Fahamu SIFA za mwanamke wa kuoa

Fahamu SIFA za mwanamke wa kuoa

Tatizo mara nyingi hizi hoja hujengwa upande mmoja. Juzi juzi kulikuwa na sifa za mwanaume anayefaa kuwa mume. Kama hizo ndio sifa za mwanamke, je huyo mwanaume anayetaka sifa hizo, yeye binafsi awe na sifa zipi? Au iandikwe wanandoa watarajiwa wawe na sifa zipi? Kibaya zaidi hata hizo zilizotajwa kila mtu ana tafsiri yake. Mfano mdogo - mwanamke mvumilivu ni yupi? Anayevumilia shida na raha katika ndoa, anayevumilia kipodo, anayevumilia michepuko ya mumewe?

Mkuu Tunajua kwamba maisha siku zote hayatabiriki, yanaweza kutokea matatizo ya kiafya ama kifedha.Huu ndio wakati wa kuona uvumilivu wa mtu.Kama mwanamke anatarajia kwamba siku zote ni za raha tu na pindi matatizo yanapotokea anachukua uamuzi wa kumtoroka mwanume, huyo siyo mwanamke wa kuoa.
 
Hizo sifa hazina maana yeyote kama kwenye sita kwa sita ni ziro.
 
Mmmmm hizi labda zinatoka katika bibilia au ni mtazamo wako tuu katika uislamu sifa hizo zote hazimo mi sichagui sifa hizo nisije kuingia cha kike bureeeee
 
Mzeee umebugi sifa ulizosema za mwanamke kuolewa sizo kabisa hebu cheki hizi halafu nambie
1 awe mzuri kioo cha macho yako
Akiwa na sifa hio ya uzuri utatulia hutohangaika na wapita njia kwani na utaepuka zambi ya zina kwa 90%
2 awe na nasabu nzuri
Mwanamke akitokea katika familia nzuri ilio na malezi hakupi tabu kwani atajua wajibu na majukumu yake kukutunza na kukuthamini
3 awe na mali
Mwanamke akiwa na mali inasaidia sana kwani munapiga maendeleo fasta na atakua ni mtuzaji na mtumiaji mzuri wa kile mungu anachokujaalie hatokua na fujo katika matumizi
4 awe na dini
Mwanamke akiwa na dini atakulelea watoto wako katika misingi mizuri ya dini atakuhimiza ili mupatr ufaulme wa mbinguni pia yakikukuta majanga atakuvumilia kwani anajua ni maandiko ya mungu

Hebu niambie unazionaje hizi?

Sent from my HTC Desire S using JamiiForums mobile app
 
Mzeee umebugi sifa ulizosema za mwanamke kuolewa sizo kabisa hebu cheki hizi halafu nambie
1 awe mzuri kioo cha macho yako
Akiwa na sifa hio ya uzuri utatulia hutohangaika na wapita njia kwani na utaepuka zambi ya zina kwa 90%
2 awe na nasabu nzuri
Mwanamke akitokea katika familia nzuri ilio na malezi hakupi tabu kwani atajua wajibu na majukumu yake kukutunza na kukuthamini
3 awe na mali
Mwanamke akiwa na mali inasaidia sana kwani munapiga maendeleo fasta na atakua ni mtuzaji na mtumiaji mzuri wa kile mungu anachokujaalie hatokua na fujo katika matumizi
4 awe na dini
Mwanamke akiwa na dini atakulelea watoto wako katika misingi mizuri ya dini atakuhimiza ili mupatr ufaulme wa mbinguni pia yakikukuta majanga atakuvumilia kwani anajua ni maandiko ya mungu

Hebu niambie unazionaje hizi?

Sent from my HTC Desire S using JamiiForums mobile app

3 awe na mali

Mwanamke akiwa na mali inasaidia sana kwani munapiga maendeleo fasta na atakua ni mtuzaji na mtumiaji mzuri wa kile mungu anachokujaalie hatokua na fujo katika matumizi
3. MWENYE UCHU NA MAENDELEO
Hivi karibuni kumekuwepo na mabadiliko ya aina yake kwa wanaume, wengi sasa hivi hawapendi kabisa kuoa mwanamke ambaye hana kazi yaani 'golikipa'. Kama atakuwa hana kazi basi awe na uchu wa maendeleo kwa kujituma kufanya kazi mbalimbali za kimaendeleo kama vile kilimo kwa wale walio vijijini na biashara ndogondogo kwa wale ambao wako mijijini na hata vijijini.
Ile dhana ya kusema mwanamke ni mama wa nyumbani wa kukaa na kujipodoa akimsubiria mwnaume arudi amstarehesha, sasa hivi imepitwa na wakati. Wanaume wengi wanapenda wanawake ambao ni wahangaikaji, wenye ndoto za maendeleo katika maisha yao. Hata kama watakuwa si wafanyakazi lakini wawe wenye kutoa ushauri kwa waume zao juu ya jinsi gani wafanye ili wafanikiwe.
Mkuu wewe umekuja na tafsiri ya sifa ila mimi nimeweka sifa tazama tafsiri yangu na yako nipe tofauti
 
Tatizo mara nyingi hizi hoja hujengwa upande mmoja. Juzi juzi kulikuwa na sifa za mwanaume anayefaa kuwa mume. Kama hizo ndio sifa za mwanamke, je huyo mwanaume anayetaka sifa hizo, yeye binafsi awe na sifa zipi? Au iandikwe wanandoa watarajiwa wawe na sifa zipi? Kibaya zaidi hata hizo zilizotajwa kila mtu ana tafsiri yake. Mfano mdogo - mwanamke mvumilivu ni yupi? Anayevumilia shida na raha katika ndoa, anayevumilia kipodo, anayevumilia michepuko ya mumewe?

Umeongea vizuri sana ndugu....neno UVUMILIVU mimi huwa silielewi.....tena huwa sikurupuki kulijibu km nikiulizwa iwapo mimi ni mvumilivu
 
Umeongea vizuri sana ndugu....neno UVUMILIVU mimi huwa silielewi.....tena huwa sikurupuki kulijibu km nikiulizwa iwapo mimi ni mvumilivu
Mwanamke mweye mapenzi ya dhati ni lazima atakuwa mvumilivu na atakuwa tayari kuishi katika maisha ya aina yoyote, yawe ya raha ama ya shida.Hawa ndio wale ambao wanaume wengi wengependa kuwa nao maishani mwao.
Uvumilivu!
 
Hizo sifa utazijuaje? Navyojua mimi these days watu wanaangalia beauty kwa kugegeda, sura, miguu, umbo na rangi.

Wanaume wengi wanapofikia hatua ya kuoa si kwamba wanakurupuka tu na kuoa mwanamke yeyote mwenye sura nzuri, bali huchukua muda wao mwingi kuchunguza mambo mengi juu ya wake ambao wanadhani kwamba wanaweza kuwa pamoja kwa kipindi chote cha maisha.
Wanawake wengi wanajisahau na kudhani kwamba kitu kinachoweza kuwafanya wakapata wachumba ni uzuri hivyo kupoteza muda wao kujichubua na kujiremba ili wawavutie wanaume bila kujua kwamba kuolewa ni zaidi ya uzuri.
Hali sasa hivi imebadilika ni tofauti na kipindi cha nyuma ambapo ukiwa na sura nzuri na umbo la kuvutia basi una asilimia 100 za kuolewa.
Utafiti ambao nimeufanya unaonesha kwamba zaidi ya uzuri wa tabia na umbo, kuna kuna sifa nyingine za msingi ambazo mwanamke anatakiwa kuwa nazo ili aweze kuwa katika mazingira mazuri ya kupata mchumba wa kumuoa kiasi kwamba asipokuwa nazo ataishia kuchezewa tu lakini haitatokea mtu kumtamkia kwamba anataka kumuoa.
1. MWEYE MAPENZI YA KWELI
2. MWENYE TABIA NZURI
3. MWENYE UCHU NA MAENDELEO
4. ASIYEPENDA MAKUU
5. MVUMILIVU
Mwanamke ukiwa na sifa hizo tano hapo juu unauwakika wa 100% kuolewa.
Nawasilisha!
 
Umesahau sifa moja muhimu sana ya kutoa ushirikiano wa hali ya juu katika tendo la ndoa, siyo mpaka alazimishwe kunywa kilevi 🙂🙂🙂

[video]http://www.youtube.com/results?search_query=hideaway+ kiesza[/video]
 
Sifa za kuoa ua kuolewa ziko subjective sana....it will depend frm one person to another
Huwezi uka generalize ktk kitu kama hicho

Aisee mkuu sirmudy kuna tabia ambazo ni common kwa kila mwanaume muoaji na anapenda mwanamke wake awe nazo mfano Uvumilivu,Upendo,Uaminifu.kwangu mimi hizo naona ndizo nguzo kwny Ndoa plus za mtoa mada...
 
ANAEPENDA na KUITAFUTA PESA
hii ndo inabeba ZOTEEE HIZOOOO

penye pesa pana amani
 
Hizo sifa zote bila huyo mwanamke kuwa mcha Mungu ni kazi bure!! Mtatwanga pilipili mshahara Wake kukohoa!!!!
 
Back
Top Bottom