Eti mke bora hutoka kwa mungu?

Seto

JF-Expert Member
Jan 15, 2011
953
53
HILI SWALA KIUKWELI SILIELEWI NA NAONA KILA MTU ANALITAFSIRI KIVYAKE.

  1. WENGINE WANASEMA ETI WANAOMBA HALAFU ROHO MTAKATIFU ANAMWONYESHA KWENYE MAOMBI HUYO MKE NDO ANAMFUATA NA KUMWELEZ ETI MUNGU KAMCHAGULIA YEYE...UHAKIKA UPO WAPI HAPA?
  2. WENGINE WANASEMA ETI UNAENDA KWA WATUMISHI WA MUNGU WANAKUELEKEZA ETI MKEO YUPO HIVI NA HIVI UENDE SEHEMU FLANI UTAKUTANA NAYE. LAKINI HAPA NDO UTATA ZAIDI, KWANI UTAKUTA YULE MKE NAYE AMEAMBIWA TENA NA MCHUNGAJI/PASTA HUYO HUYO NAYE AENDE HAPO ATAMPATA MUME, ....HAKA SI KA-MOVIE KAINA FLANI JAMANI?
Sasa huyo mke anapatikana vipi?
 
Aisee, vipi yule dada umefikia uamuzi gani. Unamuoa au unamuacha.
Unataka mke/mke mwema?

Unawalaumu watu wanofundisha habari za mke mwema anatoka kwa Mungu au?

Hiyo thread yako imekaa kibiashara zaidi sijui?

Natamani ipelekwe kule kwenye jukwaa la dini, halafu tukaongee vizuri huko.
 
aisee, vipi yule dada umefikia uamuzi gani. Unamuoa au unamuacha.
unataka mke/mke mwema?

Unawalaumu watu wanofundisha habari za mke mwema anatoka kwa mungu au?

Hiyo thread yako imekaa kibiashara zaidi sijui?

Natamani ipelekwe kule kwenye jukwaa la dini, halafu tukaongee vizuri huko.


bado...
 
Suala la Imani you either believe it or not.... Hakuna proof kwahiyo inabidi uichukulie kama ilivyo kama unaamini au uchukulie kwamba ni uongo kama hauamini...., hakuna mtu under the sun ambaye atakupa concrete evidences..
 
Suala la Imani you either believe it or not.... Hakuna proof kwahiyo inabidi uichukulie kama ilivyo kama unaamini au uchukulie kwamba ni uongo kama hauamini...., hakuna mtu under the sun ambaye atakupa concrete evidences..

OK.

 

Ukweli ni kwamba sidhani kama muumba aliumba watu wabaya ambao hakutaka wao wapate waume au wake, na nina uhakika hawezi akakuchagulia wewe mbaya alafu akamuacha yule mzuri ili nimchukue mimi..., all in all nadhani sometimes huwa tunajiroga wenyewe alafu tunasingizia muumba.
 
Mungu ndiye muumbaji wa viumbe vyote, tukiwemo sisi wanadam wake kwa waume, kwa hyo mume au mke mwema anatoka kwake.
 
Muombe Mungu kama UNAAMINI,siku zote naamini Mungu anatujua vizuri na anajua akupe nani ili uweze kuishi maisha yenye amani na yanayomtukuza.......wewe muambie hitaji lako,then mpe nafasi kwa namna yake atakukutanisha na mwenzi wako.....umuombe pia akusaidie kumtambua na kumpokea.....:coffee: kama huamini basi utakutana nae tu,mi naamini hata wasio amini ni watoto wa Mungu so najua atakupa tu mke.......:coffee:
 
Anajiiiibu maombi...
Anajiiiibu maombi...
Anajiiiibu maombiiiii.....,,.,.
 
ndugu unahitaji darasa pana sana la mambo haya. miss judith leo simuoni, yuko wapi? hebu mPM inaonekana amelala muamshe aje atumalizie huu utata
 
Just for Argument Sake.....
Hivi kuna kitu kama mke asiye bora?
Na kama yupo ni nani ambaye anafaa amuoe huyo?
Na kama Mungu anatupenda wote sawa, kwanini anichagulie mimi mke mbaya na wewe akupe mzuri?
Na je Mke akiwa bora na katikati ya ndoa akawa mapepe na hapo ni nani wa kulaumiwa?
Na wewe kama sio bora, je unahitaji mke bora?, kwanini huyo mwanamke bora abebe mzigo wa wewe ambae sio bora?

Haya ni baadhi tu ya maswali kwa yeyote awezae kunijibu....

Asanteni
 
Huo ni ulimbukeni na kutojiamini,mke bora halafu uende kwa mchungaji au pasta akuombee,wengi wao ndiyo wanaonja kidogo then wanakupa wewe ni uongo mtupu,jiaamulie kusoma kitabu cha Mungu cha imani yako muombe Mungu na kisha funga na pia angalia yupi akufaaye the utaona tu kuwa fulani unampenda na kikubwa ni mazingira,KAMA UPO MORO HUWEZI KUOA BUKOBA AU MTWARA,DEFINITELY UTAOA MORO AU DAR,PWANI,IRINGA AU DOM MAENEO AMBAYO MACHO YAKO YANAFIKA KWAHARAKA NA KIRAHISI
 
Just for Argument Sake.....
Hivi kuna kitu kama mke asiye bora?
Na kama yupo ni nani ambaye anafaa amuoe huyo?
Na kama Mungu anatupenda wote sawa, kwanini anichagulie mimi mke mbaya na wewe akupe mzuri?
Na je Mke akiwa bora na katikati ya ndoa akawa mapepe na hapo ni nani wa kulaumiwa?
Na wewe kama sio bora, je unahitaji mke bora?, kwanini huyo mwanamke bora abebe mzigo wa wewe ambae sio bora?

Haya ni baadhi tu ya maswali kwa yeyote awezae kunijibu....

Asanteni

VOR, Binafsi ninavyoona hakuna mke mbaya wala mume mbaya. Kila binadamu ameumbwa kwa tabia yake, na namna yake sijui niseme na Hulka yake.

Mume/mke anaweza akawa mbaya kwa huyu kumbe angeliishi na mwingine wangeendana tu vizuri.

Apart from hizi tabia nyingine mbaya kama uzinzi, ulevi nk nk, lakini tabia nyingine tunazo tumejikuta tu tunazo, mfano hasira,uchoyo,nk nk. Sasa kuna mtu anaweza akachukuliana na hasira alizonzoa mtu lakini mwingine hawezi, kuna mwingine anaweza akachukuliana na mtu mchafu, rafu rafu mwingine hawezi. Kuna mtu anaweza akachukuliana na mtu mlevi mwingine hawezi.

Tukumbuke kila mwanadamu ana udhaifu wake, JE mimi naweza kuchukuliana na udhaifu wa mwenzangu. Kama nikiweza tunaishi bila mikwaruzo, ukiniudhi najua jinsi ya kukueleza tunamaliza, nikikosea unajua kunirekebisha na ninakuelewa. Lakini kama huwezi kunielewa, na mimi sikuelewi huyu sio mke/mume mwema kwako, maisha yatakuwa ya ubishi na visasi kila siku.


Ndio maana sasa tunatakiwa kumuomba Mungu kwa bidii ili atukutanishe na yule ambaye mnaendana.
Na huyu ni Mungu pekee anaweza kwa sababu wengi tunaingia kwene ndoa sio kwa sababu nimeona naweza kuishi na huyu mtu na tukaenda sawasawa, ila wakati mwingine tunasukumwa tu na vitu vya nje kama vile uzuri, fedha, elimu, haja ya kuoa/kuoa nk nk nk.

Hebu jaribu kufikiria wewe ni mume wangu ukapatwa na hasira juu ya jambo fulani halafu ukaona njia sahihi ni kumuua huyo aliyekukosea, ukaniambia mimi kama mkeo nikakuambia twende tukamuue kabisa mume wangu na Rungu hili hapa, hivi nitakuwa msaidizi mzuri ktk hili kweli. Natakiwa nijue jinsi ya kuishusha hasira yako, kukupunguzia mastress badala ya kuyaongeza nk nk.

Mke/mume huyu ni mwema kwako????

Naishia hapo niko tayari kwa maswali zaidi.
 
kuna vitu vingine huwa haviuliziki...na huwa napata shida sana na mtu ambae huwa ana viuliza.....ahsante!
 
Back
Top Bottom