Eti ameniacha kisa kofi moja tu


hili ndio tatizo lenu kwanza jiulize kwanini kapigwa kofi pili kwa nini adanganye tatu kwa nini astuke.unahisi barua ni kitu muhimu saaana hebu fikiria ndani ya miezi mitatu angepata ujauzito akatoswa ungekumbuka barua? samahani kama nimekuboa ila nawewe mshkaji jaribu kua imara samahani yanini wakati yeye ndio wakwanza kutenda kosa aanze yy kuomba radhi nawe umalize
 
Je waamini kuwa huyo rafiki yako ni mkweli? Hata kama utaoa jua imekula kwako.
 
Huyo dada hakupendi hata kidogo kwanza ilibidinyeye ndio akuombe msamaha kwa kukudanganya na kumkuta na kidume Bar. Kwa ufupinhuyo jamaa ameshakupiku na bado unadanganywa ni kaka yake unaamini, toka lini mtu akakwambia yuko home anapika kumbe yuko na kiduma halafu anazidi kukufanya zuzu kwa kukwambia ni kaka yake na wewe ulivyo unakubali

Achana nae kama akigundua kosa lake yeye ndie anatakiwa kuomba msamaha sio wewe kumpiga kofi sio kosa kubwa kihivyo
 
hakufai.... wanawake waaina iyo ni hatari,kosa lake alafu anakususia,tia gia gari ianze safari
 

Sijakata kama hakufanya kosa,lakini kumpiga sio kutatua kosa,anampiga ili iweje? haya keshampiga amepata nini?
Mwanamme kwenye kujitambua hafanyi mambo haya hasa kama anajua thamani ya Mwanamke kua ni Mama yake,mwanamke ni dada yake na mwanamke ni mpenzi wake au mkewe,fikiria anampiga anaanguka ana onekana mwili wake na sehemu zake za siri ivi unadhani wanaokuona unampiga mwanamke na kama wanajitambua watakuonaje? au angekua mzazi wako au Dada yako anapigwa na mwanamme wala hajamuoa ungejisikiaje au ungefanye? vyovyote itakavyo kua amekosea kumpiga,ange muacha aka songa mbele angepungua nini? samahani kama ntakua nimekukera..
 
ila naww acha mambo ya kizamani ungekuwa napistol alafu ukampiga risasi moja akafa ungesema ''nimeua kisa risasi moja tu''
 
Achana nae huyo pasua kichwa, Wanawake wanavumilia sana. Huyo kashindwa kukusamehe kwa Kofi moja. Kesho mpo ndani atashindwa kuvumlia akilala njaa. Achana nae.
 
demu kama demu haipaswi kukuumiza kichwa sana coz kama ulikuwa na malengo ya kumuoa unatakiwa ushukuru akikuonyesha mambo ya ajabu coz anakuepushia janga kama utamwoa na hakuna haja ya wewe kumpiga unaachana nae tu songa mbele pata mwingine mweke majaribioni
 

Wewe ukifanya kosa huwa unapigwa? Hakuna aliyemkamilifu na kumpiga mtu sio ndio unamrekebisha jaribu kutumia akili na si nguvu. Nguvu tuwaachie masokwe yasiyo na utashi na akili za kufikiri
 

Kupiga kofi ni kosa jaribu kutumia akili na si nguvu hivi unajua hilo kofi linaweza sababishia murder case so be careful kama unamkono wa kupiga. Jirani yangu hapa alipiga mke kofi akaangukia kichwa mke kafa na yeye anaozea jela kwa kosa la kijinga tu watt hawataki hata kumsikia baba yao maana wao hawajui mama yao aliuwawa na kofi moja wanajua baba yao alimuua mama yao. So be careful
 
Wako wengi sio wife matarial huyo tafuta mwengine kwanza muongo
 
kumbe anaishi SINZA!!!! Hapo ni sawa na kusubiria embe chini ya mti wa muarobaini, Sasa wewe mkikutana unamnunulia FANTA KIPAPLIPAPLI, Wenzako wakikaa nae, wanamuangushia Mizinga ya Wine, nyama choma juu na lodge ya ukweli.. JIPANGE
 
Hamna cha kaka wala nani, ukweli ni kua unaibiwa. Kama angekua kaka ake kwel angesema yupo na kaka
 
Mfyuu wanaume cjui mpoje mngekua mnapgwa na nyie ingekuaje
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…