Eti fedha hutokaje serikalini kwenda kwa wananchi?

ego

JF-Expert Member
Apr 10, 2013
1,620
1,407
Nimesoma gazeti moja linauliza hivi pesa hutokaje serikalini kwenda kwa wananchi? na nikadhani tunaweza kujadili sote

Binafsi kwa uelewa wangu pesa huwa inazunguka na kuzunguka kwa pesa maana yake ni kutoka sehemu moja ikapita kule na kule na kurudi sehemu hiyo hiyo ilipoanzia huo ndio mzunguko kwa lugha ya ki layman.

Sasa mizunguko ya pesa huwa ina njia zake zinazopitisha mizunguko ya pesa. Pesa hizi zikipita kwenye mizunguko inayogusa watu wengi basi kila pesa zinakopita wale ziliowapitia huwaachia neema wale watu wanaokuwa kwenye sehemu ambazo pesa hazipiti basi hawa hulia njaa.

Chukua mfano wa baba mwenye familia akiwa na kipato, akiamua kutumia pesa nyingi kwenye pombe basi baba huyu hujenga jina baa na kuonekana kwa walevi kama mtu anayewapa neema wadau walioko kwenye sekita ya mabaa lakini yawezekana nyumbani watoto wanalia njaa na maendeleo binafsi hakuna lolote.

Yupo baba anayeamua kuweka kipaumbele chake kuwa matumizi ndani ya familia, mshahara wake wote watakula vizuri, watavaa vizuri watajirusha kadiri wawezavyo lakini hafanyi uwekezaji wa kimaendeleo au kutembelea sehemu kama mabaa. Huyu naye familia yake itamuona baba bora kwa raha za mda mfupi huku kimaendeleo akibaki palepale, anastaafu hana nyumba wala biashara fedha yote alikuwa anakula.

Yupo baba ambaye wakati anasoma chuo alikuwa anapewa hela ya kula hali anaweka pesa yote ili aje kufanya kitu cha maendeleo, amemaliza chuo kaajiriwa pesa yote kawekeza kwenye kujenga maghorofa huku watoto wakiugua kwashiakoo na watu wazima wakiwa na vidonda vya tumbo.

Serikali ni mfano wa baba katika familia, pesa yote ni mali ya serikali, mizunguko ya pesa huanzia kwake na kumalizikia kwake.

Swali la msingi ni serikali inayokuwa madarakani ni ya aina gani ndio maisha wanayoishi wananchi wake.

Kama serikali inayokuwa madarakani ni sawa na baba mlevi anayepeleka pesa yote kwenye baa ambapo kama vile vitendo vya ufisadi, mradi unagharimu bei mara mbili ya gharama halisi ni wazi walevi ambao tunaweza kuwaita mafisadi ndio wataiona serikali hiyo ya maana sana huku wananchi wakilia na nchi kutokupiga hatua kimiundombinu.

Kama serikali inayokuwa madarakani inaamua kutumia fedha tu na wanafamilia kula vizuri, kuvaa vizuri basi bila shaka wananchi wake wataiona serikali hiyo ya maana sana kwa maana kila mwananchi anapata mahitaji yake kwa wepesi.

Na kama serikali itaamua kuwa baba anayeshinda njaa na watoto kushinda njaa ilimradi amejenga jina mtaani kuwa ana ghorofa ni wazi kwa nje wataonekana familia yenye uwezo lakini wakiishi maisha ya umasikini.

Swali linabaki kuwa je maendeleo ni nini? au serikali bora ni ipi?

kwa mtizamo wangu maendeleo ni lazima yapimwe kwa kutazama living standard ya watu. Living standard ya watu inapimwa kutokana na purchasing power kwa maana kila kitu kinategemea pesa. Uko na pesa kiasi gani mfukoni ndiyo kipimo cha utaishi maisha gani.

Kama layman ambaye si mchumi kama ningekuwa nimepewa jukumu la kuinua uchumi wa watanzania basi ningeweka vipaumbele vifuatavyo

1. Kipaumbele cha kwanza kingekuwa kuinua kipato cha watanzania.
2. Kipaumbele cha pili kingekuwa kila mtanzania ni lazima alipe kodi
3. Kipaumbele cha tatu kingekuwa ujenzi wa miundombinu
4. Huduma muhimu za kijamii
5. Mambo yote ya kijamii

Kwa kuwa swali la msingi limeuliza kwa kutegemea malalamiko ya wananchi na majibu ya wenyewe basi hatuna budi kujikita huko.

Binafsi ninadhani serikali imeweka kipimo cha maendeleo kuwa
1. Ujenzi wa miradi ya maendeleo na matokeo yake ni fedha zinazokwenda kwenye miradi hii hazigusi jamii ya watanzania walio wengi.
2. Serikali imedhibiti fedha nyingi ambazo zilikuwa zinaingia kwenye jamii kupitia sekita ambazo tunaweza kusema ni za kilevi.
3. Serikali haijapandisha mishahara kwa miaka
4 Mfululizo huku rundo la kodi likiongezeka hivyo hata kipato ambacho kilikuwa kinabaki kwa watu kufanya manunuzi yao kimepungua zaidi.

Principaly binafsi siikubali sana falsafa ya kiuchumi ya awamu ya Tano. ninaiona kama falsafa ya kutengeneza uchumi wa "machinga complex" yaani unajenga uchumi wa miundombinu huku ukiua purchasing power ambayo matokeo yake ni kuwa na miundo mbinu bora kama ya jengo la soko la machinga complex huku miundombinu hiyo ikishindwa kufanya biashara.

Binafsi nakubali falsafa ya wape watu pesa nyingi lakini walipishe kodi ya kutosha na wape majukumu ya kutosha. yaani kupata pesa iwe ni rahisi lakini kuishi pia kunahitaji pesa nyingi hivyo pesa anazopata ntu hazikai na hiyo ni kuongeza kasi ya mzunguko wa pesa ili transactions ziwe nyingi sana kuongeza kodi na ajira na hapa nina uhakika ujenzi wa miundombinu kama kipaumbele cha tatu baada ya kukusanya kodi naona kitafanikiwa.
 
Mimi nadhani Kama kungekuwa na miradi mikubwa ya Kilimo wanachi wangenehemeka Sana .. Miradi mingine yote ingebaki kama ilivyo ila KILIMO na UFUGAJI seikali Kama ingesaidia watu kuwachimbia visima vya kiliko na scheme za Kilimo ili wasitegemee mvua nchi nzima ... Naamini ndani ya miaka miwili watu wasingelia njaa.


Hapo serikali ingeweka Sera za kuuza mazao nje na kutunga sheria za Kuwabana walanguzi wa mazao maana wanawafanya wakulima kuwa masikini tu ... Ningekuwa raisi ningeunda kikosi kazi Kama KMKM kule Zanzibar kazi yake Ni kudeal na watu wote wananajisi Kilimo na kuwafanya wakulima kuwa masikini wakiwemo madalali.
 
Kwa serikali kulipa madeni ya ndani kwani wafanyabiashara watatumia hizo hela kununua au kufanya investment kwa hiyo hela itaingia kwenye mzunguko.Wakati wa Mkapa alikuwa anatenga fedha za anawakopesha watumishi wa serikali hasa wanajeshi na waalimu.Ukiwapa hela za mkopo wa miaka miwili let say utakuta wanajenga nyumba (mabati,cement ,mchanga ,atalipa mafundi etc) itakuwa ndani ya nchi na biashara zitakuwa unaongeza mzunguko wa hela.Watanunua vitu around community nk.Kuna kitu kinaitwa "stimular package" inatakiwa itengenezwe na serikali kustimulate uchumi bila kuleta madhara yoyote nk.Hayo ni machache tu jinsi serikali inavyoweza ku inject fedha kwenye system na sio kama interpretation ya Rais kuwa sigawi pesa
 
tunachotofautiana hapo ni vipaumbele tu, kwangu mimi kipaumbele cha kwanza ni Miundombinu ndio mengine yafuate kwa mpangilio ulioupanga.
 
Kwa upande wangu naona hela kutoka Serikalini kwenda kwa wananchi ni kupitia mishahara iwe ya Watumishi wa Umma au Sekta Binafsi zinazopewa kandarasi na Serikali
 
benki za kibiashara ndizo zenye jukumu la kusambaza pesa (fiduciary issuer) kwa niaba ya serikali/benki kuu. njia ambazo serikali hutumia ili kuhakikisha kuwa upatikanaji au uwepo wa fedha sokoni unaendana na hali ya uchumi ni kama ifuatavyo

1)benki kuu hutoa treasury bills na kuziuza kwa taasisi za fedha au yoyote ile na kwa mtuu yeyote mwenye sifa. kila bill/kipande kimoja huuzwa 10,000/tsh na baada ya miezi mitatu wanunuzi hulipwa hela zao kwa faida ya riba mf 10% so kila kipande kitalipwa 11,000/tsh. faida ni tsh 1000 ambayo mnunuzi letus say ni benki hunufaika na kuongeza uwezo wake wa kukopesha, kumbuka mkopo huongeza upatikanaji wa pesa mtaani

2)serikali kuhifadhi pesa zake katika benki za biashara
hii husaidia benki kupunguza kiwango cha riba kwa wateja wake wanaokopa tofauti kama chanzo cha pesa ikiwa ni mkopo toka sehemu nyingine.
3kuwianisha matumizi makubwa/capital na madogo/current expenditure
makubwa ni yale ya mitambo etc na madogo ni mishahara,posho vyakula etc
matumizi makubwa huhamisha pesa na kupeleka nje wakati madogo husambaza pesa kwa wananchi, hivyo makubwa yakiwa kinyume na uwiano/ratio kwa madogo basi lazima pesa ipotee mtaani
 
Swali lako lipo kwenye kipaombele chako namba moja.

Hebu tuambie uchumi wa mwanachi mmoja mmoja utauinua vipi.?
 
Kwa upande wangu naona hela kutoka Serikalini kwenda kwa wananchi ni kupitia mishahara iwe ya Watumishi wa Umma au Sekta Binafsi zinazopewa kandarasi na Serikali

hili ni sahihi, mishahara na marupurupu mbalimbali kwa watumishi ndiyo malipo yanayogusa watanzania waliowengi zaidi.

yaani serikali ikilipa mishahara kila mtumishi anasatawanyika na kwenda kwenye maeneo yake kufanya manunuzi. kama ni chakula, kama ni mavazi, kama ni ujenzi mitaani.

Serikali ikipandisha mishahara maana yake inaongeza vitu vinavyonunuliwa na hawa, lakini serikali hii haitaki kabisa kupanua wigo wa Transactions bali inapiga kodi mtandao ilioukuta na fedha zinapelekwa katika sekita ambazo asilimia kubwa haiendi kwa wananchi.

mfano ukipeleka bilioni 1 katika kijiji kama mishahara baada ya miezi michache kijiji hicho biashara mbalimbali zitashamiri lakini ukipeleka bilioni moja kujenga hospitali baada ya miezi sita kijiji kitakuwa na hospitali lakini maisha mengine ya kijiji hicho yatabaki kama yalivyokuwa isipokuwa vijana wachache walioshirika kwenye ujenzi utakuta wamebadilisha makazi

Ndio maana binafsi nikasema naamini kupeleka bilioni moja katika kijiji kama mishahara au mapato yanayosambaa kwa watu wengi na watu hawa kuwatoza kodi kujenga mindombinu katika kijiji hiki. nina uhakika nikipeleka bilioni 1 ktika kijiji kupipa mishara kwa maana ya mfano milioni 300 kwa mwezi, ndani ya miaka 10 kijiji hiki kitakuwa kimepiga hatua kuwa sana kimaendeleo, kuliko kutegemea kuwajengea hospitali ya bilioni moja kama miundombinu itakayokuja kuchochea maendeleo baada ya miaka 10 kijiji hiki kinaweza kuwa bado kiko nyuma na jengo tu.

Sina maana ya kwamba kujenga miundo mbinu sio vizuri bali nina maana tunahitaji kubalansi ili tuwekeze kodi zetu kutengeneza more taxes, more transactions huku sehemu nyingine tunayopata tukijenga miundombinu pia. Kwa serikali kutokuongeza mishahara, kutokutokutoa ajira mpya, kukata marupurupu, huku ikiongeza kodi ni kama kupunguza mtaji unaozalisha kodi na ajira.

Mategemeo yetu ni kuona kiwango cha fedha kinachotumika kununuliana bidhaa mitaani kikiongezeka mwaka hadi mwaka. naamini kiwango hicho kikiongezeka automaticaly transactions zitaongezeka na ajira zitaongezeka.

chukua mfano mdogo wa maji

kama mtu ataweka tenki A, la maji la lita 1,000,000. akaruhusu watu 1000 waje kila mmoja na tenki B la lita 1000 na kila mwenye tenki B lita 1000 analipa lita 300 kwa mwenye tenki A na kugawa maji lita 200 kila wenye mapipa C, wenye mapipa C wagawe kwa wenye ndoo D zenye lita 20 huku wakilipa maji lita 60 kwa mwenye tenki A.

Hii inaitwa tree diagram na ndiyo mfumo wa mzunguko wa fedha ukiwa na transactions na kodi

ukiongeza uwezo wa tenki A maana yake kwa viwango vilevile unaongeza wingi wa wenye matenki B, ukiongeza wingi wa wenye matenki B ndivyo wenye matenki C nao watakavyoongezeka mpaka wale wa mwisho wanaopata lita 20, hapoha maji yanayotozwa kwa kila anayepewa maji kurudi kwa mwenye tenki A yataongezeka

Lakini tunaweza kuona awamu ya tano wanaamini katika kubakiza tenki lile lile, yaani kiwango cha pesa kilichokuwa kikitumika kulipa mishahara kibaki vilevile, ikiwezekana kipunguzwe kwa maana marupurupu mengi yameondolewa.
lakini pia wanajaribu kuongeza kiwango cha maji yanayotozwa kwa kila mpokea maji maana yake ukisema kila mpokea lita 1000 alipe lita 400 kwa mwenye tenki A huyu anabaki na lita 600 ambazo atagawa kwa watu 3 tu wa lita 200. anayepokea lita mia mbili akilipa maji mengi zaidi kwa tenki A unapunguza watu watakaopatiwa lita 20.

kwa staili hii huwezi kukuza biashara ndio maana nikaita uchumi wa machinga complex

tupo tunaotamani kama 2015 tulikuwa na tenki la 1,000,000 tukigawa maji basi target yetu namba moja tuwe na tenki la 2,000,000 ifikapo 2020 kwa maana ya kwenye mfuko wetu wa kulipa mishahara na marupurupu. na kile tunachokikusanya kutoka huku kama kodi kama 2015 kilikuwa Z basi 2020 tunaweza kuwa tumefikia 3Z
 
Serikali inapotekeleza miradi katika maeneno mbalimbali kama Halmashauri, Mikoa, Wakandarasi wazawa fedha hizi hupelekwa na kufanya kazi kupitia Wakandarasi wazawa. Hawa wakandarasi wazawa huajiri vibarua kwa maelfu na hununua vifaa/bidhaa kwa mabillioni kutoka kwa wafanyabiashara mbalimbali kwa hiyo hizi fedha husambaa mpaka kwa mtu wa chini. Kibarua ataenda kununua nyanya, dagaa n.k. mwenye duka pia atawalipa wafanyakazi wake ataenda sokoni, ataenda kwenye mahoteli kuburududika tayari fedha hizi za Serikali zinasambaa kwa wote na wengi wataifaidi. Hivi sasa miradi mingi inatekelezwa kwa force akaunti wananchi hawaifaidi. Miradi mikubwa inatekelezwa na makampuni ya nje na fedha hizo zinapelekwa kwao hivyo ni fedha kidogo ambazo zinazunguka..
 
Jitahidi kuhudhuria mikutano yake na uwe unalialia kuomba ‘maiki’, huchelewi kuambulia mapesa ukaonje mema ya nchi.... japo sijasoma ulichoandika bali heading tu.
 
benki za kibiashara ndizo zenye jukumu la kusambaza pesa (fiduciary issuer) kwa niaba ya serikali/benki kuu. njia ambazo serikali hutumia ili kuhakikisha kuwa upatikanaji au uwepo wa fedha sokoni unaendana na hali ya uchumi ni kama ifuatavyo

1)benki kuu hutoa treasury bills na kuziuza kwa taasisi za fedha au yoyote ile na kwa mtuu yeyote mwenye sifa. kila bill/kipande kimoja huuzwa 10,000/tsh na baada ya miezi mitatu wanunuzi hulipwa hela zao kwa faida ya riba mf 10% so kila kipande kitalipwa 11,000/tsh. faida ni tsh 1000 ambayo mnunuzi letus say ni benki hunufaika na kuongeza uwezo wake wa kukopesha, kumbuka mkopo huongeza upatikanaji wa pesa mtaani

2)serikali kuhifadhi pesa zake katika benki za biashara
hii husaidia benki kupunguza kiwango cha riba kwa wateja wake wanaokopa tofauti kama chanzo cha pesa ikiwa ni mkopo toka sehemu nyingine.
3kuwianisha matumizi makubwa/capital na madogo/current expenditure
makubwa ni yale ya mitambo etc na madogo ni mishahara,posho vyakula etc
matumizi makubwa huhamisha pesa na kupeleka nje wakati madogo husambaza pesa kwa wananchi, hivyo makubwa yakiwa kinyume na uwiano/ratio kwa madogo basi lazima pesa ipotee mtaani

kwa pointi yako ya Tatu mabenki yenyewe yanatoa Capital lakini pesa za matumizi ya kila siku anayedetermine ni serikali inayotunga sera na kanuni na kuweka mipango ya uchumi.

mabenki hayatoi pesa ya kwenda kununua nyama kupika bali yanatoa pesa kwa mfanyabiashara ambaye amegundua wateja wenye fedha ya kununua nyama ni wengi hivyo akifungua bucha la nyama litamlipa, huyu ndiye mteja wa benki.

Yaani kitu namba moja katika biashara ni soko kwa maana ya wanunuzi na hapa ndipo tunasema kipaumbele cha kwanza katika serikali kiwe mwaka 2019 kama tuna watanzania wenye vipato vya kati "middle income" milioni 5 basi tuweke target ya kufikia 2025 tunataka watanzania middle income wawe 10m. Tukiwatengeza hawa hayo mambo mengine yatajiseti yenyewe maana kila wakizaliwa wapya mahitaji ya bidhaa na huduma mtaani yataongezeka, watakopa wenyewe na kufungua biashara na kuwavuta wengine kutoka chini zaidi kufika maisha ya juu kupitia ajira rasmi na zisizo rasmi.

ki msingi uchumi ni kama mduara hivyo mambo yote yanaonekana kuwa linked together hivyo wapi pakuanzia popote huonekana hakuna tofauti kwa kudhani popote mtu anashika patavuta sehemu nyingine tu, lakini cha msingi ni kujua ukiwa na gurudumu limeninginia kuna sehemu ukishika ukavuta gurudumu litaenda mbele kwa kasi, kuna sehemu ukishika litaenda mbele kidogo kidogo lakini kuna sehemu ukishika ukivuta gurudumu linarudi nyuma.

tunachotafuta ni sehemu gani katika gurudumu hili la maendeleo tukishika hapo tukavuta tutaenda mbele kwa kasi ya maximum.
 
Serikali inapotekeleza miradi katika maeneno mbalimbali kama Halmashauri, Mikoa, Wakandarasi wazawa fedha hizi hupelekwa na kufanya kazi kupitia Wakandarasi wazawa. Hawa wakandarasi wazawa huajiri vibarua kwa maelfu na hununua vifaa/bidhaa kwa mabillioni kutoka kwa wafanyabiashara mbalimbali kwa hiyo hizi fedha husambaa mpaka kwa mtu wa chini. Kibarua ataenda kununua nyanya, dagaa n.k. mwenye duka pia atawalipa wafanyakazi wake ataenda sokoni, ataenda kwenye mahoteli kuburududika tayari fedha hizi za Serikali zinasambaa kwa wote na wengi wataifaidi. Hivi sasa miradi mingi inatekelezwa kwa force akaunti wananchi hawaifaidi. Miradi mikubwa inatekelezwa na makampuni ya nje na fedha hizo zinapelekwa kwao hivyo ni fedha kidogo ambazo zinazunguka..

Too general kiasi huwezi kuona ukweli

kufanya miradi sawa lakini je kweli kutopandisha mishahara, kutokuajiri watumishi wapya ni sahihi ili tujenge barabara ya miaka 50 mbele?

ni vijana wangapi unaowafahamu waliohitimu vyuoni ambao mpaka sasa wapo mitaani hawana ajira? Inashangaza hatuoni ukweli kwamba kuajiriwa au kujiari kunategemea mzunguko wa fedha tunaanza mara kulaumu mitaala ya vyuo eti haiwafundishi vijana kujiajiri, mara tunalaumu vijana wenyewe.

Ki msingi un employment sio swala la mitaala wala maamuzi binafsi kama sisi tunavyodai mikoa fulani watu ni wavivu wakiamka wanakaa kwenye vijiwe! Ni lazima tutambue anayefanya maamuzi kazi ifanyike au isifanyike sio mfanyakazi mwenyewe bali mwenye pesa. Hivyo ukiona watu wamekaa hawana wanachokifanya jua hakuna anayeweza kuwalipa kufanya chochote, wenye pesa wapo kidogo na wale wanaoweza kulipwa na hao kidogo wako bize na waliobaki hawana namna bali kukaa vijiweni. Hebu niambieni kijana kamaliza chuo kikuu ni daktari anawezaje kujiajiri? kijana kamaliza chuo kikuu ni mhandisi anawezaje kujiajiri?

kuna watu hawajawi kutafakari maisha wao wanaona ni rahisi tu, mtu katoka chuoni hana hata hela ya kupanga chumba na kula wao wanawaza afungue kidispensari ajiari mtaani. Anaanzia wapi huyu kijana?

hili swala la kujiari lingekuwa jepesi kama serikali ingetunga sera za kulirahisisha mfano madaktari wengi wakistaafu wakapewa fedha zao za uzeeni wanakwenda kufungua vidispensary, kumbe sasa serikali ikiwezekana iwape hawa fedha zao mapema wakafungue hivyo vidispensary mapema ama waajiri hawa vijana au wao wenyewe waache kazi wajiajiri huku na vijana wakaajiriwe huko.

Lakini utashangaa serikali inatunga kanuni kuchukua fedha mpaka miaka 60.

ukienda kwenye kilimo watu walikuwa wanajiajiri taratibu kwa kununua mazao na kuuza na tartibu hawa utakuta wamefika juu na ndio hao watakuja kuwa wafanyabiashara wakubwa wa kuunganisha vijiji au miji yao na masoko ya mbali lakini utasikia serikali inasema ukiwa na Tani moja na nusu lazima uonyeshe shamba umelima wapi?

1. Serikali iachie pesa za kwenda kwa wananchi kuchochea transactions ili kukuza ajira na kodi
2. Mkurabita ukijike katika kurasimisha shughuli zisizo rasmi ili kurahisisha utendaji wa kazi na ukusanyaji kodi mfano vibarua wanaweza kuwa wanaajiriwa makazini kupitia makampuni kama walinzi na haya makampuni yalipe kodi na vibarua kama walioko kwenye construction walipe kodi
3. vyama vya utambuzi na urasimishaji wajasiliamali vianzishwe na kupitia huku serikali inaweza kuwapatia faida na pia kuwalipisha kodi
4. sekita kama za madalali au vishoka si wa kupiga vita bali kurasimisha ili wafanye kazi kwa mujibu wa sheria na taratibu. wapo watu wengi ambao hawana mda wa kwenda kupanga foleni au kusumbuka kufuatilia huduma, wako tayari kutoa malipo kwa wengine ili wakahangaike na kuwaletea majibu tu, lakini serikali inachokifanya kuwacriminize hawa badala ya kuwatambua
5.
 
hili ni sahihi, mishahara na marupurupu mbalimbali kwa watumishi ndiyo malipo yanayogusa watanzania waliowengi zaidi.

yaani serikali ikilipa mishahara kila mtumishi anasatawanyika na kwenda kwenye maeneo yake kufanya manunuzi. kama ni chakula, kama ni mavazi, kama ni ujenzi mitaani.

Serikali ikipandisha mishahara maana yake inaongeza vitu vinavyonunuliwa na hawa, lakini serikali hii haitaki kabisa kupanua wigo wa Transactions bali inapiga kodi mtandao ilioukuta na fedha zinapelekwa katika sekita ambazo asilimia kubwa haiendi kwa wananchi.

mfano ukipeleka bilioni 1 katika kijiji kama mishahara baada ya miezi michache kijiji hicho biashara mbalimbali zitashamiri lakini ukipeleka bilioni moja kujenga hospitali baada ya miezi sita kijiji kitakuwa na hospitali lakini maisha mengine ya kijiji hicho yatabaki kama yalivyokuwa isipokuwa vijana wachache walioshirika kwenye ujenzi utakuta wamebadilisha makazi

Ndio maana binafsi nikasema naamini kupeleka bilioni moja katika kijiji kama mishahara au mapato yanayosambaa kwa watu wengi na watu hawa kuwatoza kodi kujenga mindombinu katika kijiji hiki. nina uhakika nikipeleka bilioni 1 ktika kijiji kupipa mishara kwa maana ya mfano milioni 300 kwa mwezi, ndani ya miaka 10 kijiji hiki kitakuwa kimepiga hatua kuwa sana kimaendeleo, kuliko kutegemea kuwajengea hospitali ya bilioni moja kama miundombinu itakayokuja kuchochea maendeleo baada ya miaka 10 kijiji hiki kinaweza kuwa bado kiko nyuma na jengo tu.

Sina maana ya kwamba kujenga miundo mbinu sio vizuri bali nina maana tunahitaji kubalansi ili tuwekeze kodi zetu kutengeneza more taxes, more transactions huku sehemu nyingine tunayopata tukijenga miundombinu pia. Kwa serikali kutokuongeza mishahara, kutokutokutoa ajira mpya, kukata marupurupu, huku ikiongeza kodi ni kama kupunguza mtaji unaozalisha kodi na ajira.

Mategemeo yetu ni kuona kiwango cha fedha kinachotumika kununuliana bidhaa mitaani kikiongezeka mwaka hadi mwaka. naamini kiwango hicho kikiongezeka automaticaly transactions zitaongezeka na ajira zitaongezeka.

chukua mfano mdogo wa maji

kama mtu ataweka tenki A, la maji la lita 1,000,000. akaruhusu watu 1000 waje kila mmoja na tenki B la lita 1000 na kila mwenye tenki B lita 1000 analipa lita 300 kwa mwenye tenki A na kugawa maji lita 200 kila wenye mapipa C, wenye mapipa C wagawe kwa wenye ndoo D zenye lita 20 huku wakilipa maji lita 60 kwa mwenye tenki A.

Hii inaitwa tree diagram na ndiyo mfumo wa mzunguko wa fedha ukiwa na transactions na kodi

ukiongeza uwezo wa tenki A maana yake kwa viwango vilevile unaongeza wingi wa wenye matenki B, ukiongeza wingi wa wenye matenki B ndivyo wenye matenki C nao watakavyoongezeka mpaka wale wa mwisho wanaopata lita 20, hapoha maji yanayotozwa kwa kila anayepewa maji kurudi kwa mwenye tenki A yataongezeka

Lakini tunaweza kuona awamu ya tano wanaamini katika kubakiza tenki lile lile, yaani kiwango cha pesa kilichokuwa kikitumika kulipa mishahara kibaki vilevile, ikiwezekana kipunguzwe kwa maana marupurupu mengi yameondolewa.
lakini pia wanajaribu kuongeza kiwango cha maji yanayotozwa kwa kila mpokea maji maana yake ukisema kila mpokea lita 1000 alipe lita 400 kwa mwenye tenki A huyu anabaki na lita 600 ambazo atagawa kwa watu 3 tu wa lita 200. anayepokea lita mia mbili akilipa maji mengi zaidi kwa tenki A unapunguza watu watakaopatiwa lita 20.

kwa staili hii huwezi kukuza biashara ndio maana nikaita uchumi wa machinga complex

tupo tunaotamani kama 2015 tulikuwa na tenki la 1,000,000 tukigawa maji basi target yetu namba moja tuwe na tenki la 2,000,000 ifikapo 2020 kwa maana ya kwenye mfuko wetu wa kulipa mishahara na marupurupu. na kile tunachokikusanya kutoka huku kama kodi kama 2015 kilikuwa Z basi 2020 tunaweza kuwa tumefikia 3Z
 
hili ni sahihi, mishahara na marupurupu mbalimbali kwa watumishi ndiyo malipo yanayogusa watanzania waliowengi zaidi.

yaani serikali ikilipa mishahara kila mtumishi anasatawanyika na kwenda kwenye maeneo yake kufanya manunuzi. kama ni chakula, kama ni mavazi, kama ni ujenzi mitaani.

Serikali ikipandisha mishahara maana yake inaongeza vitu vinavyonunuliwa na hawa, lakini serikali hii haitaki kabisa kupanua wigo wa Transactions bali inapiga kodi mtandao ilioukuta na fedha zinapelekwa katika sekita ambazo asilimia kubwa haiendi kwa wananchi.

mfano ukipeleka bilioni 1 katika kijiji kama mishahara baada ya miezi michache kijiji hicho biashara mbalimbali zitashamiri lakini ukipeleka bilioni moja kujenga hospitali baada ya miezi sita kijiji kitakuwa na hospitali lakini maisha mengine ya kijiji hicho yatabaki kama yalivyokuwa isipokuwa vijana wachache walioshirika kwenye ujenzi utakuta wamebadilisha makazi

Ndio maana binafsi nikasema naamini kupeleka bilioni moja katika kijiji kama mishahara au mapato yanayosambaa kwa watu wengi na watu hawa kuwatoza kodi kujenga mindombinu katika kijiji hiki. nina uhakika nikipeleka bilioni 1 ktika kijiji kupipa mishara kwa maana ya mfano milioni 300 kwa mwezi, ndani ya miaka 10 kijiji hiki kitakuwa kimepiga hatua kuwa sana kimaendeleo, kuliko kutegemea kuwajengea hospitali ya bilioni moja kama miundombinu itakayokuja kuchochea maendeleo baada ya miaka 10 kijiji hiki kinaweza kuwa bado kiko nyuma na jengo tu.

Sina maana ya kwamba kujenga miundo mbinu sio vizuri bali nina maana tunahitaji kubalansi ili tuwekeze kodi zetu kutengeneza more taxes, more transactions huku sehemu nyingine tunayopata tukijenga miundombinu pia. Kwa serikali kutokuongeza mishahara, kutokutokutoa ajira mpya, kukata marupurupu, huku ikiongeza kodi ni kama kupunguza mtaji unaozalisha kodi na ajira.

Mategemeo yetu ni kuona kiwango cha fedha kinachotumika kununuliana bidhaa mitaani kikiongezeka mwaka hadi mwaka. naamini kiwango hicho kikiongezeka automaticaly transactions zitaongezeka na ajira zitaongezeka.

chukua mfano mdogo wa maji

kama mtu ataweka tenki A, la maji la lita 1,000,000. akaruhusu watu 1000 waje kila mmoja na tenki B la lita 1000 na kila mwenye tenki B lita 1000 analipa lita 300 kwa mwenye tenki A na kugawa maji lita 200 kila wenye mapipa C, wenye mapipa C wagawe kwa wenye ndoo D zenye lita 20 huku wakilipa maji lita 60 kwa mwenye tenki A.

Hii inaitwa tree diagram na ndiyo mfumo wa mzunguko wa fedha ukiwa na transactions na kodi

ukiongeza uwezo wa tenki A maana yake kwa viwango vilevile unaongeza wingi wa wenye matenki B, ukiongeza wingi wa wenye matenki B ndivyo wenye matenki C nao watakavyoongezeka mpaka wale wa mwisho wanaopata lita 20, hapoha maji yanayotozwa kwa kila anayepewa maji kurudi kwa mwenye tenki A yataongezeka

Lakini tunaweza kuona awamu ya tano wanaamini katika kubakiza tenki lile lile, yaani kiwango cha pesa kilichokuwa kikitumika kulipa mishahara kibaki vilevile, ikiwezekana kipunguzwe kwa maana marupurupu mengi yameondolewa.
lakini pia wanajaribu kuongeza kiwango cha maji yanayotozwa kwa kila mpokea maji maana yake ukisema kila mpokea lita 1000 alipe lita 400 kwa mwenye tenki A huyu anabaki na lita 600 ambazo atagawa kwa watu 3 tu wa lita 200. anayepokea lita mia mbili akilipa maji mengi zaidi kwa tenki A unapunguza watu watakaopatiwa lita 20.

kwa staili hii huwezi kukuza biashara ndio maana nikaita uchumi wa machinga complex

tupo tunaotamani kama 2015 tulikuwa na tenki la 1,000,000 tukigawa maji basi target yetu namba moja tuwe na tenki la 2,000,000 ifikapo 2020 kwa maana ya kwenye mfuko wetu wa kulipa mishahara na marupurupu. na kile tunachokikusanya kutoka huku kama kodi kama 2015 kilikuwa Z basi 2020 tunaweza kuwa tumefikia 3Z
Mkuu umeelezea vizuri,. Akuna haja ya kutafuta wabobezi wa uchumi kujua Tatizo la uchumi wa Tanzania vijana wapo tayari kufanya kazi shida watu Wenye uchumi wa Kati wanabanwa kurudi kwenye uchumi wa hand to mouth..Niliwahi kuwa kwenye utafiti wa masoko na wadau flan wa nje ya Nchi hapa Tanzania mwisho waliniambia Kama serikali isipofanya mpango wa makusudi kuwainua middle class economy yaani kila Mkoa wapatikane walau watu 200-500..Wenye mitaji ya kuanzia Tzsh billion 1..Tuna safari ndefu kuja kufikia uchumi wa kueleweka..Na hapa iweleweke mitaji inaweza kuratibiwa vizuri na Benki za biashara kwa watu ambao Serikali inaona wanna potential kwenye uchumi. Kingine zile warsha semina elekezi, posho za hapa na pale vina tija Sana kwenye uchumi..Sasa amekata na Bado madawa ayako hospital..Alafu Ni Bora kumuwezesha mwananchi aweze kumlipia ada mwanae kuliko kupeleka mabilioni ya pesa Eti Elimu bure Kama Miaka hamsini ya Uhuru mwananchi awezi kulipa tsh 70000..Ya fees this is very danger..
 
Back
Top Bottom