European Parliament Orders Museveni to resign from Power before is Crashed

chadema jifunzeni jinsi ya kuongea bungeni oneni wabunge wenzenu wanavyoongea.Kwana wameandika hoja zao.Halafu wanaongea kwa nidhamu na direct to the point.chadema huwa mnaongea kama wavuta bangi bungeni
 
Tusubiri tuone! Mbona huko Yemen na kwingineko ndio wao wanapiganisha vita na kusababisha mauaji makubwa kila uchao ? Jana tu Spain imeamua kuendelea kuuzia nchi za kiarabu zinazo iaangamiza Yemen guided missiles ! Ee mungu tunusuru na wazungu hawa wasilete vita Uganda !
Inaonekana ww hata mlio wa bunduki haujawahi sikia
Na ndiyo maana kwenye suala la reasoning unakuwa na negative thoughts kabla toa hoja zenye msingi mkuu sio unatanguliza uoga mbele.
 
Sikubaliana na vitendo alivyofanyiwa Bob wine lakini hamna kitu nachukia kama Wazungu kutuambia cha kufanya. Kama Waganda wakifika boiling point watamtoa huyo Mzee.
Kwa maana nyingine ni kwamba ungependa yatokee yaliyotokea Rwanda
 
chadema jifunzeni jinsi ya kuongea bungeni oneni wabunge wenzenu wanavyoongea.Kwana wameandika hoja zao.Halafu wanaongea kwa nidhamu na direct to the point.chadema huwa mnaongea kama wavuta bangi bungeni
Sio chadema, wabunge wote wa vyama vyote.
 
Sikubaliana na vitendo alivyofanyiwa Bob wine lakini hamna kitu nachukia kama Wazungu kutuambia cha kufanya. Kama Waganda wakifika boiling point watamtoa huyo Mzee.
Hakika katika mazingira ya sasa lazima watu wenye akili wanapata taabu sana kuamua nani aungwe mkono. Watawala wetu wamegeuka kuwa miungu watu, wanakandamiza haki za watu wao, wanauwa na kuwatesa kana kwamba wanaoteswa ni binadamu daraja la chini la watesi wao! Dunia ikisubiri kila kitu kiharibike, ni dhadhari watu wengi watateseka na kufa. Yaliyotokea Rwanda mwaka 1994/95, yalitotokea Uganda mwaka 1978 hadi kung'olewa madarakani kwa nduli Idd Amin Dadaa kwa msaada wa majeshi jasiri ya Tanzania, hayawezi kuruhusiwa yajirudie tena. Hayo yote yaliyotokea Uganda, Rwanda, Somalia yamegharimu maisha ya binadamu wengi. Mnataka hili lijirudie kwa nia ya kutoingilia uhuru wa taifa la Uganda? Uhuru gani kwa wanaokandamizwa na kuteswa? Uhuru gani kwa familia zilizopoteza wapendwa wao kwa kosa moja tu, la kuwakosoa viongozi walioko madarakani?

Kama mataifa yetu yangekuwa na mfumo wa kupambana na udhalimu wa ndani kwa ndani kusingekuwepo sababu ya mataifa ya nje kuingilia kati. Lakini mfumo huo uko wapi? Umoja wa mataifa unaendelea kulaumiwa kwa kutofanya chochote kuzuia mauwaji na Kimbali ya Rwanda! Mauaji kama hayo yanapokuja kutokea dunia nzima hujumuishwa kutafuta misaada ya kibinadamu kuwasaidia waathirika. Kwanini isikemee( European Union) mapema dalili za uvunjifu wa amani zinapojitokeza? Uhuru wa anayeuwawa uko wapi dhidi ya muuwaji wake? Siuoni.
 
Sikubaliana na vitendo alivyofanyiwa Bob wine lakini hamna kitu nachukia kama Wazungu kutuambia cha kufanya. Kama Waganda wakifika boiling point watamtoa huyo Mzee.

Mbona haya yanatokea hata hapa Tanzania|?
Kitendo alichofanyia Robert Kyagulanyi a.k.a. Bobi Wine hakina tofauti na alichofanyiwa Tundu Lissu na wapinzani wengine.
Unaposema unachukia Wazungu kutuambia cha kufanya nakushangaa sana..!!!Mbona mambo mengine ya Wazungu wakiwaambia mnayafanya? Kuna misaada kibao ya KIUCHUMI, KIELIMU, KIULINZI na KIAFYA tunaletewa na tunaipokea mbona hiyo hatuchukii au kuikataa?? Tuache unafiki. Tatizo la Watawala wa Kiafrika wakiambiwa wasinyanyasa WAPINZANI wanachukia lakini wakiletewa misaada wanachekelea mpaka gego la mwisho linaonekana..!!Pambaf.
 
Sio chadema, wabunge wote wa vyama vyote.
Wameongea kwa utaratibu kwa kuwa hili wanaloliongelea halihusu maisha yao moja kwa moja. Linaihusu Africa. Waangalie wanapoongelea suala la wakimbizi kuingilia katika nchi zao. Waangalie wanapoongelea ugaidi ndani ya nchi zao! Waangalie wanapoongelea suala la Briexit . Kwanini mtu atokwe povu na suala linaloongelewa linahusu tawala za africa dhidi ya waafrica?
 
Waje na Huku Tanganyika, tunatawaliwa kinguvu na CCM kwa kutumia kiini macho cha Demokrasia fake ya ukandamizaji. EU ikiwezekana leta hata jeshi fukuza huyo mpuuzi anayelitumia jeshi kwa manufaa yake
 
Pumbavu zao, wanataka kuja kuivuruga uganda na eneo zima la afrika mashariki kwa kisingizio cha demokrasia wakati wanalenga maslahi ya kisiasa na kiuchumi, laana ya ushoga inawatafuna
 
Sikubaliana na vitendo alivyofanyiwa Bob wine lakini hamna kitu nachukia kama Wazungu kutuambia cha kufanya. Kama Waganda wakifika boiling point watamtoa huyo Mzee.

Kwanza ninapinga Raisi asiyena kikomo cha kuwa madarakani, Museveni anastahili kustaafu.

Ndugu Wile , EU NA nchi zote kama zinakuwa msaada wa maendeleo ama kusaidia Bajeti ya nchi yako, wana haki kukuingilia, kwani unatumia msaada wao kukusaidia ku tawala.

Pili unapoharibu mfumo wa utawala NA kuwadhulumu wananchi NA kuwatesa, ndipo tunaona watu wengi wakikimbia nchi zao, wengi wetu tunakimbilia nchi za ulaya, NA hilo linawahusu kwa wakimbizi waniongezea gharama nchi zao.

Mkimbizi kutoka Burundi hapendelei kukimbilia Rwanda ama Congo.

Tumewapa wazungu haki ya kutuingilia, iwapo hatujitoshelezi NA tutaendelea kuwahitaji
 
Back
Top Bottom