinti wengine wanapokuwa hawataki kuvaa nguo za heshima kusitiri maungo yao, tena mabinti wenyewe wanapenda kukaa mbele wakipanua miguu yao wanaposikiliza mahubiri wakichezesha mapaja yao kama vile mtu apigavyo makofi. Sio madada wote waendao misikitini na mahekaluni wanaenda kuabudu Mungu, wapo wanaokwenda kutafuta dawa ya ashiki zao wawanase wawatazamao. Ndio maana inashauriwa usitafute mchumba siku ya Iddi na Chrismass - mabinti wote ni warembo na wanavutia sana. Angalia watu wanavyohangaika kutafuta vazi special la kuvaa kanisani na msikitini siku ya ibada, halafu wanayatoa mara baada ya kumaliza ibada.
- Madaktari wako serious kuwasaidia wagonjwa lakini kuna wadada wengine utadhani hawaumwi kwa namna wanavyojianika na kujipamba waendapo hospitali, waganga wanachanganywa akili kwa perfumes na vivazi vilivyovaliwa kwa namna ya kumwamsha aliyelala, tena wanajiachiaaaaa mbele ya daktari anapoanza kuchukuwa maelezo ya mgonjwa kwa kumsikiliza na kuangaliana macho. Mambo yakiharibika, makoti yanasaidia kuficha dhahama ya bwana mdogo anayehangaika kutaka kufungulia kamba na kuchomoka. Waulize waganga wa meno taabu waipatayo kutibu mabinti wanaoumwa meno lakini generally ni wazima. Mganga wa meno anaangalia uso zaidi na kama hakupata breakfast kwake kuna kuchanganyikiwa na sura hizo na sauti na macho ya mlegezo.
- Labda hizo ni baadhi ya faida, kusitiriwa na aibu pale jogoo anapotaka kuleta fujo wakati usiokuwa muafaka. Lakini hasara yake ni kwamba mavazi hayo huwafanya wavaaji hao kulemaa kwa maumivu ya kila mara lakini wasiweze kuonyesha hisia zao na hata kujifunza mbadala wa focussing on specific issues. Ndio maana daktari anaweza kukaa hata saa nzima anachukuwa history ya binti na kumrudiarudia kupima kifua na tumbo akidhaniwa anatafuta ugonjwa kumbe naye ndio anamaliza fadhaa zake.
- Kama ukumuona mwanamke kwa jicho la kumtamani utakuwa umezini, basi wachungaji, mashehe na madaktari wengi wameshanaswa na mitego kila mara, hawatubu kwa sababu wameyageuza mambo hayo kuwa ni matukio ya kawaida kazini. Ndio maana hadithi hazikomi kusikia daktari, shehe, padri amebaka mhudumiwa wake tena ofisini kwake.
- mavazi hayo yanawafanya madaktari, wachungaji na mashehe wapate taabu kuchagua wenza wao kwa sababu kama ni urembo wanakutana na urembo wa kila aina kila siku hata wadumazwe kujua ni yupi zaidi kati yao wote wanaowaona kila siku. Wengi wanakujapata wenza baadaye sana, au wanamaliza hasira zao za muda kwa ama manesi na wagonjwa (kwa Madaktari), wahudumu na waumini (kwa wachungaji na mashehe), masista na waumini (kwa mapadre).