Exclusive: Kikwete kuongoza G5!?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Rais Jakaya Mrisho Kikwete anatarajiwa kuongoza mkutano wa nchi tano za Afrika ya Mashariki katika kile ambacho kinaaminiwa juhudi ya nchi hizo kukabiliana na mmonyoko wa kiuchumi duniani. Mkutano huo utakaozihusisha nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi unatarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi huu au mapema mwezi wa tano.

Kwa mujibu wa habari za ndani toka Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje, Mkutano huu unatarajiwa kuwa ni wa kupanga mikakati na hatua za kukabiliana na matatizo yakiuchumi ambayo tayari yameanza kuonekana katika nchi hizo kufuatia kuporomoka kwa uchumi katika nchi wafadhili za Kimagharibi zikiongozwa na Marekani.

"Viongozi wametambua kuwa hawawezi kusubiri nchi wafadhili kuja na mipango ya kuokoa nchi za Kiafrika kiuchumi wakati wao viongozi wa Taifa wana uwezo wa kufanya mambo kadha wa kadha kwa juhudi zao wenyewe" amesema mdokezaji wetu kwa masharti ya kutotajwa jina kwani habari hizo hazijatangazwa rasmi.

Kwa mujibu wa msemaji huyo, wazo la kuzikutanisha nchi hizi ni la Rais Kikwete ambaye kutokana na mkutano wa IMF/WB uliofanyika nchini, mkutano wake na Waziri Mkuu wa Uingereza Bw. Gordon Brown na matokeo ya mkutano wa nchi 20 tajiri zaidi duniani ameona kuwa nchi za Afrika ya Mashariki zinaweza kabisa kupanga na kufadhili programu kubwa za maendeleo ambazo zitasisimua uchumi wa nchi hizo na kuongeza ulaji wa ndani, na uzalishaji wa bidhaa kwa soko la nje.

Naye afisa wa Mambo ya Nchi za Nje Charles Kimau toka Kenya amesema kuwa wazo hilo la mkutano huo tayari limefikishwa kwa Rais Kibaki na limepokewa na wao Kenya wako tayari kushiriki katika mkutano huo. Bw. Kimau alisema kuwa mkutano huo kwa kweli umechelewa na nchi yake iko tayari itashiriki ipasavyo katika kukamilisha.

Kutoka Uganda afisa mmoja toka Ikulu ya Nakasero Uganda aliyejitambulisha kwa jina moja tu la Ssemogerere amesema kuwa Uganda tayari wamepokea mwaliko na majibu yao ya awali ni kuwa wako tayari kushiriki katika mkutano huo. Toka Rwanda na Burundi majibu ni hayo hayo kwamba nchi hizo ziko tayari kufuata uongozi wa Rais Kikwete katika suala hili na watatoa ushirikiano wote.

Pamoja na kuwa mkutano huu unazihusu nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki nchi nyingine pia zimeonesha nia ya kutaka kuwa washiriki au waalikwa. Baadhi ya nchi hizo ni pamoja na Msumbiji, DRC, Visiwa vya Comoro na Ethiopia.

Kwa mujibu wa afia aliyetudokeza mkutano huo una lengo la kupanga mkakati wa kuinua uchumi wa nchi hizi hasa katika kipindi hiki ambacho kiukweli ni kipindi muafaka kwa kuanzisha miradi mikubwa ya kiuchumi ambayo itachochea ajira, kuboresha huduma mbalimbali, na kujenga nchi hizo kuelekea mataifa ya kisasa.

"Huu ni wakati wetu" alisema ofisa huyo kwa kujiamini. "Nchi za Kiafrika ni kweli hazijachangia sana katika mmomonyoko wa uchumi wa dunia lakini ukweli ni kuwa ni kwa sababu hazichangii sana katika uchumi wa dunia!" Kutokana na mchango huu kidogo wa Afrika ni wazi kuwa sauti ya bara hili haisikiki sana. "Fikiria kuwa GDP ya Bara zima la Afrika haifikii GDP ya jimbo la California huko kwenu Marekani" alisema afisa huyo. "Sasa kwanini watusikilize" alihoji kiudadisi.

Ni kutokana na ukweli huo, kwa upande wa Afrika nchi hizi ambazo zinaelekea kuwa shirikisho zinataka kuunganisha nguvu zake katika shughuli za uzalishaji mali, kuinua soko la ndani na kupanua bidhaa zao kwa soko la nje. Kwa mujibu wa mmoja wa waandaji wa mkutano huo, utakapofikia mwisho viongozi hao wanatarajia kutia sahihi makubaliano ambayo yanatazamiwa kuhusisha mambo makubwa yafuatayo:

a. Kuanzisha programu kubwa ya ujenzi wa miundombinu ya kisasa kwa kukusanya nguvu za mataifa hayo. Katika hili nchi hizi zinatarajiwa kuanzisha ujenzi wa barabara kubwa za kisasa za kuunganisha kila mkoa na mkoa katika nchi hizo katika mfano wa "Interstate Highways Project" wa Marekani chini ya Rais D. Eisenhower. "Tukiweza kuunganisha nchi zetu kwa mtandao wa barabara kubwa tutakuwa tumepiga hatua moja muhimu.

b. Kuanzisha mfuko maalum wa kuchochea uchumi ambapo fedha za ndani tu zitatumika. Mfuko huo unatarajiwa kukusanya dola bilioni moja. Tanzania imesema iko tayari kutoa dola milioni 400 kuanzisha mfuko huo ambao matumizi yake yataelekezwa katika kuinua na kuboresha kilimo cha umwagiliaji, kuchochea utafiti na ubunifu katika Sayansi na Teknolojia kupitia taasisi mbalimbali za kisomi, kuweka mitandao ya Internet bila nyaya kwenye miji mikubwa yote ya nchi hizo n.k.

c. Kuanzisha mabadiliko ya kisheria na uboreshaji wa taasisi za kiusalama ili kukabiliana na uhalifu wa fedha. Mojawapo ya mradi ambao unapendekezwa ni kujengwa kwa gereza jipya lenye kazi ngumu na usalama wa juu (maximum security) litakalochukua wahalifu wa kiuchumi katika maeneo ya Afrika ya Mashariki. Pia uboreshaji wa taasisi za usalama wa Taifa kwa kuanzisha mtandao wa kikompyut utakaounganisha taasisi za Kipolisi kuziwezesha kuwa na mawasiliano ya moja kwa moja ndani ya nchi za jumuiya hiyo.

d. Kutengeneza sera ya pamoja ya misaada ya kigeni ili hatimaye nchi hizo ziondokokane na utegemezi wa misaada ya kigeni katika bajeti zao. "lengo ni kuhakikisha kuwa nchi hizi zinaweza kufadhili bajeti zao wenyewe kwa asilimia mia moja, huku misaada yote ya kigeni ikienda na kuendeshwa na sekta binafsi bila kuingiliwa au kuingizwa serikalini" alisema ofisa huyo. "Katika kufikia lengo hilo, utaratibu mpya wa ukusanyaji, na udhibiti wa kodi unatarajiwa kubuniwa hasa kwa kuzingatia makubaliano ya kodi ya Afrika ya Mashariki ambazo kodi nyingi zitakuwa karibu zinalingana na hivyo kuwa na mchakato bora na wa kisasa wa ukusanyaji kodi.

e. Kufanya tathmini ya maliasili na utajiri wa asili wa nchi hizi ili hatimaye kuweza kuona ni mikataba gani ya uwezekaji haina manufaa na ifutwe ili hatimaye nchi hizi ziwe na msimamo na mwelekeo wa pamoja katika suala zima uwekezaji wa moja kwa moja wa fedha za kigeni (FDI). "Tuna utajiri mwinginei na hazina nyingi lakini mashirika makubwa ya kimataifa yanatumia ukimya wetu kutunyonya na kwa kweli kama kutunyonya wametunyonya; tunataka kurudi kwenye kukata mirija hii ya kiunyonyaji" alisema ofisa huyo.

Hata hivyo licha ya taarifa hizo baadhi ya watu kutoka Ikulu ya Dar-es-Salaam ambao wameulizwa juu ya mkutano huo wamekanusha kuwepo kwa mpango huo wakisema kuwa "tayari tumeshakutana na IMF/WB, tumekutana na Brown na mapendekezo yaliyotolewa na Rais kwa G20 yamepokelewa na kama unavyoona G20 wameahidi zaidi ya kile tulichowaomba, sasa mkutano wa sisi wa nini".

Afisa huyo alihoji ulazima wa mpango huo kama ulivyodokezwa akionesha kukerwa kuwa habari kama hizo zinavuja mapema na kusikitika kuwa kwa mtindo huo "mnafanya kazi ya watendaji serikalini kuwa ngumu sana, kwani hakuna siri yoyote". "Kama mpango wa mkutano huo kuwepo au kutokuwepo, hayo ni maswala ambayo yana wakati wake, sijui kwanini mnapenda kutafuta udaku wa kisiasa namna hii" alisema na kukata simu.

Naye afisa mmoja mwingine mwandamizi toka wizara ya mambo ya nchi za Nje alisema kuwa hana taarifa ya mkutano huo kwani ndiyo kwanza wamemaliza mikutano mingine na kuwa hakuna sababu ya kuwa na mkutano wa aina hiyo. "Tayari nchi wafadhili wamekubali kutusaidia na watatusaidia sana sasa sisi tuje na mipango hiyo mikubwa yote ya nini?" Alihoji katika hali ya kushangazwa agenda ambayo tuliidokeza kuwa tumeipata. "Hiyo mipango ni mikubwa sana kwa nchi zetu changa na maskini, labda mnaota ndoto" alisema kwa sauti ya kejeli.

Wakati huo huo, taarifa kutoka Jijini Dar zinadokeza kuwa mchakato wa kuendelea kuwafikisha watuhumiwa mbaliimbali wa ufisadi unatarajiwa kuendelea muda si mrefu hasa baada ya siku za hivi karibuni kuonekana kuna ukimya wa aina fulani huku baadhi ya watu wakidai kuwa "mafisadi wote wameshafikishwa mahakamani".

Kwa mujibu wa chanzo chetu, ruhusa iliyokuwa inasubiriwa imeshatolewa ya kuendelea na kusanya kusanya ya mafisadi na raundi inayokuja inatarajiwa kushtua taifa kwa wale watakaofikishwa kizimbani. "Hata hivyo, bado la kuangalia ni mashtaka gani yataletwa, kwani hii pia inaweza kuwa mbinu ya kuwasafisha baadhi ya watu kwa kuwaleta kwa mashtaka mepesi alimradi tu wamefikishwa mahakamani kwa mbwembwe zote" amesema mdokezaji wetu toka ofisi ya Mwanasheria Mkuu mwenye kujua mpango ulioko mbeleni.
 
G5 countries, the Group of Five, consists of five of the world's leading economies. The G5 members are: France, Germany, Japan, the United Kingdom, and the United States.

Kauli-mtu!
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete anatarajiwa kuongoza mkutano wa nchi tano za Afrika ya Mashariki katika kile ambacho kinaaminiwa juhudi ya nchi hizo kukabiliana na mmonyoko wa kiuchumi duniani. Mkutano huo utakaozihusisha nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi unatarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi huu au mapema mwezi wa tano.

Kwa mujibu wa habari za ndani toka Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje, Mkutano huu unatarajiwa kuwa ni wa kupanga mikakati na hatua za kukabiliana na matatizo yakiuchumi ambayo tayari yameanza kuonekana katika nchi hizo kufuatia kuporomoka kwa uchumi katika nchi wafadhili za Kimagharibi zikiongozwa na Marekani.

"Viongozi wametambua kuwa hawawezi kusubiri nchi wafadhili kuja na mipango ya kuokoa nchi za Kiafrika kiuchumi wakati wao viongozi wa Taifa wana uwezo wa kufanya mambo kadha wa kadha kwa juhudi zao wenyewe" amesema mdokezaji wetu kwa masharti ya kutotajwa jina kwani habari hizo hazijatangazwa rasmi.

Kwa mujibu wa msemaji huyo, wazo la kuzikutanisha nchi hizi ni la Rais Kikwete ambaye kutokana na mkutano wa IMF/WB uliofanyika nchini, mkutano wake na Waziri Mkuu wa Uingereza Bw. Gordon Brown na matokeo ya mkutano wa nchi 20 tajiri zaidi duniani ameona kuwa nchi za Afrika ya Mashariki zinaweza kabisa kupanga na kufadhili programu kubwa za maendeleo ambazo zitasisimua uchumi wa nchi hizo na kuongeza ulaji wa ndani, na uzalishaji wa bidhaa kwa soko la nje.

Naye afisa wa Mambo ya Nchi za Nje Charles Kimau toka Kenya amesema kuwa wazo hilo la mkutano huo tayari limefikishwa kwa Rais Kibaki na limepokewa na wao Kenya wako tayari kushiriki katika mkutano huo. Bw. Kimau alisema kuwa mkutano huo kwa kweli umechelewa na nchi yake iko tayari itashiriki ipasavyo katika kukamilisha.

Kutoka Uganda afisa mmoja toka Ikulu ya Nakasero Uganda aliyejitambulisha kwa jina moja tu la Ssemogerere amesema kuwa Uganda tayari wamepokea mwaliko na majibu yao ya awali ni kuwa wako tayari kushiriki katika mkutano huo. Toka Rwanda na Burundi majibu ni hayo hayo kwamba nchi hizo ziko tayari kufuata uongozi wa Rais Kikwete katika suala hili na watatoa ushirikiano wote.

Pamoja na kuwa mkutano huu unazihusu nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki nchi nyingine pia zimeonesha nia ya kutaka kuwa washiriki au waalikwa. Baadhi ya nchi hizo ni pamoja na Msumbiji, DRC, Visiwa vya Comoro na Ethiopia.

Kwa mujibu wa afia aliyetudokeza mkutano huo una lengo la kupanga mkakati wa kuinua uchumi wa nchi hizi hasa katika kipindi hiki ambacho kiukweli ni kipindi muafaka kwa kuanzisha miradi mikubwa ya kiuchumi ambayo itachochea ajira, kuboresha huduma mbalimbali, na kujenga nchi hizo kuelekea mataifa ya kisasa.

"Huu ni wakati wetu" alisema ofisa huyo kwa kujiamini. "Nchi za Kiafrika ni kweli hazijachangia sana katika mmomonyoko wa uchumi wa dunia lakini ukweli ni kuwa ni kwa sababu hazichangii sana katika uchumi wa dunia!" Kutokana na mchango huu kidogo wa Afrika ni wazi kuwa sauti ya bara hili haisikiki sana. "Fikiria kuwa GDP ya Bara zima la Afrika haifikii GDP ya jimbo la California huko kwenu Marekani" alisema afisa huyo. "Sasa kwanini watusikilize" alihoji kiudadisi.

Ni kutokana na ukweli huo, kwa upande wa Afrika nchi hizi ambazo zinaelekea kuwa shirikisho zinataka kuunganisha nguvu zake katika shughuli za uzalishaji mali, kuinua soko la ndani na kupanua bidhaa zao kwa soko la nje. Kwa mujibu wa mmoja wa waandaji wa mkutano huo, utakapofikia mwisho viongozi hao wanatarajia kutia sahihi makubaliano ambayo yanatazamiwa kuhusisha mambo makubwa yafuatayo:

a. Kuanzisha programu kubwa ya ujenzi wa miundombinu ya kisasa kwa kukusanya nguvu za mataifa hayo. Katika hili nchi hizi zinatarajiwa kuanzisha ujenzi wa barabara kubwa za kisasa za kuunganisha kila mkoa na mkoa katika nchi hizo katika mfano wa "Interstate Highways Project" wa Marekani chini ya Rais D. Eisenhower. "Tukiweza kuunganisha nchi zetu kwa mtandao wa barabara kubwa tutakuwa tumepiga hatua moja muhimu.

b. Kuanzisha mfuko maalum wa kuchochea uchumi ambapo fedha za ndani tu zitatumika. Mfuko huo unatarajiwa kukusanya dola bilioni moja. Tanzania imesema iko tayari kutoa dola milioni 400 kuanzisha mfuko huo ambao matumizi yake yataelekezwa katika kuinua na kuboresha kilimo cha umwagiliaji, kuchochea utafiti na ubunifu katika Sayansi na Teknolojia kupitia taasisi mbalimbali za kisomi, kuweka mitandao ya Internet bila nyaya kwenye miji mikubwa yote ya nchi hizo n.k.

c. Kuanzisha mabadiliko ya kisheria na uboreshaji wa taasisi za kiusalama ili kukabiliana na uhalifu wa fedha. Mojawapo ya mradi ambao unapendekezwa ni kujengwa kwa gereza jipya lenye kazi ngumu na usalama wa juu (maximum security) litakalochukua wahalifu wa kiuchumi katika maeneo ya Afrika ya Mashariki. Pia uboreshaji wa taasisi za usalama wa Taifa kwa kuanzisha mtandao wa kikompyut utakaounganisha taasisi za Kipolisi kuziwezesha kuwa na mawasiliano ya moja kwa moja ndani ya nchi za jumuiya hiyo.

d. Kutengeneza sera ya pamoja ya misaada ya kigeni ili hatimaye nchi hizo ziondokokane na utegemezi wa misaada ya kigeni katika bajeti zao. "lengo ni kuhakikisha kuwa nchi hizi zinaweza kufadhili bajeti zao wenyewe kwa asilimia mia moja, huku misaada yote ya kigeni ikienda na kuendeshwa na sekta binafsi bila kuingiliwa au kuingizwa serikalini" alisema ofisa huyo. "Katika kufikia lengo hilo, utaratibu mpya wa ukusanyaji, na udhibiti wa kodi unatarajiwa kubuniwa hasa kwa kuzingatia makubaliano ya kodi ya Afrika ya Mashariki ambazo kodi nyingi zitakuwa karibu zinalingana na hivyo kuwa na mchakato bora na wa kisasa wa ukusanyaji kodi.

e. Kufanya tathmini ya maliasili na utajiri wa asili wa nchi hizi ili hatimaye kuweza kuona ni mikataba gani ya uwezekaji haina manufaa na ifutwe ili hatimaye nchi hizi ziwe na msimamo na mwelekeo wa pamoja katika suala zima uwekezaji wa moja kwa moja wa fedha za kigeni (FDI). "Tuna utajiri mwinginei na hazina nyingi lakini mashirika makubwa ya kimataifa yanatumia ukimya wetu kutunyonya na kwa kweli kama kutunyonya wametunyonya; tunataka kurudi kwenye kukata mirija hii ya kiunyonyaji" alisema ofisa huyo.

Hata hivyo licha ya taarifa hizo baadhi ya watu kutoka Ikulu ya Dar-es-Salaam ambao wameulizwa juu ya mkutano huo wamekanusha kuwepo kwa mpango huo wakisema kuwa "tayari tumeshakutana na IMF/WB, tumekutana na Brown na mapendekezo yaliyotolewa na Rais kwa G20 yamepokelewa na kama unavyoona G20 wameahidi zaidi ya kile tulichowaomba, sasa mkutano wa sisi wa nini".

Afisa huyo alihoji ulazima wa mpango huo kama ulivyodokezwa akionesha kukerwa kuwa habari kama hizo zinavuja mapema na kusikitika kuwa kwa mtindo huo "mnafanya kazi ya watendaji serikalini kuwa ngumu sana, kwani hakuna siri yoyote". "Kama mpango wa mkutano huo kuwepo au kutokuwepo, hayo ni maswala ambayo yana wakati wake, sijui kwanini mnapenda kutafuta udaku wa kisiasa namna hii" alisema na kukata simu.

Naye afisa mmoja mwingine mwandamizi toka wizara ya mambo ya nchi za Nje alisema kuwa hana taarifa ya mkutano huo kwani ndiyo kwanza wamemaliza mikutano mingine na kuwa hakuna sababu ya kuwa na mkutano wa aina hiyo. "Tayari nchi wafadhili wamekubali kutusaidia na watatusaidia sana sasa sisi tuje na mipango hiyo mikubwa yote ya nini?" Alihoji katika hali ya kushangazwa agenda ambayo tuliidokeza kuwa tumeipata. "Hiyo mipango ni mikubwa sana kwa nchi zetu changa na maskini, labda mnaota ndoto" alisema kwa sauti ya kejeli.

Wakati huo huo, taarifa kutoka Jijini Dar zinadokeza kuwa mchakato wa kuendelea kuwafikisha watuhumiwa mbaliimbali wa ufisadi unatarajiwa kuendelea muda si mrefu hasa baada ya siku za hivi karibuni kuonekana kuna ukimya wa aina fulani huku baadhi ya watu wakidai kuwa "mafisadi wote wameshafikishwa mahakamani".

Kwa mujibu wa chanzo chetu, ruhusa iliyokuwa inasubiriwa imeshatolewa ya kuendelea na kusanya kusanya ya mafisadi na raundi inayokuja inatarajiwa kushtua taifa kwa wale watakaofikishwa kizimbani. "Hata hivyo, bado la kuangalia ni mashtaka gani yataletwa, kwani hii pia inaweza kuwa mbinu ya kuwasafisha baadhi ya watu kwa kuwaleta kwa mashtaka mepesi alimradi tu wamefikishwa mahakamani kwa mbwembwe zote" amesema mdokezaji wetu toka ofisi ya Mwanasheria Mkuu mwenye kujua mpango ulioko mbeleni.

I do not get it! If Tanzania can get Dollars 400million to contribute to the group, why don't it go alone and work out projects which are pending in Tanzania? These countries are among the poorest and have the same level of development, what value will they add to each other; why an individual country not take issues alone? Why all this bureaucracy?
 
Hata mimi hiyo dola millioni 400 imenishtua kidogo. Kama tuna hela kiasi hiko, kwanini tusianze na mikakati ya ndani ya kujenga uchumi wetu. suala la umeme lingeweza kutengemaa kwa kiasi hiko.
 
I do not get it! If Tanzania can get Dollars 400million to contribute to the group, why don't it go alone and work out projects which are pending in Tanzania? These countries are among the poorest and have the same level of development, what value will they add to each other; why an individual country not take issues alone? Why all this bureaucracy?

eti tunasubiri wawekezaji kwenye umeme na wakati hela tunayo $400m.Inchi yako iko kwenye giza unajidai unataka kutoa $400m.

kwa kweli huo mkutano ni urembo, media attention wanatafuta.
 
That sounds like political posturing to me!
Reasons:
1. I do not believe that any of the 5 named countries ever enjoyed a good economic period ever. If what happened since independence (or even before) is regarded as a good economic period then whenwas it bad?
2. I do not believe that these 5 presidents can do anything differently from what they have been doing for years (some decades), and they have got nothing to show for!
3. Let's say each one gives some money to a common fund, how are they then going to divide and share? How do they choose which projects to invest in? Above all, the needs are so huge I doubt that they can do anything short term to compensate for the DONATIONS that all 5 have gotten so used to since years immemorial!!

It all sounds like a joke, if not political posturing!
 
eti tunasubiri wawekezaji kwenye umeme na wakati hela tunayo $400m.Inchi yako iko kwenye giza unajidai unataka kutoa $400m.

kwa kweli huo mkutano ni urembo, media attention wanatafuta.

Priorities zetu zimekaa kichwa chini miguu juu kutokana na kuwa na viongozi dhaifu na wasiojua nini kipewe priorities katika kuleta maendeleo ya nchi yetu.
 
Sioni lolote la maana linaloweza kusaidia nchi hizo kujikwamua kutokana na kimbunga cha mtikisiko wa uchumi duniani. Mipango kama hiyo si ya kufanywa wakati huu. Mipango hiyo inaweza kusababisha nchi chache kati ya hizo kufaidika na nyingine kupata hasara kubwa.

Kinachotakiwa sasa, ni kuangalia nini kinachoweza kuongeza pato dogo lililopo kutosheleza mahitaji ya nchi zinazotuzunguka na ziada kuuzwa nchi za mbali zaidi. Msukumo mkubwa ni lazima uwe kwenye kilimo na nishati.

Inatakiwa Tanzania ianze kuwekeza kwa makusudi kabisa kwenye kilimo cha kisasa. Serikali inaweza kuanzisha mashamba au kuwezesha wakulima kulima kwa utaalam na kwa kutumia zana za kisasa ili kuzalisha mazao ya chakula kwa wingi na kwa ubora unaotakiwa.

Serikali ni lazima iweke lengo la kukidhi mahitaji ya umeme kwa asilimia 50 ifikapo Dec 2009.

Mipango ya kujenga highways kuunganisha nchi 5 za Afrika Mashariki haiwezi kuleta tija kama nchi hizo zote zina ukwasi wa pesa. Unaweza kujenga highways hizo, zisitumike inavyotegemewa na hivyo kuwa hasara kubwa.
 
Hivi mambo kama kupunguza Income tax ya wale wanaopata less than 300,000 kwa mwezi kwenda 0%, si muhimu kustimulate uchumi??

Benki Kuu ya Tanzania haiwezi kupunguza Tbills Interest rate to almost zero kama huku ili interest rates za mabenki zishuke na kuchochea mikopo kwa wananchi???

Kama Serikali ikiacha kununua magari na vitu vingine nje na kuwekeza kwenye barabara, mahospitali, mashule si ndio mambo ya muhimu??

Yeye JK anadhani mikutano kama ya G20 ili mradi unaonekana kwenye TV ndio muhimu??

Wenzake hao wote nchini mwao wameshaweka mikakati maalamu ya kustimulate uchumi wao, then wanakuja mikutanoni kumake sure nchi nyingine zinafanya kama wao.

Sasa TZ JK hajafanya kitu cha maana, mikutano ya nini?? Hivi hao kina Museveni hata wakimuuliza haya muaandaaji mkutano wewe Tanzania umefanya nini na sisi tuige, si itakuwa aibu???
 
Rais wenu ni kama kiberenge anapenda sana kuwa chairman wa vikao visivyo na tija kwa saana, si heri angepewa Bob Geldof. Hivi huwa anaongea bollocks gani huko? He has been around the world for more than 80 days since 2006 lakini mpaka hii leo jiii anapigwa tu madude kila kukicha. Zero kabisa.
 
Sioni lolote la maana linaloweza kusaidia nchi hizo kujikwamua kutokana na kimbunga cha mtikisiko wa uchumi duniani. Mipango kama hiyo si ya kufanywa wakati huu. Mipango hiyo inaweza kusababisha nchi chache kati ya hizo kufaidika na nyingine kupata hasara kubwa.

Kinachotakiwa sasa, ni kuangalia nini kinachoweza kuongeza pato dogo lililopo kutosheleza mahitaji ya nchi zinazotuzunguka na ziada kuuzwa nchi za mbali zaidi. Msukumo mkubwa ni lazima uwe kwenye kilimo na nishati.

Inatakiwa Tanzania ianze kuwekeza kwa makusudi kabisa kwenye kilimo cha kisasa. Serikali inaweza kuanzisha mashamba au kuwezesha wakulima kulima kwa utaalam na kwa kutumia zana za kisasa ili kuzalisha mazao ya chakula kwa wingi na kwa ubora unaotakiwa.

Serikali ni lazima iweke lengo la kukidhi mahitaji ya umeme kwa asilimia 50 ifikapo Dec 2009.

Mipango ya kujenga highways kuunganisha nchi 5 za Afrika Mashariki haiwezi kuleta tija kama nchi hizo zote zina ukwasi wa pesa. Unaweza kujenga highways hizo, zisitumike inavyotegemewa na hivyo kuwa hasara kubwa.

Investment in agriculture has to go hand in hand will improvement of rural infrastructure. I agree your points but just an additional to that.
 
Rais wenu ni kama kiberenge anapenda sana kuwa chairman wa vikao visivyo na tija kwa saana, si heri angepewa Bob Geldof. Hivi huwa anaongea bollocks gani huko? He has been around the world for more than 80 days since 2006 lakini mpaka hii leo jiii anapigwa tu madude kila kukicha. Zero kabisa.

..............ha ha haaaaaaaaaaaaa, man I like your arguments. Utterly such kind of aruments are potentially very good for those who needs change. The thing is the guys can not forecast the outcome Vs costs of hosting the meeting for issues that can domestically tabled
 
Nilikuwa siku zote nawambia marafiki zangu wa nchi nyengine za kiafrika na ulaya kama watafatilia nchi yangu tanzania watagunduwa jambo moja ambalo siku zote serekali yake imekuwa wakipada wagoni kuiga kwa mfano uk leo hii watapitisha sheria au kufanya mabadiliko fulani haichuwi muda tanzania nawao watafanya takriban kama walilofanya uk sasa hapo unajiuliza hivi viongozi hawa hawana akili na mbinu zao wenywe mpaka wasubiri wakoloni wao ndio nawao wafanye na leo hii naimani watanikubalia na maneno yangu kama ni kweli huo mkutano wa g5 upo na aliyeleta mpango huo hakuna mwengine isipokuwa kwa mara nyingine tena ni mr rais kiwete wa jamuhuri ya tanzania
 
Utawala wa sultan hauna mawazo mapya haukubali ushauri wala hautumii rasilimali zilizopo ila unakula mali za umma
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete anatarajiwa kuongoza mkutano wa nchi tano za Afrika ya Mashariki katika kile ambacho kinaaminiwa juhudi ya nchi hizo kukabiliana na mmonyoko wa kiuchumi duniani. Mkutano huo utakaozihusisha nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi unatarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi huu au mapema mwezi wa tano



- Kama ni kweli atakuwa kiongozi wa G5, basi itakuwa plus sana kwa bongo hii ni safi, mazuri tuwe tunakubali sometimes jamani, hii ni plus kwa taifa letu, ila tu apunguze safari.

FMES!
 
Africa Mashariki na kati ndio eneo masikini sana duniani. Kama sio G5 ya nchi masikini sana duniani, I don't know what it's.
 
Labda ndiyo wanataka kujikwamua toka kwenye huu umasikini; unajua ukiangalia kwenye resources yawezekana we are one of the richest areas on earth..
 
Raisi akizungumzia neno misaada!, watu mnakuja juu, akichukua hatua ili kujikwamua kwa kujitegemea, watu mnakuja juu, ningekuwa mimi Kikwete kwa hoja zenu hizi dhaifu ningewacheka halafu kimoyomoyo ningejisemea "these people dont know what they are talking about".
kaalika nchi chache, lakini nchi nyingine zenye uchumi mzuri kidogo kuliko sisi
zinawania kushiriki hamuoni kuwa hili ni jambo positive.

Acheni hoja za Chuki, na msifuate mkumbo, kuweni huru wa fikra siyo kila kitu mnalaumu tu, Hili la kikao ni muhimu sana, kwa sababu hizi nchi za jirani tunafanya nazo biashara kwa hiyo ni lazima mipango isukwe kuona tunajiokoa vipi kutoka katika hili tatizo la economic crisis iliyoikumba dunia.

DOWN WITH ARROGANTS, HATERS, WHINNERS, THUMBS UP FOR TRUTH SEEKERS AND POSITIVE CONTRIBUTORS
 
Mwanakijiji acha kuchora watu.
Mimi naamini umeandika wewe ili uwashitue akili wachangamke. Kuna tofauti kubwa kati ya hizo pointi hapo juu na speech iliyotolewa majuzi. Kama ni kweli itakuwa safi, maana inakuwa kama tumefinywa kutoka usingizini.
Zaidi ya miaka 4 hivi balozi aliyekuwa hapa UK alishasema hiyo ya mabarabara (spichi nzima yeye alitoa directions from northi tu sauthi bigi rodisi), ila mpaka leo sijaona application zaidi ya ajali kuzidi na raisi kusema mapenzi ya Mungu. Huyu Mungu anawependa watanzania kinoma noma tu.
Hayo mambo uliyosema, teenager anaweza kufikiria, ila kwanini viongozi wa Tanzania hawaoni haya inashangaza sana. Halafu sijui wana wasiwasi gani wakati Gavana wa BoT mwaka jana alisema Tanzania iko shwari na credit crunch.
 
Back
Top Bottom