Desert Voice
Senior Member
- Feb 26, 2018
- 159
- 410
Japokuwa kila mtu anayo haki kikatiba ya kutoa maoni yake, lakini wewe ni bora ungekaa kimya tu.
Tuache sisi tupige kelele kulilia Demokrasia na heshima ya nchi yetu iliyopotea kwa miaka miwili iliyopita.
Leo hii wewe unamwomba Rais Magufuli akutane na viongozi wa dini? wakutane ili iweje?
Umesahau kalamu yako? Unakumbuka ulichokuwa unaandika gazetini kumpigia debe Magufuli?
Unakumbuka jinsi ambavyo ulikuwa unakosa usingizi kwa hofu ya Lowassa akiwa Rais kampuni zako zitafilisika?
"Vipi mume wangu,mbona hadi sasa umeshindwa kulala? "
"Lowassa " .
"Aah, Lowassa hawezi kushinda wewe lala ".
Nimekunukuu andiko lako mwenyewe ktk gazeti la Ijumaa Wikienda.
Watu werevu tulidhani labda ulikuwa na ugomvi binafsi na Lowassa, kumbe una chuki kubwa mno na wapinzani, sikuwahi kutarajia mtu aliyepita mapito magumu kimaisha na mcha Mungu,eti umchukie mtu ambaye hajakukosea lolote.
Wapinzani tunapita ktk kipindi kigumu mno kuwahi kutokea chini ya awamu hii ya tano.
Na hadi sasa hivi viongozi wa dini walipotoa waraka wao kwa serikali kuitaka iheshimu katiba na kurekebisha hali ngumu ya uchumi iliyopo, wamekutana na majibu ya kejeli kuanzia CCM hadi kwa Rais mwenyewe.
Wana ccm wanawaita viongozi wa dini ni vibaraka wa upinzani, na rais kasema kuwa waombe viwanda vya dawa vijengwe na siyo kutoa waraka usio na mantiki.
Sasa wewe unashauri nini wakati ulikuwa hulali Ukitaka Magufuli ashinde?
Humu mitandaoni kuna jeshi kubwa la wana CCM wenzako ambao hawajawahi kuona kasoro zozote za rais Magufuli, kazi yao kubwa ni kusifia tu kila afanyalo rais, kwa nini usiungane nao kusifia, tena una vyombo vya habari.
Sioni sababu kwa nini unalalamika, ni bora ukae kimya kwa sababu utaonekana mnafiki sana.
Unakumbuka pia uliunga mkono Rais Magufuli alivyovunja katiba kwa kupiga marufuku mikutano ya kisiasa?
Mimi ni msomaji Sana wa makala zako, uliandika hivi.
"Rais Magufuli yupo sawa kabisa, muda wa siasa umeisha, huu ni muda kufanya kazi ".
Ulishabikia Rais kuvunja katiba, kwa sababu katiba inaruhusu shughuli za vyama vya siasa na mikusanyiko yake.
Wanacholilia viongozi wa dini ni kile ambacho wewe Ulishabikia kiharibiwe.
Ndo maana nimekuambia kuwa ni bora tu ukae kimya.
Mwache Rais Magufuli afanye kazi, na tuache siye tulie, wewe kaa upande uliochagua.
Tuache sisi tupige kelele kulilia Demokrasia na heshima ya nchi yetu iliyopotea kwa miaka miwili iliyopita.
Leo hii wewe unamwomba Rais Magufuli akutane na viongozi wa dini? wakutane ili iweje?
Umesahau kalamu yako? Unakumbuka ulichokuwa unaandika gazetini kumpigia debe Magufuli?
Unakumbuka jinsi ambavyo ulikuwa unakosa usingizi kwa hofu ya Lowassa akiwa Rais kampuni zako zitafilisika?
"Vipi mume wangu,mbona hadi sasa umeshindwa kulala? "
"Lowassa " .
"Aah, Lowassa hawezi kushinda wewe lala ".
Nimekunukuu andiko lako mwenyewe ktk gazeti la Ijumaa Wikienda.
Watu werevu tulidhani labda ulikuwa na ugomvi binafsi na Lowassa, kumbe una chuki kubwa mno na wapinzani, sikuwahi kutarajia mtu aliyepita mapito magumu kimaisha na mcha Mungu,eti umchukie mtu ambaye hajakukosea lolote.
Wapinzani tunapita ktk kipindi kigumu mno kuwahi kutokea chini ya awamu hii ya tano.
Na hadi sasa hivi viongozi wa dini walipotoa waraka wao kwa serikali kuitaka iheshimu katiba na kurekebisha hali ngumu ya uchumi iliyopo, wamekutana na majibu ya kejeli kuanzia CCM hadi kwa Rais mwenyewe.
Wana ccm wanawaita viongozi wa dini ni vibaraka wa upinzani, na rais kasema kuwa waombe viwanda vya dawa vijengwe na siyo kutoa waraka usio na mantiki.
Sasa wewe unashauri nini wakati ulikuwa hulali Ukitaka Magufuli ashinde?
Humu mitandaoni kuna jeshi kubwa la wana CCM wenzako ambao hawajawahi kuona kasoro zozote za rais Magufuli, kazi yao kubwa ni kusifia tu kila afanyalo rais, kwa nini usiungane nao kusifia, tena una vyombo vya habari.
Sioni sababu kwa nini unalalamika, ni bora ukae kimya kwa sababu utaonekana mnafiki sana.
Unakumbuka pia uliunga mkono Rais Magufuli alivyovunja katiba kwa kupiga marufuku mikutano ya kisiasa?
Mimi ni msomaji Sana wa makala zako, uliandika hivi.
"Rais Magufuli yupo sawa kabisa, muda wa siasa umeisha, huu ni muda kufanya kazi ".
Ulishabikia Rais kuvunja katiba, kwa sababu katiba inaruhusu shughuli za vyama vya siasa na mikusanyiko yake.
Wanacholilia viongozi wa dini ni kile ambacho wewe Ulishabikia kiharibiwe.
Ndo maana nimekuambia kuwa ni bora tu ukae kimya.
Mwache Rais Magufuli afanye kazi, na tuache siye tulie, wewe kaa upande uliochagua.