Eti uchochezi, uchochezi gani?

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
97,988
Reaction score
142,388
Hizi habari za uchochezi mimi sizielewi kabisa.

Hao watu wanaotuhumiwa sijui kuchochea, wamechochea kitu gani?

Kumpindua Magufuli?

Huyu jamaa asipoangalia anaweza kutumia muda wake mwingi kupambana na watu wenye maoni na hisia ambazo zipo kinyume na atakavyo au apendavyo yeye.

Katika viongozi ambao Tanzania imewahi kuwa nao tokea tuanze kutawaliwa na CCM huyu jamaa atakuwa anaongoza kwa kutokuwa na busara wala hekima.

Hovyo kabisa!

Sitashangaa JF nayo ikifungiwa kwa kupromoti uchochezi wa akina Ngabu😉.
 

Labda sijui kiswahili vizuri Kwani kuchochea ni kosa?

Upinzani Kigoma wadaiwa kuchochea maendeleo

Nikichochea maendeleo nitakamatwa ?🙄
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…