EWURA yasitisha bei mpya za mafuta

EWURA yasitisha bei mpya za mafuta

MPUNGA MMOJA

JF-Expert Member
Joined
May 30, 2015
Posts
304
Reaction score
402
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetangaza kusitishwa kwa bei mpya za mafuta zilizotangazwa jana ambazo zilipaswa kuanza kutumika leo tarehe 1 Septemba.
Serikali imeelekeza bei za mafuta za mwezi uliopita kuendelea kutumika.

======

Serikali imeelekeza EWURA kusitisha bei mpya za mafuta zilizopaswa kuanza kutumika leo Septemba 01, 2021 na zile ambazo zilikuwa zinatumika mwezi Agosti ziendelee kutumika

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Godfrey Chibulunje amesema, "Serikali imeunda Timu Maalum kwa ajili ya kuangalia bei zinavyopangwa na viashiria mbalimbali vinavyosababisha bei iendelee kwenda

Ameongeza, "Bei za zamani zitaendelea kutumika mpaka pale Timu Maalum ambayo imeundwa na Serikali kupitia na kutoa majibu"
 
Ni siasa au uhalisia ndio umeazingatiwa?

Tujipe muda kujua nini kime-determine bei kama ni professionalism au ni siasa inahusika.

Bei inaweza kupanda au kushuka kutegemeana na bei katika soko la dunia au sera zetu za kikodi humu nchini.

Wacha tusubiri.
 
Mkuu huna source ya habari hii?
Wakuu EWURA imetangaza kusitisha bei mpya za mafuta zilizoanza kutumika leo Septemba Mosi 2021, na kuagiza bei za mwezi Agosti kuendelea kutumika.

Mama ameamua kuwa mkali kwa EWURA akiwachekea mambo yatakuwa magumu.
 
Back
Top Bottom