Erick Shigongo awa Mwanafunzi bora Chuo cha Tumaini

Erick Shigongo awa Mwanafunzi bora Chuo cha Tumaini

MBUNGE wa Jimbo la Buchosa, Mhe. Eric Shigongo, ametajwa kuwa miongoni mwa wanafunzi bora watatu ambao ni wahitimu wa Chuo Kikuu cha Tumaini Dar es Salaam (TUDARCO) katika kozi ya Shahada ya Kwanza ya Mawasiliano ya Umma (Bachelor of Arts in Mass Communication) mwaka 2020.

Hafla ya kukabidhiwa vyeti hivyo imefanyika katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Tumaini Kampasi ya Dar es Salaam, jana Ijumaa, Novemba 20, 2020, na kuhudhuriwa na wanafunzi wahitimu wa kozi mbalimbali chuoni hapo, wanafunzi wanaoendelea na masomo, wahadhiri na wahadhiri wasaidizi na jumuiya ya chuo kikuu hicho.

Shigongo ambaye hajawahi kusoma elimu ya sekondari, alijiunga na chuo kikuu hicho kupitia mfumo wa mitihani ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) uitwao Recognition of Prior Learning (RPL) kutokana na kipaji cha mtu na mchango wake katika tasnia husika. Baada ya kufanya mitihani hiyo mwaka 2017 alifaulu vizuri kwa kupata Daraja A ndipo akapewa kibali na TCU cha kujiunga na masomo ya chuo kikuu.

Licha ya kwamba hajawahi kusoma kabisa elimu ya sekondari kama ambavyo amekuwa akisema waziwazi katika semina na mikutano yake mbalimbali pamoja na vitabu alivyoandika, alivyopata nafasi ya kusoma chuo kikuu, aliamua kusoma kwa bidii darasani na kufuata taratibu zote za chuo hicho huku akijipunguzia baadhi ya majukumu katika makampuni yake ili aweze kuapata muda wa kutosha kujisomea.

“Kwa kweli huwa sipendi kabisa kushindwa, nilipoingia darasani mwaka 2017 kulikuwa na ushindani mkubwa, sababu wenzangu walikuwa wamesoma sekondari mpaka kidato cha sita na wengine walikuwa wana diploma, hivyo nililazimika kusoma sana ili angalau niende nao sawa, lakini juhudi zangu zimezaa matunda kwani nimekuwa mwanafunzi bora baada ya kuhitimu.

“Nimekuwa hapa chuoni kwa miaka mitatu nikisoma, hawaamini kama mimi ni darasa la saba, sijawahi kusoma elimu ya sekondari wala sijui kabisa chochote kusuhu sekondari, lakini leo nina furaha kwamba baada ya masomo yangu nimekuwa mwanafunzi baora lakini pia mbunge wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania

“Niwambie wanafunzi wenzangu mliobaki hapa shuleni na vijana wengine kote nchini, amini kwamba unaweza kuwa chochote, kikubwa ni juhudi zako tu, usikate tamaa, fanya kile unachokiamini, jitume sana utakipata kile unachokipata,” amesema Shigongo baada ya kukabidhiwa cheti cha ushindi.

KONGOLE MWESHIMIWA ERICK SHIGONGO, AMA KWELI BORA KUWA NA AKILI KULIKO KUWA NA ELIMU UKAKOSA AKILI

Awake kwenye CV yake kama kabundi. Huyo mwenye mimacho imo kuwa alikuwa best student wa DS100 pale udsm.

No wonder we have no idea whether the 2020 was anyhow free or fair.
 
MBUNGE wa Jimbo la Buchosa, Mhe. Eric Shigongo, ametajwa kuwa miongoni mwa wanafunzi bora watatu ambao ni wahitimu wa Chuo Kikuu cha Tumaini Dar es Salaam (TUDARCO) katika kozi ya Shahada ya Kwanza ya Mawasiliano ya Umma (Bachelor of Arts in Mass Communication) mwaka 2020.

Hafla ya kukabidhiwa vyeti hivyo imefanyika katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Tumaini Kampasi ya Dar es Salaam, jana Ijumaa, Novemba 20, 2020, na kuhudhuriwa na wanafunzi wahitimu wa kozi mbalimbali chuoni hapo, wanafunzi wanaoendelea na masomo, wahadhiri na wahadhiri wasaidizi na jumuiya ya chuo kikuu hicho.

Shigongo ambaye hajawahi kusoma elimu ya sekondari, alijiunga na chuo kikuu hicho kupitia mfumo wa mitihani ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) uitwao Recognition of Prior Learning (RPL) kutokana na kipaji cha mtu na mchango wake katika tasnia husika. Baada ya kufanya mitihani hiyo mwaka 2017 alifaulu vizuri kwa kupata Daraja A ndipo akapewa kibali na TCU cha kujiunga na masomo ya chuo kikuu.

Licha ya kwamba hajawahi kusoma kabisa elimu ya sekondari kama ambavyo amekuwa akisema waziwazi katika semina na mikutano yake mbalimbali pamoja na vitabu alivyoandika, alivyopata nafasi ya kusoma chuo kikuu, aliamua kusoma kwa bidii darasani na kufuata taratibu zote za chuo hicho huku akijipunguzia baadhi ya majukumu katika makampuni yake ili aweze kuapata muda wa kutosha kujisomea.

“Kwa kweli huwa sipendi kabisa kushindwa, nilipoingia darasani mwaka 2017 kulikuwa na ushindani mkubwa, sababu wenzangu walikuwa wamesoma sekondari mpaka kidato cha sita na wengine walikuwa wana diploma, hivyo nililazimika kusoma sana ili angalau niende nao sawa, lakini juhudi zangu zimezaa matunda kwani nimekuwa mwanafunzi bora baada ya kuhitimu.

“Nimekuwa hapa chuoni kwa miaka mitatu nikisoma, hawaamini kama mimi ni darasa la saba, sijawahi kusoma elimu ya sekondari wala sijui kabisa chochote kusuhu sekondari, lakini leo nina furaha kwamba baada ya masomo yangu nimekuwa mwanafunzi baora lakini pia mbunge wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania

“Niwambie wanafunzi wenzangu mliobaki hapa shuleni na vijana wengine kote nchini, amini kwamba unaweza kuwa chochote, kikubwa ni juhudi zako tu, usikate tamaa, fanya kile unachokiamini, jitume sana utakipata kile unachokipata,” amesema Shigongo baada ya kukabidhiwa cheti cha ushindi.

KONGOLE MWESHIMIWA ERICK SHIGONGO, AMA KWELI BORA KUWA NA AKILI KULIKO KUWA NA ELIMU UKAKOSA AKILI
Haiwezekani ni uongo mtu kashinda zaidi ya miezi 4 kwy kampeni alafu awe mwanafunzi Bora, labda kawa mwanafunzi Bora kwa vilaza
 
Kuna elimu ya darasani na elimu ya uraiani yaani maisha.
Binafsi mm pia STD 7 ila naongoza watu wenye Degree za Udom na UD.
na muda mwingine mtu ukimwambia hujawahi kuingia mlango wa secondr atabisha hadi mishipa ya fahamu itasimama.
 
Hizi mbwembwe hizi,hakuna kitu hapo,Wala sio ajabu,Mbunge Msukuma hakwenda shule,Diamond hakwenda shule,Mzee Bakheresa alikuwa anauza ice cream miaka ya 80,
Sasa maswala ya kwenda na benz,V8,Vogue,!what is the heck!!!hayo magari ya kawaida sana kitaa,
Kwanza Elimu aliyosoma ni nyepesi sana,angesoma uandisi wa mitambo,mechanical engineering,au civil,au umeme,Tena kwenye chuo Kama UD,au Udom,au DIT,tungesema yeees,
Kule south Africa,Kuna binti kapiga shahada ya Kwanza,ya pili(masters)mpaka PHD Tena ana miaka 30,kutoka bongo,hayo ndio Maajabu sio hizi Kiki,wajameni
 
Hizi mbwembwe hizi,hakuna kitu hapo,Wala sio ajabu,Mbunge Msukuma hakwenda shule,Diamond hakwenda shule,Mzee Bakheresa alikuwa anauza ice cream miaka ya 80,
Sasa maswala ya kwenda na benz,V8,Vogue,!what is the heck!!!hayo magari ya kawaida sana kitaa,
Kwanza Elimu aliyosoma ni nyepesi sana,angesoma uandisi wa mitambo,mechanical engineering,au civil,au umeme,Tena kwenye chuo Kama UD,au Udom,au DIT,tungesema yeees,
Kule south Africa,Kuna binti kapiga shahada ya Kwanza,ya pili(masters)mpaka PHD Tena ana miaka 30,kutoka bongo,hayo ndio Maajabu sio hizi Kiki,wajameni


Shigongo ni muandishi wa hadithi na habari.. biashara yake ni mmiliki wa vyombo vya habari... utajiri wake kaupata kwenye magazeti ya habari..

Kaenda chuo kusomea taaluma ya habari ambayo anaifanya kupata utajiri...wewe unataka akasome engineer kama anauza mitambo ya engineering ama ana kampuni ya ujenzi... ama angesomea udaktari kama anamiliki kairuki hospital vile?

Huyo binti wa south hana uwezo wa kumuajiri shigongo...ila shigongo ana uwezo wa kumuajiri huyo binti...hapo ndipo tofauti ilipo... kutengeneza hela mpaka kuwa tajiri ni kipimo kikubwa sana cha akili kuliko kukariri madesa
 
Shigongo chuo anaenda na range rover.. siku nyingine V8, siku nyingine benz... yaani pale tumaini gari ya shigongo hupati shida kuigundua maana haifanani na zingine zote...

Walimu wa Tumaini na wafanyakazi wote wa chuo full shobo kwa shigongo .. kwa nini asiwe mwanafunzi bora?

Shigongo kuanzia ma lecture, wafanyakazi wa canteen, ma secretary mpaka wafagiaji wa chuo walikuwa wanamuheshimu sana..
Degree yenyewe ya Mass Com
 
I mean ni rahisi kuwa mwanafunzi bora kwa course hiyo.

Shigongo ameenda chuo kurasimisha ujuzi na kujifunza zaidi.. ila ujuzi wa mass communication alikuwa nao tayari kwa experience kubwa kuliko wanafunzi wenzake waliotoka straight shuleni... sasa why asiwaongoze?

Na inasemekana wanafunzi wenzake wote darasani waliokosa nafasi za field...shigongo aliwaruhusu waje wakafanye field kwenye kampuni yake
 
Hizi mbwembwe hizi,hakuna kitu hapo,Wala sio ajabu,Mbunge Msukuma hakwenda shule,Diamond hakwenda shule,Mzee Bakheresa alikuwa anauza ice cream miaka ya 80,
Sasa maswala ya kwenda na benz,V8,Vogue,!what is the heck!!!hayo magari ya kawaida sana kitaa,
Kwanza Elimu aliyosoma ni nyepesi sana,angesoma uandisi wa mitambo,mechanical engineering,au civil,au umeme,Tena kwenye chuo Kama UD,au Udom,au DIT,tungesema yeees,
Kule south Africa,Kuna binti kapiga shahada ya Kwanza,ya pili(masters)mpaka PHD Tena ana miaka 30,kutoka bongo,hayo ndio Maajabu sio hizi Kiki,wajameni

mkuu, mbona unachukulia hiyo jamaa kwenda chuo na range kama show off wakati mwenzio ndio uwezo wake ulipo ?
wala haendi nazo hizo gari ili aonekana hapana ni watu wanaomuona hasa sisi vijana tunajikuta tunatamani hizo gari na kuishia kumsifu lakini haimaanishi jamaa kuendesha hizo ndinga ni kutaka sifa
mkuu punguza jazba ume panic sana,let us let the man live his life he deserve it
 
Ningependa kujua chuo hicho (TURDACO) kimemdahili vipi Shigongo kama ni kweli hana elimu ya secondary? Je kuna njia tofauti alipitia?
 
Mimi sijaelewa kwamba ameenda kuchukua degree akiwa na elimu ya darasa la saba?
Kwangu naona hapa kuna kitu hakisemwi. Hakuna Chuo Tanzania kitakudahili ukiwa na elimu ya darasa la 7 tena enzi hizi za uncle Magu. Ni kipi cha zaidi alifanya hadi akapata udahili hapo chuoni na udahili wake ukathibitishwa na TCU? Wanaojua watueleze.
 
Kwangu naona hapa kuna kitu hakisemwi. Hakuna Chuo Tanzania kitakudahili ukiwa na elimu ya darasa la 7 tena enzi hizi za uncle Magu. Ni kipi cha zaidi alifanya hadi akapata udahili hapo chuoni na udahili wake ukathibitishwa na TCU? Wanaojua watueleze.

Ni program maalum. Vyuo vingi vinafanya hivyo. Wanawachukua ma CEO kutoka katika makampuni yanayofanya vizuri na watu waliobobea katika fani mbali mbali kwenda kurasimisha ujuzi wao.
 
Shigongo ndie kiumbe pekee alieamua kujiajiri na kutengeneza maisha kisha ndio akaenda kusoma.

Mtu mwenye akili ya kuendesha Mass Media Press company kwa mafanakio makubwa na kuajiri mamia ya wafanyakazi huku akiweza kuwa manage vizuri na kujitengenezea ukwasi wa aina yake ingenishangaza sana kama angeshindwa kumaliza degree ambayo ime base kwenye kukariri madesa na kutapika😂!

Achilia mbali tu matumizi yake ya u "MOGUL" katika tasnia ya habari na mawasiliano na nguvu ya pesa.
 
Chuoni anaenda na magari ya bei juu.. mpaka ma lecture wanayashangaa.. kasoma kibabe sana shigongo... yeye kila desa ama kitabu anapewa moja kwa moja haangaiki kutoa ma photocopy.. baadae anapewa bill tu na mwalimu.. analipia
Hahahahah hii ni ndoto yangu nikienda kusoma Masters, lazma niende kama shigongo. Siwezi kusoma Masters kimasikini 😂😂😂
 
Ukiwa na title na pesa walimu wa chuo wanakuogopa... kuna watu wamesoma PHD part time na wamezipata muda mfupi kuliko wanaosoma full time na hawajawai kuonekana maaabara na thesis zao hazieleweki
Mmenikumbusha sijui ni mar Saanane
 
Back
Top Bottom