Eritrea panatisha, Bora Tanzania

Hivi inakuwaje mtu mmoja anaweza kuwaburuza mamilioni atakavyo?.Ndio kusema Africa hamnaga wana mapinduzi wa kweli.

Mbona hata hapa jiwe anatuburuza apendavyo. Ni kama hapa tu, kinachofanyika mpaka kufikia huko vyombo vya dola hutumika na sana ni kwakupewa mishahara minono, na hawasumbiliwi wala kukaguliwa vyeti fake. Vyombo vya dola huweza kufanya lolote na hutekwa na maneno ya viongozi kwa kujifanya wazalendo, ghiliba hiyo huwaingia vyombo vya dola na hasa ukizingatia mishahara na marupurupu manono wanayopewa hugeuka vipofu wa unyama wote. Kisha huundwa kundi la watu wasiojulikana, hili hufanya ukatili wa kutisha huku vyombo vya dola vikifumbia macho mambo hayo, mfano hapa kwetu. Viongozi wa vyombo vya dola huhongwa vyeo na kuwa upande wa kiongozi kwa lolote mfano hapa kwetu. Chaguzi zote huwa kiini macho, na wanaotangazwa washindi ni wale wanaotakiwa na mtawala ili kumpitishia sheria zake za ukandamizaji, mfano huo pia uko hapa kwetu.

Bunge na mahakama nazo hujikuta katika hali hii ya kutii kila kitu kwani kundi la watu wasiojulikana hutumika kumnyamazisha yoyote anayekuwa kikwazo. Gia inayotumika kupandikiza unyama wote huu ni neno uzalendo. Yoyote asiyemtii mtawala huonwa ni msaliti. Wakati hayo yakiendelea zaidi ya nusu ya wananchi hulishwa propaganda na ghafla nchi nzima hujikita ikimsifia mtawala wa aina hiyo. Mifano ya mambo hayo iko wazi hata hapa nchini.
 
Kuna watu hawaipendi Tanzania yetu, bora wahamie huko.
 
Mkuu usiseme afadhali ya Tanzania wakati,Magufuli ndo anatamani tufike huko, wakati wa kikwete hali haikuwa Kama ilivyo leo.
Endapo Magufuli atang'ang'ania madarakani na sisi Tanzania tutakuwa kama Eritrea pia, kwanza mpango wake ni kuua sekta zote binafsi ,Tazama alivyoiua fast jet ili ATCL iinuke, amezima uhuru wa Habari hata humu JF yale mazito tunayoandika mods wanayafuta kwa hofu ya kukamatwa.
 
Niliwahi kufika Massawa mji wa bandari wa Eritrea katika harakati za kutafuta maisha. Wakati wa ujenzi wa barabara kutoka Massawa kwenda Asseb.
Miongoni mwa safari zilizonikatisha tamaa sana kutokana na hali mbaya niliyokutana nayo.

Hali yao ni duni sana hasa ikielezwa kwa sababu ya Vita kati yake na Ethiopia (miaka hiyo)
Mambo machache kuhusu Eritrea
1. Nchi ina mfumo wa Chama kimoja na Rais wake ni Isaias Afrwerki ambaye amekuwa rais tangu 1993.

2. Hakuna uchaguzi ambao umewahi kufanyika

3. Nchi ina rekodi mbaya kwenye Haki za Binadamu inaifuatia Korea Kaskazini kwa rekodi mbaya zaidi.

4. Inakadiriwa ina idadi ya watu takribani milioni tano.

5. Vyombo vyote vya habari vinamilikiwa na serikali.

6. Kuna vyuo vikuu viwili tu ambavyo ni Asmara University na Eritrea Institute of Technology.

7. Wana shirika la ndege linalomiliki ndege moja tu Boeing 767-366/ER

8. Kuna wanawake wazuri sana, wanafana sana na Waethiopia.

9. Mjini Massawa kuna vijana wengi wa Kitanzania ambao hufanya kazi kwenye kampuni za Kichina kwenye miradi ya ujenzi.
Nilibahatika kukutana na vijana zaidi ya 40 wa Kitanzania na Kenya.

10. Waeritrea ni wapole sana. Si mahali ambapo kuna fujo na uhuni sana.
 
Wana njaa sana ukiwakuta wanaishi Europe na America walivyo na dharau utafikiri kwao kuna neema
 
Tumefikia kujilinganisha na Eritrea?!
Kweli tumerudi nyuma miaka 50.
Nakulilia Tanganyika yangu.
 
Tanzania majina ya vituo vya televisheni ni mengi lakini taarifa ya habari ni moja kwa vituo vyote.
 

Tatizo letu Watanzania ni kukosa kumbukumbu. Mtu kasema hadharani kuwa anatamani malaika wangeshuka kuja kuzima mitandao; sijui watu walidhani anamaanisha nini.
 
Zitto Kabwe anayelalamika udikteta aende akaishi huko ili auone udikteta wa kweli unafanana vipi.

Mtu analia kunyimwa uhuru wa habari wakati akijisikia tu anaweza kupeleka andiko lake ni likachapishwa gazetini.
 
Zitto Kabwe anayelalamika udikteta aende akaishi huko ili auone udikteta wa kweli unafanana vipi.

Mtu analia kunyimwa uhuru wa habari wakati akijisikia tu anaweza kupeleka andiko lake ni likachapishwa gazetini.
ukiwa na malaria 1 bado unaumwa hata kama icu kuna mtu hajitambui kwa maradhi,haiponyi maradhi yako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…