Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,499
- 113,608
Wanabodi,
"Wema usizidi uwezo!" ila pia too much of anything is harmful, hivyo "wema nao ukizidi, unaweza kukuponza!".
Bwana Mungu alitupa amri kuu "mpendane"!, katika utekelezaji wa amri hii, kuna baadhi ya wenzetu waliojaaliwa uwezo mkubwa wa upendo, hadi kufikia level ya kuwa na "upendo wa mshumaa", kumulikia wengine huku kwake kunateketea!, hivi ndivyo ulivyo wema wa Mzee Wetu huyu, Mzee James Rugemalila, (Mzee JR), ule wema wake sasa unataka kumponza!. Laiti baada ya kujivutia ule mpunga wake, angelijikalia kimya na kujifanya kama ana roho mbaya ya uchoyo, labda yote haya yasingalitokea, you never know!. Tumuombee ulinzi wa Roho Mtakatifu, amlinde kwa nguvu na uwezo wake ili yasimkute yale yaliyoimbwa na mwanamuziki, Patrick Balisidya kuwa "Wema Hawana Maisha!", au Hemedi Maneti kuhusu "Wanaopendwa na Wengi!".
Nimesikia kwa juu juu, kuwa utekelezaji wa yale Maazimio batili ya Bunge kuhusu Escrow, unatarajiwa kuanza, hivyo ni pamoja na lile azimio la uonevu la kukamatwa na kutiwa nguvuni kwa Singa Singa wa PAP na Mzee wetu, mwema, Mzee James Rugemalila, mwenye roho ya upendo wa ajabu, na moyo wa huruma iliyopitiliza, kuwa na yeye anatakiwa kukamatwa!. Singa Singa atakuwa ameishajitimkia zake ughaibuni siku nyingi kama walivyotimka kina Vithlani, ila namshauri Mzee wetu James Rugemalila, yeye asitimkie popote, kwa sababu hajafanya kosa lolote na tunamuombea ulinzi kwa Mungu Baba kupitia Roho Mtakatifu wake, na sala zetu, amlinde, atampigania na atashinda!.
Naomba kwa hapa tuwe wakweli, huyu Mzee JR akamatwe kwa kosa gani?. Aliyechota fedha za escrow ni kalasinga wa PAP, fedha za Escrow zimelipwa PAP, yeye amefanya biashara halali kabisa ya kuuza hisa zake halali ndani ya VIP kwa kumuuzia PAP, na amelipwa na PAP malipo halali kwa hisa zake, na baada ya kupokea malipo, amelipa kodi zote stahiki na halali za serikali, pesa zilizobaki ndizo amezifanyia wema kuzigawa kama sadaka au asante kwa wale aliowachagua, sasa kosa lake ni lipi?!, na waliopokea sadaka ya wema ule wana kosa gani?!. Hakuna kosa lolote kwa mtu yoyote kugawa fedha zake mwenyewe kwa yeyote, na hakuna kosa lolote kwa mtu kupokea fedha zozote halali toka kwa yeyote.
Kwa mliofuatilia kisa kizima cha IPTL tangu kuingia kwake, mtakubaliana na mimi kuwa Mzee James Rugemalia amefanya sana 'wema', haiwezekani, watu wale wale waliofanyiwa 'wema' ule, leo ndio waje wamgeuke na kumtia misukosuko!. Huu utakuwa ni utovu wa fadhila unless waje wengine wasiojua wema wake!.
Naomba kukiri, nimekuwa inspired kuandika haya, kufuatia post ya mwana jf huyu.
Kama ni kweli, kamtumia e-mail Mhe rais, ni nyinyi tuu msiojua kuwa hiyo sio e-mail ya maelekezo, bali ni kumkumbusha tuu, mhe. Rais akumbuke fadhila!. Na mimi namuunga mkono JR kwa asilimia 100%, ombi langu ni moja tuu, nawaomba sana viongozi wetu, wasiwe watovu wa fadhila!, wawe watu wa shukrani, wakumbuke walikotoka na jinsi walivyotendewa 'wema' na Mzee wetu huyu James Rugemalila!, hivyo wanapaswa kulipa fadhila!.
Mimi nakikumbuka kukisoma kisa kimoja cha 'wema' fulani Mzee wetu huyu, alioutandaza kipindi cha kukaribia sikukuu ya Krismasi fulani!, aliwazungukia "wanene" wote wanaohusika na usajili wa VIP na kuwatendea 'wema' stahiki. Katika waliotendewa wema huo, kuna jitu fulani moja la ajabu sana likiitwa li Patrick Rutabanzibwa, lenyewe lilikuwa ni jitu bold, kiburi, jeuri na roho mbaya ya ajabu, hata kuthubutu, kuukataa 'wema' wa James Rugemalila, kwa vile 'wema' wenyewe uliachwa nyumba hadi nyumba kabla ya sikukuu, wengine wote waliukubali wema ule na wakaupokea na kusherehea krismasi njema! kwa raha mustarehe kwa 'wema' wa JR!. Hiri rijamaa, li Patrick Rutabanzibwa na jiroho lake baya, lilikuwa bold, kiburi na jeuri ya ajabu ya kuthubutu kuukataa 'wema' wa JR ulioachwa nyumbani kwake kabla ya Krismasi, kisa hawezi kupokea 'wema' wa mashaka bila kujua 'wema' huo ni wa nini!. hivyo baada tuu ya sikukuu, ya Krismass li Patrick Rutabanzibwa, liliubeba 'wema' ule vile vile ulivyo, likaurudisha kwa JR!.
JR akaripoti kwa mabosi wake ambao wao waliopokea 'wema' wake, hao mabosi wakalikomesha hilo lijamaa kwa kulikomoa, na kuliadhibu kwa kuliweka pembeni!, IPTL ikapita!.
Sasa hii IPTL ilipita pitaje na ni kina nani waliipitisha, na kwa 'wema' upi wa mradi huu!, wote tunaojua, tunajua!, na wahusika wanajulikana kwa majina na 'wema' wote waliotendewa na huyu Mzee wetu wa wema, James Rugemalila!, unajulikana!, iweje leo wakose shukrani?!, wakose fadhila kutaka kumuadhibu?!. Not this time labda wakija wengine!.
Haya majina yanayopigiwa kelele humu kuwa wamelipwa, ni majina ya 'wema' kiduchu tuu wa kale kajibenki kadogo tuu, ka Mkombozi ambako kazi yake ni kuwakomboa watu!, laiti watu wangeliyaona majina ya recipients wa sadaka za wema kubwa wa PAP toka libenki likubwa la Stanbic!, au majina ya 'wema' mkubwa wa JR kutoka kwenye ile account yake ya nchini Holland, kuwa transifia "wanene" kupitia account zao zilizoko Credit Suisse!, watu humu wangebaki midomo wazi!.
Haiwezekani mtu ufanye 'wema' huo wote!, alafu leo wema wako uje kukuponza usumbuliwe na vijitu vidogo vidogo visivyojua kitu!. Enyi wote mliofanyiwa wema na JR kumbukeni fadhila wajameni!, huwezi kutendewa mema ukalipa kwa maovu, hata Mungu hapendi!, mtalaaniwa!.
Kama Mzee wetu huyu, JR, hata baada ya wema wote huo, na bado anasumbuliwa!, mimi ninachohofia sasa, ni uwezekano wa kumyamazisha jumla!.
Majina yote yaliyo leak, ni yale majina ya tuji 'sadaka' tudogo twa "Mkombozi tuu!", no names kwenye ile miji bingo mikubwa minene ya 'mijisadaka' mikubwa ya PAP iliyochotea cash kutoka Stanbic bank na kubebwa kwe magunia ya sandarusi, na no names za big fishes wa 'mijisadaka' mikubwa ya account yake ya Holland!.
Threat kubwa kwa JR, sasa ni kutoka kwa hao hao "big fish" recipients, aliowatendea 'wema' mkubwa kwa mijisadaka mikubwa mikubwa, ambao kama ni kweli JR atatiwa misuko suko, watakosa amani kwa kuhofia asije kuwa harassed too much, akakasirika na hatimaye mwisho akaamua kufungua mdomo!.
Ili kujihakikishia usalama wao na majina yao kutotajwa, wanaweza kabisa kuamua "kumfunga mdomo" jumla!, kwa kuitumia ile kanuni ya ikibidi punda afe, na afe tuu ili mradi mzigo ufike!, kama usalama wao ni ile "silence yake", silence hiyo ikiwa threatened, kuliko wao kujulikana, bora kumremainisha silent!.
Watanzania wote wenye mapenzi mema na uhai wa binadamu, na wenye kupenda kuujua ukweli, majina ya Mkombozi ni cha mtoto!, tuungane kwa sala na maombi, kumuombea uzima Mzee wetu James Rugemalila, tena sii kwa ulinzi tuu wa binadamu tuu, maana hatuwezi, hila za mwovu shetani ni nyingi, tuombe na tumfungie novena apate ulinzi wa nguvu na uweza wa Roho Mtakatifu, awe salama, ili siku ya siku itafika ataweza kumulikiwa na ule mwanga mkubwa kama wa Sauli kwenye ile njia ya kwenda Jeriko, mwanga ule ukamfungulia, Sauli akaona mwanga, akanena, akabadilika na kuwa Paulo. Vivyo hivyo tumuombe uzima Mzee wetu James Rugemalila, ili ifike siku na yeye aone mwanga!, atanena!, ndipo mtaujua ukweli!.
Kitakachokuja kumtokea James Rugemalila ni kile kile kilichowatokea wana wa Israel utumwani Misri. Aliyewaleta Israel Misri ni Yusufu kwa wema alioutenda wa kutabiri ile ndoto ya Farao. Hivyo Waisrael wakahamia Misri kwa shangwe. Baada ya muda akatokea Farao mwingine ambaye hakuujua wema wa Yusufu, hivyo akawageuza Wa Israel kuwa ni watumwa!.
Hivyo tuendelee kuomba na hapa nchini kwetu kusije tokea utawala mwingine ambao haujui wema wa James Rugemalila, hivyo msije kushangaa siku ya siku mambo yakabadilika huu wema Rugemalila alioutenda ukaja kumponza na kumtokea puani!.
Mimi ni muumini wa "ukweli usemwe!", "the truth must be told no matter who, what, where, when, and how (5W+H) hivyo kuna siku itafika na ukweli utasemwa!.
Eh Mungu, kupitia Roho Mtakatifu wako, na jeshi lako lote la Malaika wa Mbinguni, mlinde Mzee Wetu, James Rugemalila na majaribu yote yaliyo mbele yake, hadi afike ile siku uliompangia ya ukweli kujulikana kwanza, na ndipo baadaye aje atimize mapenzi yako kwa kadri ulivyompangia wewe!.
Amen.
Paskali.
"Wema usizidi uwezo!" ila pia too much of anything is harmful, hivyo "wema nao ukizidi, unaweza kukuponza!".
Bwana Mungu alitupa amri kuu "mpendane"!, katika utekelezaji wa amri hii, kuna baadhi ya wenzetu waliojaaliwa uwezo mkubwa wa upendo, hadi kufikia level ya kuwa na "upendo wa mshumaa", kumulikia wengine huku kwake kunateketea!, hivi ndivyo ulivyo wema wa Mzee Wetu huyu, Mzee James Rugemalila, (Mzee JR), ule wema wake sasa unataka kumponza!. Laiti baada ya kujivutia ule mpunga wake, angelijikalia kimya na kujifanya kama ana roho mbaya ya uchoyo, labda yote haya yasingalitokea, you never know!. Tumuombee ulinzi wa Roho Mtakatifu, amlinde kwa nguvu na uwezo wake ili yasimkute yale yaliyoimbwa na mwanamuziki, Patrick Balisidya kuwa "Wema Hawana Maisha!", au Hemedi Maneti kuhusu "Wanaopendwa na Wengi!".
Nimesikia kwa juu juu, kuwa utekelezaji wa yale Maazimio batili ya Bunge kuhusu Escrow, unatarajiwa kuanza, hivyo ni pamoja na lile azimio la uonevu la kukamatwa na kutiwa nguvuni kwa Singa Singa wa PAP na Mzee wetu, mwema, Mzee James Rugemalila, mwenye roho ya upendo wa ajabu, na moyo wa huruma iliyopitiliza, kuwa na yeye anatakiwa kukamatwa!. Singa Singa atakuwa ameishajitimkia zake ughaibuni siku nyingi kama walivyotimka kina Vithlani, ila namshauri Mzee wetu James Rugemalila, yeye asitimkie popote, kwa sababu hajafanya kosa lolote na tunamuombea ulinzi kwa Mungu Baba kupitia Roho Mtakatifu wake, na sala zetu, amlinde, atampigania na atashinda!.
Naomba kwa hapa tuwe wakweli, huyu Mzee JR akamatwe kwa kosa gani?. Aliyechota fedha za escrow ni kalasinga wa PAP, fedha za Escrow zimelipwa PAP, yeye amefanya biashara halali kabisa ya kuuza hisa zake halali ndani ya VIP kwa kumuuzia PAP, na amelipwa na PAP malipo halali kwa hisa zake, na baada ya kupokea malipo, amelipa kodi zote stahiki na halali za serikali, pesa zilizobaki ndizo amezifanyia wema kuzigawa kama sadaka au asante kwa wale aliowachagua, sasa kosa lake ni lipi?!, na waliopokea sadaka ya wema ule wana kosa gani?!. Hakuna kosa lolote kwa mtu yoyote kugawa fedha zake mwenyewe kwa yeyote, na hakuna kosa lolote kwa mtu kupokea fedha zozote halali toka kwa yeyote.
Kwa mliofuatilia kisa kizima cha IPTL tangu kuingia kwake, mtakubaliana na mimi kuwa Mzee James Rugemalia amefanya sana 'wema', haiwezekani, watu wale wale waliofanyiwa 'wema' ule, leo ndio waje wamgeuke na kumtia misukosuko!. Huu utakuwa ni utovu wa fadhila unless waje wengine wasiojua wema wake!.
Naomba kukiri, nimekuwa inspired kuandika haya, kufuatia post ya mwana jf huyu.
Isitoshe, kamtumia mh rais emails zenye maelekezo ya hatua za kuchukuliwa na serikali. He owns this impotent corrupt government
Kama ni kweli, kamtumia e-mail Mhe rais, ni nyinyi tuu msiojua kuwa hiyo sio e-mail ya maelekezo, bali ni kumkumbusha tuu, mhe. Rais akumbuke fadhila!. Na mimi namuunga mkono JR kwa asilimia 100%, ombi langu ni moja tuu, nawaomba sana viongozi wetu, wasiwe watovu wa fadhila!, wawe watu wa shukrani, wakumbuke walikotoka na jinsi walivyotendewa 'wema' na Mzee wetu huyu James Rugemalila!, hivyo wanapaswa kulipa fadhila!.
Mimi nakikumbuka kukisoma kisa kimoja cha 'wema' fulani Mzee wetu huyu, alioutandaza kipindi cha kukaribia sikukuu ya Krismasi fulani!, aliwazungukia "wanene" wote wanaohusika na usajili wa VIP na kuwatendea 'wema' stahiki. Katika waliotendewa wema huo, kuna jitu fulani moja la ajabu sana likiitwa li Patrick Rutabanzibwa, lenyewe lilikuwa ni jitu bold, kiburi, jeuri na roho mbaya ya ajabu, hata kuthubutu, kuukataa 'wema' wa James Rugemalila, kwa vile 'wema' wenyewe uliachwa nyumba hadi nyumba kabla ya sikukuu, wengine wote waliukubali wema ule na wakaupokea na kusherehea krismasi njema! kwa raha mustarehe kwa 'wema' wa JR!. Hiri rijamaa, li Patrick Rutabanzibwa na jiroho lake baya, lilikuwa bold, kiburi na jeuri ya ajabu ya kuthubutu kuukataa 'wema' wa JR ulioachwa nyumbani kwake kabla ya Krismasi, kisa hawezi kupokea 'wema' wa mashaka bila kujua 'wema' huo ni wa nini!. hivyo baada tuu ya sikukuu, ya Krismass li Patrick Rutabanzibwa, liliubeba 'wema' ule vile vile ulivyo, likaurudisha kwa JR!.
JR akaripoti kwa mabosi wake ambao wao waliopokea 'wema' wake, hao mabosi wakalikomesha hilo lijamaa kwa kulikomoa, na kuliadhibu kwa kuliweka pembeni!, IPTL ikapita!.
Sasa hii IPTL ilipita pitaje na ni kina nani waliipitisha, na kwa 'wema' upi wa mradi huu!, wote tunaojua, tunajua!, na wahusika wanajulikana kwa majina na 'wema' wote waliotendewa na huyu Mzee wetu wa wema, James Rugemalila!, unajulikana!, iweje leo wakose shukrani?!, wakose fadhila kutaka kumuadhibu?!. Not this time labda wakija wengine!.
Haya majina yanayopigiwa kelele humu kuwa wamelipwa, ni majina ya 'wema' kiduchu tuu wa kale kajibenki kadogo tuu, ka Mkombozi ambako kazi yake ni kuwakomboa watu!, laiti watu wangeliyaona majina ya recipients wa sadaka za wema kubwa wa PAP toka libenki likubwa la Stanbic!, au majina ya 'wema' mkubwa wa JR kutoka kwenye ile account yake ya nchini Holland, kuwa transifia "wanene" kupitia account zao zilizoko Credit Suisse!, watu humu wangebaki midomo wazi!.
Haiwezekani mtu ufanye 'wema' huo wote!, alafu leo wema wako uje kukuponza usumbuliwe na vijitu vidogo vidogo visivyojua kitu!. Enyi wote mliofanyiwa wema na JR kumbukeni fadhila wajameni!, huwezi kutendewa mema ukalipa kwa maovu, hata Mungu hapendi!, mtalaaniwa!.
Kama Mzee wetu huyu, JR, hata baada ya wema wote huo, na bado anasumbuliwa!, mimi ninachohofia sasa, ni uwezekano wa kumyamazisha jumla!.
Majina yote yaliyo leak, ni yale majina ya tuji 'sadaka' tudogo twa "Mkombozi tuu!", no names kwenye ile miji bingo mikubwa minene ya 'mijisadaka' mikubwa ya PAP iliyochotea cash kutoka Stanbic bank na kubebwa kwe magunia ya sandarusi, na no names za big fishes wa 'mijisadaka' mikubwa ya account yake ya Holland!.
Threat kubwa kwa JR, sasa ni kutoka kwa hao hao "big fish" recipients, aliowatendea 'wema' mkubwa kwa mijisadaka mikubwa mikubwa, ambao kama ni kweli JR atatiwa misuko suko, watakosa amani kwa kuhofia asije kuwa harassed too much, akakasirika na hatimaye mwisho akaamua kufungua mdomo!.
Ili kujihakikishia usalama wao na majina yao kutotajwa, wanaweza kabisa kuamua "kumfunga mdomo" jumla!, kwa kuitumia ile kanuni ya ikibidi punda afe, na afe tuu ili mradi mzigo ufike!, kama usalama wao ni ile "silence yake", silence hiyo ikiwa threatened, kuliko wao kujulikana, bora kumremainisha silent!.
Watanzania wote wenye mapenzi mema na uhai wa binadamu, na wenye kupenda kuujua ukweli, majina ya Mkombozi ni cha mtoto!, tuungane kwa sala na maombi, kumuombea uzima Mzee wetu James Rugemalila, tena sii kwa ulinzi tuu wa binadamu tuu, maana hatuwezi, hila za mwovu shetani ni nyingi, tuombe na tumfungie novena apate ulinzi wa nguvu na uweza wa Roho Mtakatifu, awe salama, ili siku ya siku itafika ataweza kumulikiwa na ule mwanga mkubwa kama wa Sauli kwenye ile njia ya kwenda Jeriko, mwanga ule ukamfungulia, Sauli akaona mwanga, akanena, akabadilika na kuwa Paulo. Vivyo hivyo tumuombe uzima Mzee wetu James Rugemalila, ili ifike siku na yeye aone mwanga!, atanena!, ndipo mtaujua ukweli!.
Kitakachokuja kumtokea James Rugemalila ni kile kile kilichowatokea wana wa Israel utumwani Misri. Aliyewaleta Israel Misri ni Yusufu kwa wema alioutenda wa kutabiri ile ndoto ya Farao. Hivyo Waisrael wakahamia Misri kwa shangwe. Baada ya muda akatokea Farao mwingine ambaye hakuujua wema wa Yusufu, hivyo akawageuza Wa Israel kuwa ni watumwa!.
Hivyo tuendelee kuomba na hapa nchini kwetu kusije tokea utawala mwingine ambao haujui wema wa James Rugemalila, hivyo msije kushangaa siku ya siku mambo yakabadilika huu wema Rugemalila alioutenda ukaja kumponza na kumtokea puani!.
Mimi ni muumini wa "ukweli usemwe!", "the truth must be told no matter who, what, where, when, and how (5W+H) hivyo kuna siku itafika na ukweli utasemwa!.
Eh Mungu, kupitia Roho Mtakatifu wako, na jeshi lako lote la Malaika wa Mbinguni, mlinde Mzee Wetu, James Rugemalila na majaribu yote yaliyo mbele yake, hadi afike ile siku uliompangia ya ukweli kujulikana kwanza, na ndipo baadaye aje atimize mapenzi yako kwa kadri ulivyompangia wewe!.
Amen.
Paskali.