Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 16,559
- 41,078
Hivi karibuni, huko Canada, Spika wa Bunge alilazimika kujiuzulu baada ya kulaumiwa na watu mbalimbali kwa kosa la kumkaribisha mzee mmoja (jina silikumbuki) ambaye alikuwa miongoni mwa wafuasi wa chama cha manazi cha Hitler.
Huyu mzee, hakuna taarifa yoyote au ushahidi kuwa akiwa kwenye chama cha manazi cha Adolf Hitler, kama aliwahi kuua au kutesa au kuteka mtu yeyote, lakini ile kuwepo tu kwenye chama kilichoendesha mauaji, imetosha kwa yeye kuwa mhalifu, kwa kiwango cha kutostahili heshima mahali popote kwenye taasisi za umma na Serikali. Spika wa bunge alikiri kufanya kosa, na kisha akajiuzulu.
Hapa kwetu tuna mtu ambaye kuna ushahidi wote kuwa ni mwovu mkubwa, kuanzia kuwa jambazi la kutumia silaha (alioneshwa na CCTV camera akiwa anavamia kituo cha Clouds), jambazi la kutishia watu kwa silaha (alionekana akitoa maelekezo kwa watu waliomtishia Nape kwa pisto) , mtesaji, muuaji (US wakasema asikanyage nchini mwao kwa sababu anawanyima watu haki ya kuishi), ana tuhuma za kusimamia zoezi la kutaka kumwua Tundu Lisu, na pia kusimamia zoezi la kumpoteza Ben Sanane, na kumteka mwanamuziki Roma. Maajabu makubwa ni kuwa CCM wamemzawadia cheo kikubwa. Bila shaka ni namna ya kuutambua utumishi wake uliotukuka kwenye maovu aliyokuwa akiyafanya na kuyasimamia.
Nadhani ujumbe kwa wananchi upo wazi, yale aliyokuwa akiyafanya yalikuwa ya CCM. Yale ndiyo mambo ambayo CCM inayapenda na kuyasimamia, na hivyo wamemteua ili ayasimamie vizuri.
Watanzania walio wema, jitafakarini, msije siku moja mkawa kama yule aliyekaribishwa bungeni Canada, na baadaye akasababisha hata spika ajiuzulu kwa sababu ya kumkaribisha mtu mwovu kwenye taasisi ya umma.
Watu wema tujitenge na waovu, tujitenge pia na vyama vinavyofurahia na kusimamia uovu. Basi, na laana ya Mungu ikakae na hawa waovu na wazao wao hata kizazi na kizazi
Mungu wa rehema azijalie pumziko jema Roho ya Azory, Ben, Kanguye na wengine wote walionyimwa haki ya kuishi na yule mwovu. Wote walioteswa na kutekwa wajaliwe nguvu mpya, na ushindi uwe juu yao.
Huyu mzee, hakuna taarifa yoyote au ushahidi kuwa akiwa kwenye chama cha manazi cha Adolf Hitler, kama aliwahi kuua au kutesa au kuteka mtu yeyote, lakini ile kuwepo tu kwenye chama kilichoendesha mauaji, imetosha kwa yeye kuwa mhalifu, kwa kiwango cha kutostahili heshima mahali popote kwenye taasisi za umma na Serikali. Spika wa bunge alikiri kufanya kosa, na kisha akajiuzulu.
Hapa kwetu tuna mtu ambaye kuna ushahidi wote kuwa ni mwovu mkubwa, kuanzia kuwa jambazi la kutumia silaha (alioneshwa na CCTV camera akiwa anavamia kituo cha Clouds), jambazi la kutishia watu kwa silaha (alionekana akitoa maelekezo kwa watu waliomtishia Nape kwa pisto) , mtesaji, muuaji (US wakasema asikanyage nchini mwao kwa sababu anawanyima watu haki ya kuishi), ana tuhuma za kusimamia zoezi la kutaka kumwua Tundu Lisu, na pia kusimamia zoezi la kumpoteza Ben Sanane, na kumteka mwanamuziki Roma. Maajabu makubwa ni kuwa CCM wamemzawadia cheo kikubwa. Bila shaka ni namna ya kuutambua utumishi wake uliotukuka kwenye maovu aliyokuwa akiyafanya na kuyasimamia.
Nadhani ujumbe kwa wananchi upo wazi, yale aliyokuwa akiyafanya yalikuwa ya CCM. Yale ndiyo mambo ambayo CCM inayapenda na kuyasimamia, na hivyo wamemteua ili ayasimamie vizuri.
Watanzania walio wema, jitafakarini, msije siku moja mkawa kama yule aliyekaribishwa bungeni Canada, na baadaye akasababisha hata spika ajiuzulu kwa sababu ya kumkaribisha mtu mwovu kwenye taasisi ya umma.
Watu wema tujitenge na waovu, tujitenge pia na vyama vinavyofurahia na kusimamia uovu. Basi, na laana ya Mungu ikakae na hawa waovu na wazao wao hata kizazi na kizazi
Mungu wa rehema azijalie pumziko jema Roho ya Azory, Ben, Kanguye na wengine wote walionyimwa haki ya kuishi na yule mwovu. Wote walioteswa na kutekwa wajaliwe nguvu mpya, na ushindi uwe juu yao.