Equity Bank wanahujumu uchumi wetu

Equity Bank wanahujumu uchumi wetu

Syzygus

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2014
Posts
267
Reaction score
118
Wadau,

Hata kama ni uwekezaji lazima ufuate sheria za nchi husika, lazima kuwe na win win situation.

Kwa bahati mbaya sivyo hivyo kwa haya mabenki ya nje yanayofurika nchini kila uchao, wanakuja kutuibia na kutuhujumu. Najiuliza, wanapata wapi ujasiri wa kukiuka masharti ya biashara na uwekezaji? Hivi ni kweli Benki Kuu haina mechanism ya kucheki kama haya mabenki yanafuata sheria za nchi.

Wiki tatu zilizopita nilienda Equity Bank pale Golden Jubilee kuchenji dola elfu mbili ili nipate shilingi niweze kufanya malipo mbali mbali ya kiofisi. Nilipofika Equity Bank nilielekezwa nipande ghorofani ambapo nilimpatia teller hizo dola ili anipe shilingi. Ajabu ni kuwa, nilipomwomba risiti akagoma ati hawatoagi risiti! Nikamwambia hicho kitu haiwezekani na hakipo, dada akasema ndivyo ilivyo na akamuuliza jirani yake ili nithibitishe, na mwenzake akanithibitishia! Ndipo nikawaambia wanirudishie dola zangu nikaenda kubadilishia Bureau de Change ambao baada ya kudai risiti walinipa.

Ijulikane kuwa hata hizo Bureau de Change nao ni hivyo hivyo, risiti ni hadi uidai. Wenzetu Uganda hata ukiwa unauza dola ili upate shilingi yao lazima wadai passport na wajaze fomu kadhaa na kukupa risiti yako, yaani huhitaji kuuliza.

Nachotaka kusema ni kuwa hawa Equity Bank wanahujumu uchumi wetu, wanatorosha dola zetu kupeleka kwako na hivyo kusababisha kushuka na kuporomoka kwa shilingi yetu.
 
Sasa wewe unatarajia nini kitokee pale watu wanapopata nafasi ya kuingia kwenye shamba la bibi?
 
Kama wako hivyo wanakosea sana
 
Wapi Mchumi Mbobezi wa Daraja la Kwanza jamani..!!
 
Tatizo ni kuwa watu waliopewa nafasi ndani ya vyombo vyetu yya umma kufuatilia na kudhibiti mambo kama hayo, wako busy kughushi nyaraka na kufanya uizi maofisini badala ya kufanya kazi walizoajiriwa. Scandal nyingi za wizi wa hela ya umma zimenzia BOT
 
Wadau,

Hata kama ni uwekezaji lazima ufuate sheria za nchi husika, lazima kuwe na win win situation.

Kwa bahati mbaya sivyo hivyo kwa haya mabenki ya nje yanayofurika nchini kila uchao, wanakuja kutuibia na kutuhujumu. Najiuliza, wanapata wapi ujasiri wa kukiuka masharti ya biashara na uwekezaji? Hivi ni kweli Benki Kuu haina mechanism ya kucheki kama haya mabenki yanafuata sheria za nchi.

Wiki tatu zilizopita nilienda Equity Bank pale Golden Jubilee kuchenji dola elfu mbili ili nipate shilingi niweze kufanya malipo mbali mbali ya kiofisi. Nilipofika Equity Bank nilielekezwa nipande ghorofani ambapo nilimpatia teller hizo dola ili anipe shilingi. Ajabu ni kuwa, nilipomwomba risiti akagoma ati hawatoagi risiti! Nikamwambia hicho kitu haiwezekani na hakipo, dada akasema ndivyo ilivyo na akamuuliza jirani yake ili nithibitishe, na mwenzake akanithibitishia! Ndipo nikawaambia wanirudishie dola zangu nikaenda kubadilishia Bureau de Change ambao baada ya kudai risiti walinipa.

Ijulikane kuwa hata hizo Bureau de Change nao ni hivyo hivyo, risiti ni hadi uidai. Wenzetu Uganda hata ukiwa unauza dola ili upate shilingi yao lazima wadai passport na wajaze fomu kadhaa na kukupa risiti yako, yaani huhitaji kuuliza.

Nachotaka kusema ni kuwa hawa Equity Bank wanahujumu uchumi wetu, wanatorosha dola zetu kupeleka kwako na hivyo kusababisha kushuka na kuporomoka kwa shilingi yetu.

Lengo la kuficha risit ni ili TRA wasijue wanapata faida kiasi gani . Nchi ya hovyo hovyo kabisa hii
 
Mtoa maada umesema mwenyewe kuwa hata huko Bureau De Change ni mpaka uombe risit ndo unapewa vinginevyo hupewi....sasa hapa ni kuwaonea Equity Bank bila sababu yeyote. BOT ndo tatizo usig=dhani kwamba hawajui...wanjua kwa undani kuliko wewe ufikiriavyo na hii sio jambo jipya. Kila mradi ama bank hapa nchini vigogo na wtawala wana share zao humo kwahiyo tuwalaumu viongozi wetu kabla ya kuwalaumu Equity Bank.
 
Acha mambo yako wewe kwanza equity bank wako vizuri sana mie nina akaunti yangu pale ya dola tena wako vizuri sana kwenye rate zao sio kama mabenki yetu hapa wanatudhulumu sana sasa ukienda crdb, nmb au nbc utaambiwa dola1=1700tsh badala ya 2000tsh, lakini equity wanawazidi hata hizo bureau de change kwa rate. Watu wengi siku hz wanaenda kubadilishia fedha zao equity kwa sababu hizo, na mie risiti huwa napewa!
 
hoja zuri lakini haitapata watu wa kuchangia kwa sababu wachangia wa forum hii wanapenda kujadili watu badala ya issue

Uliandika vizuri ila ulipochanganya lugha ndo umeharibu kabisa
 
Hapana sio kweli ukiomba risit equity unapatiwa labda km hao mateller walikuwa wageni lakini inawezekana kabisa
 
Hivi unesoma mada na kuielewa au umekurupuka kujibu kwa kuwa kuna mpwa wako anafanya kazi pale?

Point kubwa hapa ni wizi unaofanywa na Bank hiyo dhidi ya mapato ya nchi yako Tanzania, wanauza bidhaa hawataki kutoa receipt.

Acha mambo yako wewe kwanza equity bank wako vizuri sana mie nina akaunti yangu pale ya dola tena wako vizuri sana kwenye rate zao sio kama mabenki yetu hapa wanatudhulumu sana sasa ukienda crdb, nmb au nbc utaambiwa dola1=1700tsh badala ya 2000tsh, lakini equity wanawazidi hata hizo bureau de change kwa rate. Watu wengi siku hz wanaenda kubadilishia fedha zao equity kwa sababu hizo, na mie risiti huwa napewa!
 
Kwa nini una badlisha fedha za kigeni Bank, "Rate" zao ni ndogo sana. Nenda kwenye maduka ya kubadilisha fedha, "Rate" nzuri na hawana longo longo kwenye kutoa risiti.
 
Hapana sio kweli ukiomba risit equity unapatiwa labda km hao mateller walikuwa wageni lakini inawezekana kabisa

Heeeeee!!!!!! Wajameni!!!! Why mpaka uombe risiti???? Tena hawa Equity objective yao from the beginning ni kuua kabisa mabenki yetu hapa TZ halafu wafanye watakalo. Tena kwenye hizo consultancy wanatoa rushwa nje nje ili kufanikisha malengo yao.

WaTZ hasa viongozi kuweni makini tusiiue nchi yetu kwa MIKONO yetu wenyewe!!! Hata haya mambo kila Consultancy wanapewa wa Kenya hiyo ni DHARAU. Pia Siri nyingi za Serekali na mashirika ya UMMA wanazijua!!!! TUKO UCHIII.

Hata nyumba yako isipokuwa na controls na limitation inakuwa Kama pagala la wanyanganyi.

Katiba na sheria ziweke wazi mtanzania apewe nafasi ya kwanza kwenye ushindani wa consultancy zinazohusu mambo ya Serikali na mashirika ya UMMA hasa kwenye maeneo ambayo uwezo huo tunao. Aidha anapokiuka makualiano afungwe na Hilo litaleta uwajibikaji.

Hawa majirani zetu sio wazuri ki hivyo, ni hicho Kiingereza chao tuu ndio kinawapaisha. Tuwekeze kwenye elimu kwa watoto wetu jamani.

Ni hayo tu.

Queen Esther
 
Hivi unesoma mada na kuielewa au umekurupuka kujibu kwa kuwa kuna mpwa wako anafanya kazi pale?

Point kubwa hapa ni wizi unaofanywa na Bank hiyo dhidi ya mapato ya nchi yako Tanzania, wanauza bidhaa hawataki kutoa receipt.

Bt kubadilisha hela kwan kuna mapato unalipia?!!cjaelewa coz zile rate zimequotiwa cdhani km kuna vat pale
 
Si Equity Bank tu,hapa Tanzania hakuna udhibiti wowote wa exchange ya pesa za Kigeni.Nchi za Wenzetu mfano Rwanda kuna udhibiti mkubwa wa Pesa za Kigeni,ni sehemu chache wanakopokea malipo kwa pesa yakigeni.Nenda India,ukienda India mwaka hadi Mwaka rupee 4 ni Dolar 1.Ukienda hata kwenye duka la kuuza pesa unahitaji Dolar lazima ujaze form yenye maelezo malefu kama una haraka ya Kitanzania Unaweza ukaondoka bila kuhudumiwa.Unaambiwa utoe Passi ya kusafiria, makusudi ya dola hizo labda niza matumizi ukiwa kwnye Transit nyumbani,lakini ukisema unahitaji kufanya shopping India utaambiwa utumie Rupee .
 
Kama hili ni kweli unaweza kuwa'report F.I.U wawafuatilie coz kwa bank hauwez kufanya multi currency transaction kama hauna suporting evidence, sasa sijui in your case walikubadilishiaje kama huna multi-currency accounts
 
Back
Top Bottom