Eti ameniacha kisa kofi moja tu

Eti ameniacha kisa kofi moja tu

Sasa ulimuomba msamaha wa nini? Kwani alikuwa nyumbani anapika? Amelielezea vipi hilo? By the way hilo kofi unasema limekukosesha mke ilhali kuna uwezekano limekuokoa usiingue choo cha kike!!

We mwenyewe hujielewi kwanza....jirekebishe.
 
Mkuu, hapo angalia 50 zako tu.
Mazingira tu ya ugomvi wenu yanaonesha kuwa binti sio mwaminifu kwako.
1. Umemkuta bar na njemba kwenye simu akaongopa
2. Alipokuona live unexpectedly alichanganyikiwa.
3. Alikuambia uongo kuwa ni kaka yake, na kama ni kaka why ajikanganye location yake ya mda huo kama ana nia njema?
Mwisho kabisa anakueuzia kesi kuwa wewe ndio mkosaji ili next time akushike vizuri zaidi yaani kama mkirudiana ni lazima utakuwa kiganjani mwake tu.
My take:
Achana nae mapema while it is early, you still have chance ahead of you ( maana umesema uhusiano wenu una miezi 3 tu) so hadi hapo bado mizizi ya penzi haijaenda mbali saaana moyoni.
The cards are on your lap, take them or leave them
 
Kwanza unampiga mkeo? umemtolea mahari? mahusiano ya miezi mi3 unampiga yangekua miezi sita? au akitimiza mwaka na meno hana, Mwanamme anatakiwa awe muelewa ungemuuliza kwa hekma na upole ungejua yote lakini kwakipigo anajitambua huyo mwanamke ndio mana anaona naiwe basi, ivi mpaka leo kuna wanaume wanaopiga wanawake kweli?
Kaka kama mmeshindwana TABIA muache na huo mchezo kwanza amekufundisha nani au umeona wapi? huyo ni mtoto wawatu unampiga kofi na anakufia unafanyaje? tumia busara sana mara nyengine,sorry kama ntakua nimeongea sana.
Unamuuliza swali anajibu uongo atapigwa tu, hamna namna nyingine atapigwa tu na mimi nasema apige tu maana ni muongo.
 
Wewe usiwe mjinga huyo demu ni malaya kashakuona wewe ----- ..huyo aliyekuwa nae sio ndugu yake ...kama angekuwa ndugu asingekudanganya ...ukivyompiga ni sawasawa mpuuzi huyo achana nae kabisaaa
 
Ulitaka umpige makofo mangapi ndio akukimbie? Jmn jmn nani alikuambia mwanamke ni wa kupiga? They are delicate, they must be handled carefully, pampered n what mot. Hujamuoa unadiriki kumpiga hadharani!!!!!! Akiingia kwako si atakuwa dekio?? Pole sana. Hata km alikudanganya hilo kofi halifuti kosa lake. Sahau tafuta kwingine na urekebishe tabia zako
Kofi halifuti kosa ila linamkumbusha kuwa hatakiwi kufanya upuuzi!
 
Habari wandugu, natumaini mko poa.

Mimi nina mpenzi wangu tumekuwa nae kwenye mahusiano huu ni mwezi wa tatu,sio siri huyu binti nampenda sana, nimejitahidi kumhudumia kadri niwezavyo kwa mda mfupi nilikuwa nae, kwa sababu nina nia ya kumuoa, sasa juzi nilikuwa na rafiki yangu tupo maeneo ya Sinza tukapita kwenye bar moja hivi ghafla nikamuona mpenzi wangu nae yupo mle ndani ya bar anakunywa kinywaji wakiwa wamekaa na mwanaume mmi simjui, ndipo nikaamua kumpigia simu mpenzi wangu nakumuuliza yuko wapi.

Akapokea simu nakunijibu yupo nyumbani kwao anapika na wakati minamuona yupo na kijeba wanakunywa vinywaji huku wanacheka, sio siri nilipatwa na hasira ndipo nikaamua kumtuma rafiki yangu akamuite ili niongee, aliponiona alishangaa na aliponisogelea tu sikumsemesha neno lolote nikampiga kofi moja la nguvu rafiki yangu akanishika mikono na watu wakajaa kidogo, nikaamua kuondoka na yule binti akawa amekipingia.

Sasa zimepita siku mbili yule binti nimempigia simu akapokea akaniambia yule alikuwa kaka yake mtoto wa baba yake mdogo na pia ameniambia mimi na yeye basi amesema hawezi kuishi na mtu kama mmi tena, nimejaribu kumuomba msamaha lakini wapi amekataa katakata.

Naombeni msaada wa mawazo jamani nifanyeje? Eti kofi moja tu linikoseshe mke jamani.
mara paap umeachwa
 
yaan ww umemuonea huruma sna itakua ni mwanaume wa dar si bure mim namngoa meno matatu hapo hapo mbele ya huyo kijeba
 
Back
Top Bottom