Kwanza unampiga mkeo? umemtolea mahari? mahusiano ya miezi mi3 unampiga yangekua miezi sita? au akitimiza mwaka na meno hana, Mwanamme anatakiwa awe muelewa ungemuuliza kwa hekma na upole ungejua yote lakini kwakipigo anajitambua huyo mwanamke ndio mana anaona naiwe basi, ivi mpaka leo kuna wanaume wanaopiga wanawake kweli?
Kaka kama mmeshindwana TABIA muache na huo mchezo kwanza amekufundisha nani au umeona wapi? huyo ni mtoto wawatu unampiga kofi na anakufia unafanyaje? tumia busara sana mara nyengine,sorry kama ntakua nimeongea sana.
hili ndio tatizo lenu kwanza jiulize kwanini kapigwa kofi pili kwa nini adanganye tatu kwa nini astuke.unahisi barua ni kitu muhimu saaana hebu fikiria ndani ya miezi mitatu angepata ujauzito akatoswa ungekumbuka barua? samahani kama nimekuboa ila nawewe mshkaji jaribu kua imara samahani yanini wakati yeye ndio wakwanza kutenda kosa aanze yy kuomba radhi nawe umalize
hili ndio tatizo lenu kwanza jiulize kwanini kapigwa kofi pili kwa nini adanganye tatu kwa nini astuke.unahisi barua ni kitu muhimu saaana hebu fikiria ndani ya miezi mitatu angepata ujauzito akatoswa ungekumbuka barua? samahani kama nimekuboa ila nawewe mshkaji jaribu kua imara samahani yanini wakati yeye ndio wakwanza kutenda kosa aanze yy kuomba radhi nawe umalize
Huyo dada hakupendi hata kidogo kwanza ilibidinyeye ndio akuombe msamaha kwa kukudanganya na kumkuta na kidume Bar. Kwa ufupinhuyo jamaa ameshakupiku na bado unadanganywa ni kaka yake unaamini, toka lini mtu akakwambia yuko home anapika kumbe yuko na kiduma halafu anazidi kukufanya zuzu kwa kukwambia ni kaka yake na wewe ulivyo unakubali
Achana nae kama akigundua kosa lake yeye ndie anatakiwa kuomba msamaha sio wewe kumpiga kofi sio kosa kubwa kihivyo
Wako wengi sio wife matarial huyo tafuta mwengine kwanza muongo
acha ubweg.e wewe, unafikiri huyo ni kakayake?
kumbe anaishi SINZA!!!! Hapo ni sawa na kusubiria embe chini ya mti wa muarobaini, Sasa wewe mkikutana unamnunulia FANTA KIPAPLIPAPLI, Wenzako wakikaa nae, wanamuangushia Mizinga ya Wine, nyama choma juu na lodge ya ukweli.. JIPANGEHabari wandugu, natumaini mko poa.
Mimi nina mpenzi wangu tumekuwa nae kwenye mahusiano huu ni mwezi wa tatu,sio siri huyu binti nampenda sana, nimejitahidi kumhudumia kadri niwezavyo kwa mda mfupi nilikuwa nae, kwa sababu nina nia ya kumuoa, sasa juzi nilikuwa na rafiki yangu tupo maeneo ya Sinza tukapita kwenye bar moja hivi ghafla nikamuona mpenzi wangu nae yupo mle ndani ya bar anakunywa kinywaji wakiwa wamekaa na mwanaume mmi simjui, ndipo nikaamua kumpigia simu mpenzi wangu nakumuuliza yuko wapi.
Akapokea simu nakunijibu yupo nyumbani kwao anapika na wakati minamuona yupo na kijeba wanakunywa vinywaji huku wanacheka, sio siri nilipatwa na hasira ndipo nikaamua kumtuma rafiki yangu akamuite ili niongee, aliponiona alishangaa na aliponisogelea tu sikumsemesha neno lolote nikampiga kofi moja la nguvu rafiki yangu akanishika mikono na watu wakajaa kidogo, nikaamua kuondoka na yule binti akawa amekipingia.
Sasa zimepita siku mbili yule binti nimempigia simu akapokea akaniambia yule alikuwa kaka yake mtoto wa baba yake mdogo na pia ameniambia mimi na yeye basi amesema hawezi kuishi na mtu kama mmi tena, nimejaribu kumuomba msamaha lakini wapi amekataa katakata.
Naombeni msaada wa mawazo jamani nifanyeje? Eti kofi moja tu linikoseshe mke jamani.