Fahamu dawa na mambo yatakayoweza kukupatia mwanamke umtakae..

Da'Vinci

JF-Expert Member
Dec 1, 2016
35,627
106,589
Salute
Psychological Manipulation, jinsi ya kumpata umpendae kwa kumteka kihisia na kiakili.

Kwanza kabisa ili uweze tengeneza computer inakubidi uelewe jinsi mifumo na vifaa vyote vilivyomo ndani ya Computer na jinsi vinavyofanya kazi..Chukulia mwili wa binaadamu ni Computer nzima, ubongo ni Processor,Monitor (kioo) ni Moyo. So inakua hivi unapomuona mtu unayempenda moyo hudunda haraka haraka mwili unajaa uoga pengine hua mtu anatoka hadi jasho usoni , hii inafanya watu wengi
tunaamini kua Upendo/Mapenzi yanatoka au yanakaa moyoni. Jibu ni NOOOO! Mapenzi hayakai moyoni wala hayatoki moyoni, moyo hauhusiani kabisa nawewe kumpenda mtu, moyo hua unafanya kazi ya kusukuma damu tu! Pia unatoa output ya Upendo.

Ubongo umegawanyika katika maeneo mbalimbali , ndani ya ubongo kuna sehemu inayoitwa
Paleomammalian Cortex (Limbic System) hii ndio sehemu ya ubongo inayohusika nma kupenda mtu, unapomuona mtu yoyote unayempenda hii sehemu ya ubongo inatoa chemicals mbazo zinapelekea moyo kwenda kasi, halafu unasikia moyo unampenda sana huyo mtu lakini ukweli huo upendo upo kwenye ubongo. Hizo hisia unazisikia kwenye moyo sababu kuna Nerve mbalimbali ndani ya moyo ambazo huhisi maumivu ua hali yoyote kutokana na jinsi ubongo ulivyoamua moyo uhisi…

Emotions zinakaa ndani ya Akili (Mind, kumbuka mind ipo ndani ya Ubongo) hivyo basi kupitia Limbic system Love
Emotions hutafsiriwa na kutolewa huko kwenye Moyo kama output Device.

NB
. Mambo haya nitakyoelezea hapa yanaweza kufanywa na mtu wa jinsia yoyote, ila nimeegemea kwa jinsi ya kumpata mwanamke kwakua mwanamke ndio tamaduni yake kiafrika kutafutwa na mwanaume.

Je nifanyeje ili kumpata nimpendae…?

Ili kumpata mtu unayempenda baada ya kujua kua hisia za mapenzi ya mtu zinakaa kwenye Mind inabidi
ucheze na Mind ya muhusika na ukiweza kufanya hivyo nakuhakikishia utampata yoyote umtakae.
Unachotakiwa kufanya ni kua mvumilivu maana mazuri hua yankuja polepole ukiwa umayatolea jasho.
Yafuatayo ni mambo makuu matatu ambayo ukiyafanya una uwezo wa kumpata hata Beyonce kama una
ukaribu nae..​
  • Kindness (Wema)​
Hapa tunaweza kusema kua ni mtu kua mwema na kufanya matendo ya wema na huruma, matendo hayo yanaweza kua Uaminifu,Loyality,Heshima,Kua Romantic nk. Kama unampenda mwanamke Fulani
tafuta kila njia uwe karibu nae, jua anavyopendelea na matatizo aliyonayo. Ukishamfahamu anza kumfanyia matendo ya wema kama Kumjulia hali, kusimama nae katika shida alizonazo, mtembelee, mtoe out, fanya kila kitu kuonyesha jinsi gani unavyomjali ,unamthamini, unamlinda,unamheshimu,nk.
mind ya kila binaadamu imewekea Wema, so Unapomfanyia mtu matendo ya wema unakua unaivuta
mind yake kujenga na attention kwenye mind yako.

Baada ya kua unamfanyia matendo ya wema mwanamke mind inaanza kutengeneza Emotions juu yako
kwakua unakua umekua umeigusa kwa kufanya vitu ambavyo Mind imeumbiwa kufanya na kufanyiwa.
Baadae zile emotions zitakua zinatolewa kutoka kwenye Mind na kupelekwa kwenye ile sehemu ya ubongo inayoitwa limbic system kisha moyo utakua unatoa outup sasa juu yako jinsi Mind inavyokufeel.

Ndio pale sasa ukimfanyia kitu Fulani anahuzunika pengine anaweza hata kulia kutokana na jinsi jinsi gani matendo yako yanvyogusa mind yake. Mwisho utakua ume win moyo wake kama tulivyozoea kusema lakini kiuhalisia ni Mind yake ndio unakua umeu-win. Utakua umejipatia mpenzi wa ndoto zako.

Hii njia inaweza kua ndefu, yenye vikwazo na yenye kukatisha tama, so itumie hii njia kwa Yule ambae
unayeona ndio wako wa maisha kama akikubalia ila kama unataka ku hit and run hii njia utaona ni
usumbufu na mzunguko mkubwa. Pia kuna vitu baadhi unaweza kuvitumia wakati unatekeleza hio njia,
vitakusaidia kuongeza point 3 muhimu katika kumteka moyo/akili mrembo huyo umtakae. Vitu hivyo ni..
  • Humbleness
Kua mtu usiye na makuu, hujikwezi,msikivu nk. Wanawake wanapenda watu ambao hawana makuu, sio
wabishi bishi kwa kila kitu, sio mr misifa. Humbleness ni bure kabisa waweza kuimudu bila kutumia
ghalama yoyote ile, Heshimu mwenzako hisia na mawazo yake. Akikuambia sitaki kutoka leo
usilazimishe, muda mwingine inabidi ujifanye mjinga ili uweze kutimiza malengo yako.​
  • Be smart
Kua smart kichwani sio kila muda wewe mdomo wako unafyatua maneno yasiyo na staha au ya kihuni..Play smart and wise. Unaweza kua smart kichwani ila huna hekima, ukiwa na smart kua wise
katika vitendo na maongezi yako. Trust me ladies wengi wanapenda mno Man ambaye yupo vizurii kichwani akichambua kitu anakichambua . Jitambue kama mwanaume smart ambae unaweza
kumwongoza mwanamke pamoja na watoto mtakaowapata kama ikitokea mmeingia ndani ya ndoa! Kua
smart kichwani utapendwa na kila mwanamke.

NB. Katika maansishi yangu nimetaja Mwanaume sio Boy na mwanamke sio girl nikimaanisha kua njia hi itumiwe na watu wenye commitment na ndoa sio wanaotaka kufanya ngono na kuondoka. Kama utakua
unamuhitaji mtu kwa ajili ya ndoa hii njia itakua rahisi na utaweza kuvumilia usumbufu utakai upata si
unajua mambo mazuri huchelewa ili kukupima uwezo wako wa kuvumilia.
All the best MEN.

The End…
~Da’Vinci.
El maestro.
 
Victims wakubwa wa hii njia ni Wanawake wanaolea watoto wao peke yao (Singo mazas) Samahani sana waliopo kwenye kuni hili kama nitawakwaza, tatizo sio langu bali ni jamii ilivyoamua kuwachukulia katika
mlengo hasi kama watu Fulani ambao hawafai au watu Fulani ambao hawastahili kua kwenye jamii.

Lakini wanasahua kua ili singo mama atokee basi nyuma yake kunakua na baba aliyeshindwa kusimamia majukumu yake ipasavyo kama mwanaume. So jamii inamchukulia singo maza kama something to get rid of..But kunakua na sababu nyingi sana hadi kuona mwanamke anabaki mwenyewe. Anyway Dunia haina huruma kwa nyonge.

Mara nyingi mwanamke anapotengana na Mzazi mwenzake hua Desperate, kutokana na shida mbalimbali zinazomsumbua, mbaya zaidi mental Health yake inakua Disturbed so akitokea mtu akaonyesha mambo hayo juu hapo wanakua wepesi mno kumpokea.

Bahati mbaya wengi anaowafuata wanakua wameenda kwa ajili ya ku Hit tu, otherwise itokee kweli mwanaume awe amekupenda kweli. Dada zangu mliozalia home au mmetengana na wazazi wenzenu kuweni makini nawatu hawa, wengi wanatumia udhaifu wa shida mnazokua nazo kiakili na kiuchumi ili kukupata. Fanya Enhanced Evaluation kabla ya mtu kumkabidhi moyo wako baada ya kuona anakujali sana.

Sorry kama nimekwaza mtu
 
Back
Top Bottom