Mfalme Daud
Senior Member
- Feb 3, 2012
- 166
- 109
Wanajanvi wenzangu, Asalam aleykum? Ninalo tena jaribu linaloitesa roho yangu. Mapenzi yanataka kunifanya, sijui? Sahibu langu ni kama ifuatavyo; miaka mitano iliyopita nilikuwa na mpenzi. Alikuwa mwanafunzi wa sekondari minikiwa mtumishi wa serikali. Nilimpenda na kumtimizia chochote alichohitaji. Kwasababu nilikuwa na mpango wa kumuoa na yeye akiwa mwanafunzi sikupenda kabisa ku"do" naye na tulikubaliana hivyo. Matokeo ya kidato cha nne yakatoka, kwake hayakuwa mazuri kwani alifeli kabisa. Ok misikujali suala la elimu kwangu hakikuwa kigezo. UKAFIKA MUDA WA KUOANA. Tulipanga miezi minne kabla sijaenda kuongeza elimu tufunge ndoa na awe wa kwangu kwelikweli. Tulipendana sana. Muda huo ulipofika nikaanza kumfuatilia ili tuanze maisha, hapo ndio utata ukaanza. Alikuwa haoneshi RESPONSE yoyote. Nilimbembeleza utadhani ndo tunaanza mapenzi, kwa kweli hakunielewa. Minikaenda Shule, baada ya miezi kadhaa nikasikia ni mjamzito. Roho iliniuma kweli lakini sikuwa na jinsi. Akawa ameolewa na jamaa alompa mimba, akaanza kumtesa. Baadaye binti akaachana na jamaa na kujifungulia nyumbani salama. Yule jamaa alishaoa mke mwingine. Huyu binti anajutia makosa aliyotenda NA ANATAKA TUSAHAU YALIYOPITA. WANAJF naombeni ushauri JICHUKULIE KAMA ni wewe. NIFANYEJE