GE2025 Ezekiel Wenje: Kupiga Kura siyo suala la Vyama vya Siasa ila ni la Kikatiba

GE2025 Ezekiel Wenje: Kupiga Kura siyo suala la Vyama vya Siasa ila ni la Kikatiba

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

PAYE

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2025
Posts
354
Reaction score
395
Aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Victoria, Ezekiel Wenje, amesema suala la kwenda kupiga kura si la vyama vya siasa, bali ni la Mtanzania mmoja mmoja kama ilivyoainishwa kwenye Katiba ya Nchi.

Wenje ameyasema hayo leo, Oktoba 28, 2025, katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, wakati wa hitimisho la mikutano ya kampeni za Uchaguzi Mkuu wa 2025 ya mgombea wa urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu Hassan.

"Huu uchaguzi ni uchaguzi halali wa kikatiba, umefuata sheria na kuna waangalizi wa kimataifa na ndiyo maana mpaka kesho tutakapoenda kupiga kura hakuna chama chochote cha kisiasa ama mtu yoyote ambaye ameenda mahakamani kupinga kwamba huu uchaguzi ni batili. Tunaenda kwenye uchaguzi halali, wa kisheria na unaosimamiwa kikatiba, twendeni tukapige kura."
 
Huyu jamaa kama anafikiri watu wanaomuonea kwa kumuona kama mtu asiye na akili baada ya kurudi kwenye chama chake cha zamani, ccm! Basi atakuwa amekosea sana. Hata hawamuonei! Wako sahihi kabisa.

Hakuna mtu anayepinga kama huo mchakato siyo wa kikatiba! Watu wanapinga namna ya huo mchakato unavyo endeshwa kwa maslahi ya kikundi cha watu wachache ndani ya ccm, badala ya nchi na wananchi wake!

Na ndiyo maana tunataka mabadiliko ya kweli ndani ya tume ya uchaguzi, lakini tunataka kuwepo na katiba ya wananchi ili tuondokane na hii katiba mbovu ya sasa, iliyoundwa kwa ajili ya kuhakikisha ccm inatutawala milele. Tumechoka kutawaliwa kinguvu, na kinyume na matakwa yetu.
 
Huyu ni kiazi kweli anaongea upupu mtupu sasa unapigaje kura wakati tume ni ya magumashi??

Useless and hopeless idiot!
 
Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ezekiah Wenje amesema haki ya kupiga kura kwa wananchi wa Tanzania haitolewi ama kusimamiwa na vyama vya siasa, bali ni suala la msingi lililoko kwenye Katiba ya Tanzania na ni haki ya mtu mmoja mmoja, akiwataka wananchi kutokubali kupangiwa ikiwa wakapige kura hapo kesho ama laa.

Wenje amebainisha hayo leo Oktoba 28, 2025 Jijini Mwanza kwenye Viwanja vya CCM Kirumba, wakati wa ufungaji wa kampeni za mgombea Urais wa Chama Cha Mapinduzi Dkt. Samia Suluhu Hassan akisema uchaguzi huu pia ni halali, wenye kufuata sheria ikiwa ni pamoja na kualika waangalizi wa kimataifa, hivyo Watanzania wasihadaike kuwa uchaguzi huu haupo kisheria.

Soma pi: Wenje: Chama kinachosusia uchaguzi ni cha fujo, nimepata wokovu CCM



"Huu uchaguzi ni uchaguzi halali wa kikatiba, umefuata sheria na kuna waangalizi wa kimataifa na ndiyo maana mpaka kesho tutakapoenda kupiga kura hakuna chama chochote cha kisiasa ama mtu yoyote ambaye ameenda mahakamani kupinga kwamba huu uchaguzi ni batili. Tunaenda kwenye uchaguzi halali, wa kisheria na unaosimamiwa kikatiba, twendeni tukapige kura." Amesema Wenje.

Katika hatua nyingine Wenje ameeleza kuwa sheria zote zilizopo nchini zinatungwa bungeni, akisisitiza kuwa namna pekee ya kurekebisha na kutunga sheria mpya ni katika chombo hicho cha bunge na sio barabarani ama mtaani kama ambavyo baadhi ya watu wamekuwa wakishinikiza kutaka mabadiliko ya kisheria kupitia njia mbalimbali Mitaani ikiwemo maandamano na mengineyo.

Wenje amesisitiza umuhimu wa kuheshimu vyombo vya usimamizi wa sheria vilivyoweka kisheria, akikilaumu chama chake cha zamani CHADEMA kwa kushindwa kushiriki katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu ili kuwa na wawakilishi wa kwenda kusimama bungeni na kushiriki katika utungaji wa sheria.

Amekemea pia taasisi za kimataifa zinazodai kuwa hakuna demokrasia nchini na CHADEMA imezuiwa kushiriki uchaguzi mkuu wa hapo kesho, akibainisha kuwa chama chake cha zamani ndicho pekee kwa maamuzi yake binafsi kiliamua kususia uchaguzi huo wa kesho Jumatano Oktoba 29, 2025.
 
Back
Top Bottom