Eti dowans kumbe imeshalipwa?

Eti dowans kumbe imeshalipwa?

Mkombozi

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2008
Posts
844
Reaction score
476
Wakuu,mwenye taarifa atujuze zaidi.Nasikia kuna kikao kilichowahi kufanyika huko bagamoyo,hela zikachotwa kila wizara,zikaambiwa zipunguze budget,hazina ikakauka.Je ni kweli imeshalipwa?Kesi mahakamani ni geresha tu.Mwenye taarifa zaidi atujuze jamani
 
yawezekana kuna ukweli fulani,
kuna jamaa yangu, yupo wizara ya bwana KAWAMBWA, alinidokezea mwanzoni mwa wiki ya jana kuwa mambo hayaendi, hawapati 'per diem' zao, wamekatwa pia masurufu na safari za nje zimefutwa hadi itakapotangazwa. Waliambiwa pia fungu lao ktk hazina litokanalo na 'other charges' lilishafyekwa. Hali mbaya, wamebakia 'kujikunyata' tu.
 
hivi huyu jk anafikiria nini kichwani mwake? rais asiye na nguvu dah wa tz tumekwisha
e
 
kuna uwezekano ikawa kweli, kwani hata wakilipwa mtajuaje? au wasipolipwa mtajuaje? ni nani anayekwenda kukagua na kuhakikishia umma kuwa hawajalipwa? inawezekan sana ikawa ni ukweli ndio maana mkwele alikaa kimya tu huku wakisema wataliipa..then mwisho anakana..huo ni uwongo mtupu
 
Kwa vile walipaji ni serikali yenyewe na tayari wengi wao waliridhia malipo hayo, huenda ni kweli. Swali ni je ikithibitishwa na umma kuwa malipo tayari yameshafanywa tufanye nini?
 
Makato ya mishahara ya wafanyakazi wa serikali yasiyokuwa na maelezo sahihi kutoka hazina ulifikiri ni ya nini?
Na bado ndugu yangu.
Kuchagua sisisemu ni maafa. Q; dr. Slaa 2010
 
Kumbuka hotuba ya JK ya mwaka mpya alivyotete kupanda kwa gharama za umeme wa Tanesco. Nafikiri pia walishaanza kulipana. wanauchumi wangetwambia pia kama uchapishaji wa noti mpya unaweza kuhusika na hili pia.
 
it is very possible, wanasema kelele za chura hazimzuii ng'ombe kunywa maji
 
Kama kilivyo kitendawili cha kurejeshwa kwa fedha za EPA ndivyo ilivyo kwa malipo ya DOWANS wakilipa kimya kimya nani atajua? Yawezekana tayari.
 
yawezekana kuna ukweli fulani,
kuna jamaa yangu, yupo wizara ya bwana KAWAMBWA, alinidokezea mwanzoni mwa wiki ya jana kuwa mambo hayaendi, hawapati 'per diem' zao, wamekatwa pia masurufu na safari za nje zimefutwa hadi itakapotangazwa. Waliambiwa pia fungu lao ktk hazina litokanalo na 'other charges' lilishafyekwa. Hali mbaya, wamebakia 'kujikunyata' tu.

Anyway... Kama haya ndiyo yalikuwa matumizi ya hizo hela, then sioni tofauti sana na kulipa Dowans...
 
Back
Top Bottom