Erolink na nbc kuna nini????

Erolink na nbc kuna nini????

adebisi

Senior Member
Joined
Jul 31, 2012
Posts
100
Reaction score
111
Wananjamvi kuna issue imekuwa ikinisumbua muda mrefu, nina mdogo wangu alimaliza chuo kikuu 2011,katika harakati za kutafuta ajira akafanikiwa kutafutiwa kazi na hawa jama EROLINK na akawa attached NBC kama karani wa bank kwa makubaliano baada ya miezi sita atakuwa full employed na NBC. Cha ajabu sasa ni mwaka unaisha hakuna cha ajira, anabaki kusainishwa vimkataba vya miezi mitatu mitatu..

Swali la kujiuliza hivi kweli hizi bank zinaruhusu kuajiri temporary staff for more than a year.??na kwa habari za chinichini inasemakana 70% ya staff wa NBC ni temporary staffs as outsourced by EROLINK..kwa kufanya hivyo kunawanyima hawa wafanyakazi haki zao nyingi za msingi kama vile Bima ya afya, uniform za kazi,staff loans..n.k..

My take sekta ya Bank ni very sensitive, huwezi kuajiri temporary staff for more than a year na ukampa full access ya kila kitu ndani ya Bank. Tunapoelekea kunahatarisha usalama wa fedha zetu coz matukio ya wizi ndani ya bank yanaweza kuongezeka coz hawa temporary staffs they are lowly paid automatically watakuwa na tamaa..vile vile service watakayokuwa wanatoa tofauti na yule mtu ambae yupo parmanently employed.. Ningependa kutoa ombi kwa BOT walichunguze hili as well as Wizara ya Kazi kabla mambo hayajakuwa mabaya..
 
Ndo maana wizi haushi kwenye mabenki na bado hawajifunzi. Aibu tupu.
 
hao erolink ni wapigaji sana hawapo hapo tu wako pia voda kitengo cha customercare wanatumikisha vijana na kuwalipa ujira mdogo sana ukilinganisha na kazi wanazofanya!kiburi chao kikubwa ni tatizo la ajira hivyo imekuwa kama wamewekezza kwa vijana wa kitanzania wanaotafuta ajira na kugeuza kuwa sehemu yao ya kujipatia pesa kwa kuwanyonya.hii serikali sijui iko wapi
 
Huyo mdogo wako ni sawa na mdogo wangu,yeye wamemweka headquaters lakini hali yake ni mbaya sana.
Ni kweli BOT waliangalie hili suala.
 
HATARI zaidi wamewapa access ya kila Kitu wakitaka kuwapiga ni very simple..BOT IPO , wizara ya kazi IPO..sijui wanafanya nini?? Mbaya zaidi hao EROLINK hawawatreat fairly hao wafanyakazi..wanawafanya kama vibarua wao wakati wanawaingizia fedha..wanatumia unyonge wao wa kutokuwa na ajira kuwanyanyasa...!

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Yeah..hata xim kwenye kitengo cha sales wapo hao watu...hata sijui nisemeje..ila kama mtu una moyo mgumu,unapiga chini kazi!!!hakuna utakachopata zaidi ya stress,kujidharau na kudharau elimu yako!!!!
 
Sheria ya kazi nafikiri mtu akikaa zaidi ya miezi sita(6) inabidi apewe permanent contract
sasa sijui mtu anawezaje kukaa kipindi chote hicho bila kupewa permanent.
Kwanini serikali yetu inashindwa kuintervene kampuni nyonyaji kama hizi,watu wamelala au na wao wanakula humo
Narudi kwa nbc,nafikiri umauti unaikaribia hii bank inawezekanaje kuwa staff zaidi ya aina 2,permanent staff,temporary
na outsourced,kweli kuna baadhi ya vitu vinafanyika only in tz.
 
Nimefikisha malalamiko yako kwa wahusika na wanachunguza kujua ukweli.
 
kutokana na HABARI za kiintelejensia zinasema mkuu wa operation wa NBC Maharage Chande ndio deal yake hii ..na hii idea alitoka nayo Vodacom (kwenye ajira yake kabla hajahamia NBC) akishirikiana na Mkuu wa Bank hiyo aliejiuzulu walifanikiwa kuimplement uozo huu wakitumia kama source ya income yao..nafikiri wakati umefika kuwaondoa watu wasio na misingi ya uongozi bora..la sivyo NBC IPO hatarini kufilisika..kila mtu anataka achote aondoke..Mafuru kafanya yake kasepa ...tusubirie....

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Hawa EROLINK niliwahi kuwatolea nje, wakabaki wakinishangaa nakuniambia sikuwa na haja ya kazi.

Kusema kweli mshahara ulikuwa ndogo ukilinganisha na kazi yenyewe, nikaona bora niingie mtaani niendelee na ujasilamali kuliko mshahara uchwala.
 
Erolink to the best of my knowledge are contracted for outsourcing staff-as required by an institution! Examples as sales and marketing of products, services etc etc. The somehow provides a loophole since the 'recruits' may continue at the discretion of Erolink and their contract with the respective institution.
 
Inasemekana ni ya Mkubwa fulani hivi ndio maana wana nyodo ...Hawa dawa yao hao erolink staffs wajiorganise wastrike against them ...

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Inasemekana ni ya Mkubwa fulani hivi ndio maana wana nyodo ...Hawa dawa yao hao erolink staffs wajiorganise wastrike against them ...

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums

Wazo lako linaweza kusaidia, lakini kwa watz sidhani, wana upole wa woga.
 
Inasemekana ni ya Mkubwa fulani hivi ndio maana wana nyodo ...Hawa dawa yao hao erolink staffs wajiorganise wastrike against them ...

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums

Huo ujasiri wanao watanzania wachache sana mkuu,
 
Hao waajiri wanafanya hivyo kimakosa sana..wanakwepa mambo mengi ikiwa ni pamoja na malipo ya mfanyakazi pindi anapoacha au kuachishwa kazi...ilinitokea new africa hotel wanaweka watu ata kwa mwaka mzima uku wakimwota trainee..kuna kipindi cha nyuma(2008)58%ya wafanyakazi wa pale walikuwa ni trainees sababu ya njaa walikuwa wanaendelea kufanya kazi...ni aina fulani ya utapeli hawana tofauti na magamba...lakini wakupe barua ya kiajiriwa au la (employment contract letter)kisheria ukishafanya sehemu zaidi ya miezi 6 wewe ni mwajiriwa mwenye haki zote
 
Inasemekana ni ya Mkubwa fulani hivi ndio maana wana nyodo ...Hawa dawa yao hao erolink staffs wajiorganise wastrike against them ...

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums

Mkuu erolink nijanga
Nliwaifanya nao vodacom kitengo cha customercare wanyanyasaji hasa na istoshe wamepandikiza watu wao pia so kila mnachotakakukifanya kupigania maslai wao wanakijua dawa ni kuachana nao tu mana hawakamatiki popote.wanatumia ubabe wanafukuza kama mbwa
 
Acheni kubwatuka hamna facts, research wala law...duh hyo data ya 70% hata sijui mmeitoa wapi ...aluu bado inabidi tujielimishe


Sent from JamiiForums
 
Back
Top Bottom