Excel kupanga matokeo, divisions na points

Hill tatizo baada ya kukopy formula kwenye celi zingine linasababishwa na mini jamani

0562625ba56803d04df25f44a8bfc2dd.jpg
 
Screenshot_2017-01-14-21-14-08.png
Njia ya pili na ambayo itabadilisha points na division ukibadili marks za mwanafunzi.
Sasa kwanza download excel yangu hapo inayoitwa "Mfano Marks" halafu tuelekezane. (Kwa bahati mbaya office yangu ni 2007, pengine tunaweza kupishana kama una version ya mbele).
Utaona ina tabs tatu (Original, Points na Final) Kwenye excel tabs zinaweza kuongezwa na kupewa majina.
View attachment 453675

1. Kwenye Tab ya kwanza, utaona nimeweka table original zenye marks za wanafunzi, pamoja na vi-refference table viwili. Kimoja cha points na kingine cha divisions.
(By the way :- Unaweza pia kuweka kila kitu kwenye tab moja ila kazi itakua pana sana, kama unajua mbinu za kuhide cells inakua vizuri pia)
2. Kwenye tab ya Pili nimetengeneza Table ya vlookup.
Nimefanyaje.
Kwanza nikiwa hapo kwenye "tab" ya "points", nimeclick cell ya kwanza kabisa ambayo ni A1. Nikaweka alama ya swasawa "=". Nikaenda kwenye tab ya Original, nikaclick cell ya A1 ambayo ni "Student name" kisha nika bonyeza enter, Student name ikaja kwenye A1 ya tab ya Points. Nika click cell hiyo na kuivuta kwa kikona kwenda pembeni hadi mwisho. kama 0 zikitokea umepitiliza, zifute.
View attachment 453682
Kisha nika-select Student name na Sex hapohapo, nikazivuta kwenda chini kwa mtindo huo huo.
View attachment 453685
Nikaenda kiboksi cha kwanza juu kushoto C2 kenye tab hiyo hiyo ya Points, nika-click na nikaanza kuandika formula yangu ya vlookup.
Nikaandika hivi
=vlookup( kisha nikaclick tab ya original, halafu nikaclick C2 pale original, nikabonyeza mkato (coma). Baada ya hapo natakiwa niweke table array, nikaselect table B yote isipokua heading yake, kisha nikaboyeza F4 kuweka alama ya Dollar, nikabonyeza mkato tena, halafu nikaandika 3 kwamba ninachotakiwa kupata hapo ni points column ya tatu, mkato tena, halafu nikaandika true Nikafunga mabano. nikapress enter. Kwenye kiboksi C2 kwenye tab ya points ikaja point. Nikaiselect kisha nikaidrag kushoto kisha chini kama kawaida kujaza viboksi vya points vilivyo baki.
Kisha hapo hapo kwenye tab ya points nikaongeza column za columns za Points na divisions
3.Kwenye divisions nikatumia utaratibu wa Sum na small kama maelekezo awali.

4. Kwenye division nikaandika vlookup namna hii
Kwanza nikaclick kiboksi cha kwanza ambacho ni M2, kisha nikaandika =vlookup( kisha nikaclick kiboksi cha nyuma yake ni L2, nikabonyeza mkato, kisha nikaclick tab ya original, nikaselect table C yote isipokua heading, kisha nikabonyeza F4 kuweka alama za dola, kisha nikaweka mkato tena, nikaandika 2 kisha mkato, nikaandika true kisha, nikafunga mabano, kisha nikabonyeza enter. Division ikaja kwenye kiboksi cha M2 kwenye tab ya points. Nikaishika kwa kona nikaidrag chini kama kawaida kujaza viboksi vyote.

5. Kwenye tab ya final cell A1, nikaweka alama ya "=" Kisha nika-click tab ya points, na pale nikaclick cell ya kwanza yaani A1, nikabonyeza enter, Student name ikaja kwenye cell ya A1 kwenye tab ya final. Nikadrag kushoto, kujaza, kisha nika select student name na Sex, nikadrag chini kama nilivyo fanya awali kwenye tab ya points.
Nikaenda kwenye tab ya points tena. nikaclick cell ya somo ya kwanza juu kushoto, yaani C2. Nika-right click kisha nika-copy. Nikaenda kwenye tab ya final kwenye C2 nika-paste. Ikaja function ya vlookup niliyotumia kwenye tab ya points. Nikaenda kwenye kipengele cha 3 cha function hiyo ya vlookup, nikabadili 3 kuwa 2, kisha nikabonyeza enter. Kwenye kiboksi cha C2 kwenye tab ya final ikaja "A" ambayo ni mark ya mwanafunzi Chungwa Tamu katika somo la Biology.
View attachment 453690
Nika drag kushoto kisha chini kama kawaida kujaza viboksi vyote

6. Kwenye kiboksi cha L2 kwenye tab ya final, ambacho ni points za mwanafunzi Chungwa, nikaweka alama ya sawasawa "=" , kisha nika-click tab ya points nikaclick pale kiboksi L2, kisha enter. Points za mwanafunzi chungwa zikatokea pia kwenye kiboksi cha L2 kwenye tab ya final. Nikadrag kushoto hadi usawa wa division, kisha nikadrag zote chini hadi mwisho kujaza points na division kwenye tab ya final. Kitu kikawa kimetokea na mabadiliko yoyote ya marks yatakayo fanyika kwenye tab ya original tatatokea kila mahali.
View attachment 453691
Ndefu sana, lakini jaribu kuielewa. Usisahau kudownload excel yenyewe
Nimefanikiwa mkuu ahsanteh sana!!
Screenshot_2017-01-14-21-14-39.png
Screenshot_2017-01-14-21-14-27.png
 
Samahani, kuna mahali nimeona nimeongeza mabano hapo.
Hivi =SUM(SMALL(E28:M28,{1,2,3,4,5,6,7})) ingetosha. Haya mabano ya mwisho yanafunga yote yaliyokua yamefunguliwa mwanzoni.
Nimesikia kuwa kwenye version nyingine za excell, pengine chini ya office 2007 "{ } haikubali, sijajaribu maana sina 2003 na chini yake.
Lakini kwa urahisi kabisa inaweza pia kuandikwa kama hivi. =SMALL(E28:M28,1)+SMALL(E28:M28,2)+SMALL(E28:M28,3)+SMALL(E28:M28,4)+SMALL(E28:M28,5)+SMALL(E28:M28,6)+SMALL(E28:M28,7) inakuja pia

View attachment 453378

Manake ni namba ndogo kabisa iliyo kati ya E28 na M28, jumlisha namba ya pili kwa udogo katika mstari huo huo wa E28:M28, jumlisha namba ya tatu kwa udogo etc hadi 7
View attachment 453381
Hii formula nyingine ni ya kufupisha tu lakini kama inazingua afadhali kupitia parefu.

Vipi kama ana F katika Maths anapigwa penati ya kwenda Div III
 
Umetumia nguvu nyingi. Kama ungetumia IF function, the job could have been done within a minute
 
Dah sijui nikulipe nini kwa elimu hii aisee, mungu akubariki sana. Akuongezee na akulinde

sent by mwenyewe
 
kazi nzuri sana, nimekuelewa sana. Vipi kale kautaratibu ka zamani ka penalty, tunaweza kufanya vipi?
Namimi nlikuwa naswali kama wewe umeniwahi mkuu, kama baadhi ya masomo ni compulsary kama mathematics ambayo ufaulu au ufeli they have to be counted inakuwaje

sent by mwenyewe
 
Mimi pia ningependa kujua utaratibu wa penalty unafanyikaje kwa kutumia formula.
 
Back
Top Bottom