ESCROW scandal: Pinda apata watetezi

Huyu jamaa huwa anakurupuka ktk kauli zake bungeni na hizo ndiyo kitanzi chake, mara pesa za ESCROW siyo za umma, mara mihimili isiingiliane yaani ilimradi ripoti isisomwe,huyu ni kama chura tu hasafishiki.
 

Sina hakika kama uko sahihi kwenye red bold. Kama Pinda ndiye alitoa maagizo ya uchunguzi kufanyika, kwa nini matokeo ya uchunguzi yapelekwe bungeni?? Kwa kumbukumbu zangu, bunge liliamuru uchunguzi huo ufanyike, na ndiyo maana hata kale ka-memo kutoka mahakamani kaligonga ukuta pale Idodomya.

mkuu, nakumbuka MALKIA WA NYUKI ndiye aliyeagiza iundwe kamati ya zitto kwa ajili ya kuchunguza skandali hii. hata hivyo, matarajio yake yalikuwa kwamba kamati itamlinda badala yake wamemkaanga sawia!
 
Hata wewe unakuja na hoja marehemu hapo hakuna kupanga ngoja ukweli uchukue mkondo wake....Mzee Pinda yuko vizuri....ni ukweli usiopingika kuwa Pinda ni kati ya PMs waadilifu na waelewa ukimtoa Mzee wetu late Moringe S....tusubili...

huyo pinda wako amelifanyia nini taifa hili tangu awe waziri mkuu? njaa zitakuua!
 
Kweli hata mimi namtetea kwa sababu yeye alishasema ni mtoto wa mkulima lakini mkampa ofisi.
Mlitegemea nini?
 
mi sijatumwa na yeyote lakini kiukweli kutoka moyoni pindahana hatia,kuagiza tu uchunguzi ufanyike ni kutekeleza wajibu wake.
 
Huyu jamaa is so weak bdo tu anataka Kuwa Rais?for that matter bora ya Lowassa kuliko PM ingawa wote wezi

ni bora FISADI Lowasa awe rais wa nchi kuliko Pinda--mtu dhaifu kuliko wote nchi hii.
 
Doesn't help. Huyu aondoke tu. Hii ni laana aliyoipata baada ya kuamrisha raia wapigwe bila kufuata sheria. Sasa anapigwa yeye. Na sisi tunasema apigwe tu maana sasa tumechoka
 
Watu kama Ole Sendeka wanajifanya hawajui kuwajibika maana yake ni nini. Pinda must go.
 
Kuna taarifa kwamba Pinder amewapanga wabunge kadhaa (majina kapuni) wamtetee bungeni leo ili asiende na maji. Kwa kufanikisha utetezi wao wanadai kwamba Pinder hajahusika yeye binafsi katika ufisadi huu bali ni watendaji wa chini yake ndio wanapaswa kuchukuliwa hatua.

Kete ya pili wanayotumia 'watetezi' hawa ni kwamba ikiwa Pinder alihusika kwenye ufisadi huu basi asingeagiza uchunguzi ufanyike. So the guy is clean and innocent.

Aidha, kuna timu kubwa imetumwa kumtetea Pinder kwenye social media, hasa JF, kwa lengo la kuupotosha umma na kuwafanya wananchi wasadiki kwamba Pinder anaonewa bure.

Kisingizio kingine kitakachotumiwa kumsafisha ni uwepo wa makundi ya urais, 2015 yanayochafuana.

Anyway, ngoja tusubiri tuone hao vibaraka wake wamejipangaje kumtetea kwa kuwa naona kama wanatumia hoja mfu kumsafisha mtu ambaye amechafuka kiasi cha kutosafishika tena. Mbivu na mbichi tutazipata leo bungeni wakati utetezi wa serikali (utakaotolewa na Pinder mwenyewe) utakaporindima.

Nawasilisha
:israel:

Tupo source mkuu,isije zikawa ni hisia zako na walio katika malango yako
 
kwa jinsi skandali hii ilivyokaa, pinda ajiudhuru ama asijiudhuru, tayari serikali na chama chake imechafuka kwa kiasi cha kutosha.
 
Hii ingekuwa Rwanda wallahi ujinga huu usingetokea na hawa mafisadi wangeipata fresh...
Tanzania sio nchi ya kuwa masikini kiasi hiki. Tunakosa uongozi bora.
 
Kuna njama kati ya spika makinda na serikali, wanataka kuchelewesha muda, ili kesho wahairishe mjadala! Kama taifa tumekwama, bunge linatumika kutetea mafisadi!
 
Back
Top Bottom