EU yatangaza vikwazo vipya dhidi ya Moscow

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,482
9,242
Halmashauri Kuu ya Ulaya imependekeza leo vikwazo vipya dhidi ya Urusi, ikiwemo marufuku ya ununuzi wa makaa ya mawe.

Katika vikwazo vinavyopendekezwa, ambavyo mataifa ya Umoja wa Ulaya lazima yaidhinishe, vitazuia uagizaji wa bidhaa za Urusi zenye thamani ya euro bilioni 9 na uuzaji nchini Urusi wa bidhaa za thamani ya euro bilioni 10, zikiwemo kompyuta na kuzizuia meli za Urusi kuingia katika bandari za Umoja wa Ulaya.

Rais wa Halmashauri ya Ulaya Ursula von der Leyen amesema wanapanga kupiga marufuku uagizaji wa mafuta pia. Hayo ni kutokana na ushahidi wa kuuawa raia katika mji wa Ukraine uliokuwa umekamatwa na Warusi.

Tangazo hilo limekuja saa chache baada ya meya wa mji mkuu wa Ukraine Kyiv Vitali Klitschko kutoa wito wa kusitishwa mahusuano yote ya kibiashara na Urusi kwa kile alichokiita kuwa kusitisha usambaaji wa fedha za umwagaji damu."
 
Vikwazo vyovyote atakavyo weka EU havito muumiza Russia, bali vitaendelea kuwaumiza wananchi wao. Yaani kama US na EU wangekuwa wanashikilia hewa ya Oksijeni mpaka sasawangekuwa washaizuia Russia may be wangeiumiza Russia lkn ndio hivyo vingine Russia alisha jiandaa navyo.

Vikwazo vyao vya kipuuzi havimuumizi Russia, ila kikwazo kimoja tena sio kikwazo kwani Russia hajamzuia mtu kununua mafuta na gesi bali kabadilisha utaratibu wa kununua kwa hela yake, still wananchi wao wa EU na US gharama za maisha zimepanda, je angesema afunge mafuta na gasi si wangetafutana.
 
Vikwazo vyovyote atakavyo weka EU havito muumiza Russia, bali vitaendelea kuwaumiza wananchi wao. Yaani kama US na EU wangekuwa wanashikilia hewa ya Oksijeni mpaka wangekuwa washaizuia Russia may be wangeiumiza Russia lkn hivyo vingine Russia alisha jiandaa navyo...
Zifatazo ni kampuni zilizosepa urusi, Google, Amazon, Pepsi, Coca-Cola, Apple, Nike, Master card,visacard, Instagram, YouTube, Facebook, Boeing, Nissan, Toyota, hakuna kununua makaa ya Mawe,n.k hizo kampuni ziliajiri warusi wengi so wamekosa ajira, na capital flow imepungua so Urusi sio mungu lazima vikwazo vitamuathiri Sana tu
 
Zifatazo ni kampuni zilizosepa urusi, Google, Amazon, Pepsi, Coca-Cola, Apple, Nike, Master card,visacard, Instagram, YouTube, Facebook, Boeing, Nissan, Toyota, hakuna kununua makaa ya Mawe,n.k hizo kampuni ziliajiri warusi wengi so wamekosa ajira, na capital flow imepungua so Urusi sio mungu lazima vikwazo vitamuathiri Sana tu
Hebu niambie Urusi alivyo badilisha utaratibu wake wa kuuza gesi kwa hela yake, vipi kampuni za huko EU na US pamoja na wananchi wao wana hali gani?

US kaweka vikwazo kote ila kwenye mbolea ya Russia hajaweka vikwazo,ushajiuliza kwa nini?

Vipi kesho Russia akiweka vikwazo wananchi wake US watakuwa na hali gani?
Halafu hapo unazungumzia chakula sio YouTube, Facebook, Apple, Coca-Cola, Boeing,Nissan na Toyota ambazo sio muhimu kwele mwili wa binadamu,hizo ni luxury needs na si basics needs.
 
Hizo Kampuni zilikuwa huko kufanya biashara au kutoa misaada ya kibinadamu?

Zenyewe kuondolewa kwa mashinikizo ya Serikali zao kunaziongezea Faida au hasara? Kodi ambazo wangelipa kwny nchi zao zitaongezeka au kupungua kwa kuondoka kwao?

Hizo Kampuni ziliajiri warusi pekee au kuna Raia wa Mataifa yao nao watakosa kazi?

Pia kumbuka

Russia anasambaza bidhaa za lazima kama Mbolea, dawa, gas, fuel n.k

Ulaya wao wanasambaza mambo ya Tweeter, facebook sijui Cococola, sijui products za Apple n.k

Zifatazo ni kampuni zilizosepa urusi, Google, Amazon, Pepsi, Coca-Cola, Apple, Nike, Master card,visacard, Instagram, YouTube, Facebook, Boeing, Nissan, Toyota, hakuna kununua makaa ya Mawe,n.k hizo kampuni ziliajiri warusi wengi so wamekosa ajira, na capital flow imepungua so Urusi sio mungu lazima vikwazo vitamuathiri Sana tu
 
Sasa inayumba vipi wakati vyote vipo kwake.kuna soda za kirusi,computer za kirusi.sasa nani anakomoka.iyo google walikuwa wanatumia asilimia 40 ya warusi.kule yandex ndo inatumika sana.kwa iyo wameipa kampuni ya yandex kutumika kwa asilimia 100
Yaani Google wasepe, Coca-Cola wasepe, Pepsi, Nike, Amazon, no visa card, master card, no kuuza mafuta no kuuza makaa ya mawe afu useme Urusi haitayumba,
 
Zifatazo ni kampuni zilizosepa urusi, Google, Amazon, Pepsi, Coca-Cola, Apple, Nike, Master card,visacard, Instagram, YouTube, Facebook, Boeing, Nissan, Toyota, hakuna kununua makaa ya Mawe,n.k hizo kampuni ziliajiri warusi wengi so wamekosa ajira, na capital flow imepungua so Urusi sio mungu lazima vikwazo vitamuathiri Sana tu
Mbuzi kabisa hii,watu wanalia gharama za maisha,ikiwemo chakula kua juu wewe unazungumzia instagram kuondoka urusi? Kwaio apo ulipo unakula instagram.?
 
Hii vita inadhihirisha jinsi Russia ilivyo na influence katika nyanja mbali mbali duniani.
Marekani alipoivamia Iraq, Afghanistan na Libya hizi tabu hazikutokea
Nadhani hata USA angewekewa vikwazo pasingekua na mabalaa ya kupanda kwa gharama za maisha kama ilivyo sasa
We all underestimated the influence of Russia in geopolitics, and now we are paying the price of our ignorance.
 
Vikwazo vyovyote atakavyo weka EU havito muumiza Russia, bali vitaendelea kuwaumiza wananchi wao. Yaani kama US na EU wangekuwa wanashikilia hewa ya Oksijeni mpaka wangekuwa washaizuia Russia may be wangeiumiza Russia lkn hivyo vingine Russia alisha jiandaa navyo.

Vikwazo vyao vya kipuuzi havimuumizi Russia, ila kikwazo kimoja tena sio kikwazo kwani Russia hajamzuia mtu kununua mafuta na gesi bali kabadilisha utaratibu wa kununua kwa hela yake, still wananchi wao wa EU na US gharama za maisha zimepanda, je angesema afunge mafuta na gasi si wangetafutana.
Vikwazo vitaiumiza EU kwa kiasi fulani ila vitaiumiza Russia zaidi long-term. Kusema kuwa vikwazo havitoiumiza kabisa Russia si kweli.

Russia inahitaji kuuza nje hasa nishati ambapo mteja wake mkuu ni EU. Inahitaji mapato kutokana na mauzo hayo kwaajili ya kuendesha nchi kiuchumi. Hata hiyo issue ya "kununua gesi kwa hela yake" ambayo ilizua mjadala mwanzoni, haipo tena kwa sasa sababu itakwamisha mapato. Utaratibu wa sarafu ni uleule wa awali wa euro.
 
Hii vita inadhihirisha jinsi Russia ilivyo na influence katika nyanja mbali mbali duniani.
Marekani alipoivamia Iraq, Afghanistan na Libya hizi tabu hazikutokea
Nadhani hata USA angewekewa vikwazo pasingekua na mabalaa ya kupanda kwa gharama za maisha kama ilivyo sasa
We all underestimated the influence of Russia in geopolitics, and now we are paying the price of our ignorance.
Angewekewa US ingekuwa balaa lingine maana karibia mifumo ya fedha na makampuni mengi ya tech tunzotegemea ni ya kwao.
 
Zifatazo ni kampuni zilizosepa urusi, Google, Amazon, Pepsi, Coca-Cola, Apple, Nike, Master card,visacard, Instagram, YouTube, Facebook, Boeing, Nissan, Toyota, hakuna kununua makaa ya Mawe,n.k hizo kampuni ziliajiri warusi wengi so wamekosa ajira, na capital flow imepungua so Urusi sio mungu lazima vikwazo vitamuathiri Sana tu
Mbona huongelei jinsi watu wa magharibi wanavyoteseka chakula kimepanda, gas na oil?
 
22 Reactions
Reply
Back
Top Bottom