FAHAMU: Ugonjwa wa mtu ni siri kati ya Mgonjwa husika na Daktari, hayo ndiyo maadili ya kitabibu dunia nzima

COARTEM

JF-Expert Member
Nov 26, 2013
3,598
3,644
Confidentiality: Daktari au mtumishi yoyote anayehusika kumtibu mgonjwa anatakiwa kutunza siri ya ugonjwa aliyonayo mgonjwa huyo. Daktari haruhusiwi kutoa taarifa za huyo mgonjwa bila idhini ya mgonjwa husika.

Lakini pia mgonjwa anaweza yeye mwenyewe kutoa taarifa ya nini anaumwa kwa mtu wake wa karibu akipenda au kwa watu wote bila kushurutishwa na kitu chochote.

Ni kosa la kimaadili kwa daktari au mtumishi wa Afya kutoa siri za wagonjwa.

Kwa faida zaidi someni : MEDICAL ETHICS / BIOETHICS

 
Ushachomoa betri hapo
Taarifa za mgonjwa zinaanzia pale anapokuja Hospitali na kusema naumwa mpaka kutambua anachoumwa.
( PATIENT INFORMATIONS ARE STRICTLY CONFIDENTIAL)
Akiamua yeye mgonjwa kujitangaza sheria inamruhusu
 
kwa hiyo unataka taarifa za wafanyakazi wote wa serikali na wabunge wote wanaoumwa uwe unapewa kwa kuwa wanalipwa kwa kodi za serikali?
Tena huko ukiumwa tu..siku unarudi kazini lazima uende na kile cheti cha ugonjwa...kuepeusha kutumia muda wa walipa kodi vibaya na pia kuongopa.Lipo wazi kabisa hilo...sasa sijaelewa kwanini huwa vyeti vinahitajika na akijua HR dunia umejua.
 
kwa hiyo unataka taarifa za wafanyakazi wote wa serikali na wabunge wote wanaoumwa uwe unapewa kwa kuwa wanalipwa kwa kodi za serikali?
Hata wale wabunge walionyimwa matibabu kutokana na kukosa saini ya Rais tulijulishwa.

Rais anapata 100% care ili aliongoze taifa. Ndiyo maana anasafiri first class ili awe na uwezo wa kuendelea na kazi huko afikapo.
 
Nilisikitika Magufuli yuko
kanisani, anamuanika mama mtawa aliyekatwa ziwa!
 
Mtazunguuka sana, ila mwisho wa siku mjinga atapatikana,kati ya nyie au wananchi!
Tunaendelea kuhesabu siku.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…