Eti shetani kanipitia!!!!?

streat Anthem

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2016
Posts
395
Reaction score
476
Moja ya kauli ambazo watu wengi hutumia kujiplease pale wanapofanya jambo baya ni hii ya shetani kumpitia mtu.
Huwa najiuliza unakuwa wapi pale hichi kitu kinachoitwa shetani kinapokupitia?

Je huwa kinakupitia kwa usafiri gani?
Huwa unakitaarifu ili kikupitie au kinajileta chenyewe?.
Na Kikikupitia huwa kinakupeleka na kukurudisha au kinakuacha huko huko?

Je na wewe ulishawahi kukipitia?

Ili mtu akupitie lazima muwe mnajuana kabla au kufahamiana, je hichi kitu huwa mnafahamiana nacho mpaka kiwe na mazoea ya kukupititia?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hiyo ni moja ya njia ya binadamu kujifariji/kujitoa kwenye hatia lkn si kwamba watu wote wanapotenda kitu kibaya hawajitambui,no wanajijua ila hutumia kujieleza hivyo kama kujiokoa.. lkn moja kati ya swali nalopenda kuwahoji watu hasa wa dini,ni kama wanasema shetani ndo anawatendesha kwanini hiyo hukumu asipewe shetani pekee bali nayeye anapewa..?

Dini/imani imewasaidia wengi hasa wale wasiokuwa na uwezo wa kuhimili vitu vizito! Mf:unakuta mtu anamzigo wa mawazo,shida,magonjwa,kazi,umaskini n.k anakuwa anajifariji kutokana na imani yake kuwa ipo siku mungu wake atamsaidia n.k so hiyo inaleta hope kubwa tu,tofauti na mtu asieamini/ubongo wake ndo solution au mtu fulani ikitokea ikashindikana kutatuka shida basi mtu huyu kama ni mwepesi anaweza kujiuwa ama kujidhuru kwa namna yoyote.
 
Ni unafik tu...

Sent using Jamii Forums mobile app from my Andoid phone
 
Ni porojo.
Pia, huo ndiyo unafiki wa dini zote kwa kumsingizia sijui pepo, mara jini oooh oooh, shetani.
Kwa hiyo, watu wanafanya mambo kwa makusudi ila wanamsingizia ibilisi!!!
 
Shetani anasingiziwa mambo mengi sana aisee, nadhani hata mungu anachukizwa na hiki kitendo cha shetani kusingiziwa kila baya. Jamani shetani nae ni kiumbe, mpunguzieni mzigo.
 
Mkuu umetoa maelezo mengi ila haujamsaidia mleta mada kumuelewesha ni nini maana ya kupitia na shetani.
 
Ni porojo.
Pia, huo ndiyo unafiki wa dini zote kwa kumsingizia sijui pepo, mara jini oooh oooh, shetani.
Kwa hiyo, watu wanafanya mambo kwa makusudi ila wanamsingizia ibilisi!!!
Mkuu mada inazungumzia mtu kupitiwa na shetani ila wewe unazungumzia habari za dini.

Msaidia mleta mada kuelewa huko kupitiwa na shetani hasa ndiyo inakuaje?
 
Mkuu mada inazungumzia mtu kupitiwa na shetani ila wewe unazungumzia habari za dini.

Msaidia mleta mada kuelewa huko kupitiwa na shetani hasa ndiyo inakuaje?

Chanzo cha shetani si ni hizo dini za wazungu koko na waarabu pori?
Hao si ndiyo wamemtengeneza Mungu na Shetani kwa wakati mmoja?.
Hizo ni porojo za kujitakia eti shetani kakupitia.
 
88% ya walimwengu niwa shetani

Sent using Jamii Forums mobile app


Hakuna cha shetani wa Mungu wa mapepo.

Ni mawazo tu ya watu hasa wazungu koko na waarabu pori wamekamata watu wengine akili watu wanaishi kwa uoga na kumsingizia aidha Mungu au Shetani .
Mfano, ajali ikitokea wengine wanasema ni mipango ya Mungu, wengine utasikia kwenye ajali ile ile wanasema mara eti oooh oooh, ni mipango ya Mungu wengine shetani kasababibisha.

Mimi huwa sielewi.

Kwa hiyo mwisho, nikaona kuwa hakuna wote wawili.
 
Chanzo cha shetani si ni hizo dini za wazungu koko na waarabu pori?
Hao si ndiyo wamemtengeneza Mungu na Shetani kwa wakati mmoja?.
Hizo ni porojo za kujitakia eti shetani kakupitia.
Mleta mada anataka kujua kupitiwa na shetani hasa ndiyo inakuaje? sidhani kama kataka kujua nani aliyemtengeneza shetani,hata jambo la uongo pia lina elezwa na mtu anaelewa ila wewe unaona habari za shetani ni uongo ila hujui ni vp maana ya mtu kupitiwa na shetani na pengine ndiyo maana huwezi kuelezea.



Halafu pia mkuu sasa kama hizo dini ni za wazungu na waarabu ilikuwaje zikawepo mataifa mengine wasio wazungu wala waarabu?
 
watu bwana kila dhambi inayofanyika kuna mkono wa shetani, hadi shetani mwenyewe anashangaa

be___blessed
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…