Ewe mwanamke hebu njoo unipe jibu hapa!!!!!!

Ewe mwanamke hebu njoo unipe jibu hapa!!!!!!

Eiyer

JF-Expert Member
Joined
Apr 17, 2011
Posts
28,259
Reaction score
20,914
Hebu chukulia tu kwamba ulikuwa na boy friend ambae mlikuwa pamoja toka secondary halafu mkamaliza pamoja masomo yenu[a level] na kwenda kuendelea na maisha na baada ya muda mkaamua kuoana,maisha ya mke na mume yakaanza.

Baada ya kumaliza masomo mlifanikiwa nyote kupata kazi sehemu tofauti

Baada ya hapo wewe ukawa unajiendeleza kimasomo zaidi na ukafanikiwa kuongeza elimu yako hiyo na kupanda kiwango,kwa upande mwingine mumeo akawa busy na maisha mengine,hakupenda kuendelea kwani yeye aliridhika na elimu aliyokuwa nayo

Kitendo cha wewe kuongeza elimu yako kilikufanya ukapandishwa cheo kazini kwako kitendo kilichoongeza kipato chako kuwa kinono sana,mshahara wako ukawa ni mara 5 ya mshahara wa mumeo,ila kwa kipindi chote mlichokuwa pamoja mlikubakiana msipate kwanza mtoto ili uweze kupata muda mzuri wa kujiendeleza kimasomo

Kitabia mumeo sio mtu wa watoto[wanawake] ni mpole sana na huwa anaonesha kukujali sana kiasi kwamba mtu akija anaweza kudhani umemloga,yaani ni kama goigoi fulani hivi

Pia kwenye upande wa maamuzi ni mzito sana yaani kukiwa na tatizo anachukua muda sana kuamua yeye kama mwanaume hadi wakati mwingine unaingilia kati,yaani huduma ya maji inaweza kuondolewa hapo nyumbani kama yeye ndie alikuwa na jukumu la kulipia au kusimamia ulipaji,pia kutokana na udogo wa kipato chake mara nyingi wewe umekuwa ukichangia karo za watoto na hata mahitaji ya nyumbani kwa kiwango kikubwa sana,na hili wala halioneshi kumkera hata kidogo mumeo yeye anaona ni sawa tu

Mmefanikiwa kujenga nyumba ambayo haijaisha lakini gharama za ujenzi wa nyumba hiyo wewe umegharamia kwa 90% na imebakiza mambo madogo tu mhamie

Kutokana na shughuli unayofanya kuna wakati unachelewa kurudi nyumbani na kumkuta anakusubiri na wala haoneshwi kukerwa na hili,anaona sawa tu

Kwenye familia wewe ndio unaonekana kama mhimili wa hiyo familia kutokana na wewe kuwajibika kwa kiasi kikubwa kwenye mambo mbalimbali

SWALI NI HILI:
Ikitokea ukapewa fursa ya kubadili mume,je utamuacha huyu?
Na kwanini?
 
nimeisoma hii thread kwa umakin...lakin nimeona kuna vitu vitanifanya nisimuanche huyu mwanaume...

No body is perfect..nitaachana na huyu anaechelewa kutoa maamuzi..ntaenda kwa anae act immedietly

lakin ni kiwembe tena kile Gillette..We should learn to appreciate what we have..not what we don't have

He loves ME..yes.I love him yes why leaving such a nice man


Hana pesa nying but he contribute something to our life that's okay....Most men are NATURAL LEADERS they just step

back when their wives think they want to be the leaders..Mbona hakuact hivo when we were boyfriend what If I am the

SOURCE!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!I will consider some facts before I pull the PLUG..
 
nimeisoma hii thread kwa umakin...lakin nimeona kuna vitu vitanifanya nisimuanche huyu mwanaume...

No body is perfect..nitaachana na huyu anaechelewa kutoa maamuzi..ntaenda kwa anae act immedietly

lakin ni kiwembe tena kile Gillette..We should learn to appreciate what we have..not what we don't have

He loves ME..yes.I love him yes why leaving such a nice man


Hana pesa nying but he contribute something to our life that's okay....Most men are NATURAL LEADERS they just step

back when their wives think they want to be the leaders..Mbona hakuact hivo when we were boyfriend what If I am the

SOURCE!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!I will consider some facts before I pull the PLUG..

Hii imetoka moyoni au kinywani?

Maana nyie ni watata sana!
 
nimeisoma hii thread kwa umakin...lakin nimeona kuna vitu vitanifanya nisimuanche huyu mwanaume...

No body is perfect..nitaachana na huyu anaechelewa kutoa maamuzi..ntaenda kwa anae act immedietly

lakin ni kiwembe tena kile Gillette..We should learn to appreciate what we have..not what we don't have

He loves ME..yes.I love him yes why leaving such a nice man


Hana pesa nying but he contribute something to our life that's okay....Most men are NATURAL LEADERS they just step

back when their wives think they want to be the leaders..Mbona hakuact hivo when we were boyfriend what If I am the

SOURCE!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!I will consider some facts before I pull the PLUG..

Wakati mwingine huwa napenda mawazo yako Aunt,but hofu yangu ni implementations...maana takwimu zinaonesha wanamama wenye contribution kubwa katika kurise family wana nyodo sana (most of em) Hamchelewi hata kuwaleta wanaume zenu reserve nyumbani...
 
huyu si goigoi, ni muungwana, hats babu yangu alikuwa hivi na bibi aliendelea kumpenda maana ile kazi ya ndoa alikuwa anaitekeleza kwa moyo wote.
 
Wakati mwingine huwa napenda mawazo yako Aunt,but hofu yangu ni implementations...maana takwimu zinaonesha wanamama wenye contribution kubwa katika kurise family wana nyodo sana (most of em) Hamchelewi hata kuwaleta wanaume zenu reserve nyumbani...

Most of them that mwans NOT ALL...what if among those Few........

kuna vitu huwa nawazaga sometimes acha tu.....lakin with this scenario nimekuwa mtu

tofauti sanaa.....
 
huyu si goigoi, ni muungwana, hats babu yangu alikuwa hivi na bibi aliendelea kumpenda maana ile kazi ya ndoa alikuwa anaitekeleza kwa moyo wote.

Babu yako kuwa hivyo hakuhalalishi hayo!
 
Back
Top Bottom