Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 14,939
- 20,399
Mtandao wa jamii maarufu duniani kwa jina la FACEBOOK wameanza mchakato wa kufuta kaunti zote ambazo uhalisia wake haujulikani yaani ni za bandia.
Baada ya uchunguzi wa muda kufanyika kwenye mtandao huo na hasa baada ya kujiorodhesha kwenye soko la mitaji la NewYork, imegundulika kuwepo kwa akaunti za uongo za watu zipatazo milioni 83.
Baadhi ya watumiaji maarufu wa mtandao huo kama Justin Timberlake, Rihanna na Lady Gaga na wengine wamejikuta wakiwa na upungufu wa wafuasi wao kwenye mtandao huo.
Lady Gaga ana wafuasi wapatao milioni 53,238,735
Hatua hiyo ya FACEBOOK imekuja katika wakati ambao mtandao huo unatafuta pesa zaidi kupitia matangazo ambapo ni wale watumiaji halisi ndio wataweza kulengwa na makampuni ambayo yanatangaza kwenye mtandao huo. Pia imeaminika kuwa asilimia 8.7 ya watumiaji wake wapatao 845 hawatumii majina ya kweli, hivyo kufanya nasafi yake kwenye soko la mitaji kuwa ndogo.
Rihanna nae anavutia wafuasi wanaofikia milioni 60,370,797 sasa.
Moja ya tatizo kubwa la watumiaji wa majina ya uongo ni kuweza kutengeneza pongezi au "likes" kwa kutumia software maalum za Malware ambazo huingilia kazi za computer husika na kuharibu utendaji wa program zake, kwa kufanya hivyo jina la FACEBOOK linakuwa linakuuzwa lakini katika hali isiyo rasmi.
Pia kwa mtindo huo wale watumiaji maarufu wanakuwa hawajui uhalisi wa wafuasi wao. FACEBOOK siku ya Alhamisi walitoa taarifa kwenye blog yao wakieleza hatua hiyo wanayochukua na kwamba wanaamini itasaidia kupunguza hizo "likes" kwa asilimia 1.
Utumiaji wa majina yasiyo rasmi umeleta matatizo kwa mitandao mingi ya kijamii na umekuwa shughuli nyingi za kihalifu pia zimekuwa zikifanika kwa kutumuia majina bandia kwenye mitandao hiyo.
Nembo ya mtandao wa FACEBOOK nje ya jengo la makao yake makuu mjini California kwenye kitongoji cha Palo Alto.
Mtandao wa JamiiForums tayari ulikwishajiandaa na yote haya na ndio maana tumefika hapa tulipo.
Idumu JF.
Baada ya uchunguzi wa muda kufanyika kwenye mtandao huo na hasa baada ya kujiorodhesha kwenye soko la mitaji la NewYork, imegundulika kuwepo kwa akaunti za uongo za watu zipatazo milioni 83.
Baadhi ya watumiaji maarufu wa mtandao huo kama Justin Timberlake, Rihanna na Lady Gaga na wengine wamejikuta wakiwa na upungufu wa wafuasi wao kwenye mtandao huo.
Lady Gaga ana wafuasi wapatao milioni 53,238,735
Hatua hiyo ya FACEBOOK imekuja katika wakati ambao mtandao huo unatafuta pesa zaidi kupitia matangazo ambapo ni wale watumiaji halisi ndio wataweza kulengwa na makampuni ambayo yanatangaza kwenye mtandao huo. Pia imeaminika kuwa asilimia 8.7 ya watumiaji wake wapatao 845 hawatumii majina ya kweli, hivyo kufanya nasafi yake kwenye soko la mitaji kuwa ndogo.
Rihanna nae anavutia wafuasi wanaofikia milioni 60,370,797 sasa.
Moja ya tatizo kubwa la watumiaji wa majina ya uongo ni kuweza kutengeneza pongezi au "likes" kwa kutumia software maalum za Malware ambazo huingilia kazi za computer husika na kuharibu utendaji wa program zake, kwa kufanya hivyo jina la FACEBOOK linakuwa linakuuzwa lakini katika hali isiyo rasmi.
Pia kwa mtindo huo wale watumiaji maarufu wanakuwa hawajui uhalisi wa wafuasi wao. FACEBOOK siku ya Alhamisi walitoa taarifa kwenye blog yao wakieleza hatua hiyo wanayochukua na kwamba wanaamini itasaidia kupunguza hizo "likes" kwa asilimia 1.
Utumiaji wa majina yasiyo rasmi umeleta matatizo kwa mitandao mingi ya kijamii na umekuwa shughuli nyingi za kihalifu pia zimekuwa zikifanika kwa kutumuia majina bandia kwenye mitandao hiyo.
Nembo ya mtandao wa FACEBOOK nje ya jengo la makao yake makuu mjini California kwenye kitongoji cha Palo Alto.
Mtandao wa JamiiForums tayari ulikwishajiandaa na yote haya na ndio maana tumefika hapa tulipo.
Idumu JF.