Epuka sana kukopesha mtu pesa

Epuka sana kukopesha mtu pesa

Aisee. Mdaiwa afungwi.
Katika maisha yako ya utafutaji epuka sana kumkopesha mtu pesa kwa lengo la kurudishiwa pesa yako ya awali.

Kumbuka kuwa pesa unayompa mtu kwa mkopo sio yako tena.

Aliwai kuniambia baba yangu"mtu akikuomba umkopeshe pesa mpe nusu ya pesa alio omba kama sadaka mbele ya Mungu, Ila usije weka matarajio yeyote kwa pesa uliomkopesha mtu.

Mfano
Rafiki akikuomba umkopeshe elfu Kumi...basi wewe kiroho Safi mpe elfu tano ili kumuwezesha katika jambo husika.

Sio ndugu
Sio rafiki
Wala nini.

Usikopeshe Ila wezesha.

Wapo wengi sana walirudishwa nyuma kwa kukopesha pesa kwa watu.

Asante
Umenena
 
Aisee. Mdaiwa afungwi.
Katika maisha yako ya utafutaji epuka sana kumkopesha mtu pesa kwa lengo la kurudishiwa pesa yako ya awali.

Kumbuka kuwa pesa unayompa mtu kwa mkopo sio yako tena.

Aliwai kuniambia baba yangu"mtu akikuomba umkopeshe pesa mpe nusu ya pesa alio omba kama sadaka mbele ya Mungu, Ila usije weka matarajio yeyote kwa pesa uliomkopesha mtu.

Mfano
Rafiki akikuomba umkopeshe elfu Kumi...basi wewe kiroho Safi mpe elfu tano ili kumuwezesha katika jambo husika.

Sio ndugu
Sio rafiki
Wala nini.

Usikopeshe Ila wezesha.

Wapo wengi sana walirudishwa nyuma kwa kukopesha pesa kwa watu.

Asante
Kuna jamaa mpaka leo hawezi kuongea nami kwa sababu anajistukia kanikopa pesa halafu hajarudisha.
 
nina List ya marafiki wangu 6 ambao nimewakopesha fedha hata salamu hatusalimiani,


huwa nashindwa hata kuwajulia hali maana wataona kama nawakumbusha deni.

kinachoniuma ni watu wangu wa karibu daaah
Waambie umewasamehe, watakuelewa
 
Hivyo ni vitu viwili tofauti,
Kukopa mbali na kusaidia mbali,
Huwezi enda benki au kwa yeyote yule utake mkopo wa milioni 200 halafu wakuonee huruma wakupe milioni 100,
Kukopesha na kukopa ni fani ukifuata kanuni zake wala hakuna shida,
Mfano chukua dhamana kwa kila mkopo
Na vitu kama hivyo
 
Katika maisha Ni bora mtu akuone mbaya kwa kumwambia Sina kuliko wewe kuja kumuona mbaya pindi pale unapomdai na yeye anakuwa anakuzungusha kukupa pesa yako.
Kweli kabisa, ila wabongo tumezidi jamani, unakuta mtu anakusumbua kuwa ana matatizo ya kiasi fulani. Unampa, pale pale anaanza kuwa adui yako na kukusema kwa watu ili tu mgombane kisha asikulipe. Nimejifunza mengi sana na watanzania wenzangu.
 
***** nimemkopa jamaa Kama laki 2 tukiwa safarini akaniambia kasahau kadi nimpe tunatoka mwanza ilikuwa jumanne na hapo mi nilikuwa nayo nikampa kasena jumatano anakamlisha ya wiki iliyopita

Na huku tumemaliza kazi pesa tulipewa jumatano hyo maana tumefika jumatatu mpaka leo jamaa hajanipa hana hata wasiwasi
 
Ukweli mchungu ni kwamba ili ufanikiwe lazima uwe na Roho ngumu I mean acha kukopesha

Matajiri wengi Wana Roho ngumu mno ndo maana wanatoboa
Ila hao matajiri wanakopeshana pesa pia.

Binafsi naona, tukopeshane tu pesa kwa sababu wengine tunakuwa tumetingwa na hatuna namna.

Binafsi naona ni bora kuwa na marafiki na ndugu wachache wenye tija, kuliko kuwa na marafiki na ndugu wengi wasio na tija.

Yaani nikiwa na shida usiponikopesha pesa wakati unazo, basi nakata mawasiliano na wewe kwa sababu hauna faida kwangu. Ukiugua siji kukuona, ukipata msiba siji, pesa zako zikusaidie!

Unaweza kuwa na pesa, ila unahitaji msaada wa wafu pia, mf, nguvu kazi ukiwa unashida.

Tukopeshane, kwa sababu tunategemeana. Mtu mmoja akikudhulumu isiwe kigezo cha kuacha kukopesha wengine waaminifu.
 
Tena nakazia ndugu au rafiki au wale imani ,moja iwe kanisani au msikitin USIJARIBUU HATA SIKU MOJa UTAJUTA
 
Ukitaka kumkopesha mwanamke. Mkopeshe aliyekuzidi umri awe sawa na mama au shangazi yako. Ila ukimkopesha ambaye mpo rika moja. Imekula kwako
Nishaacha kukopesha watu na huwa sina mazoea ya kukopa pesa kwa mtu.
Unakuta mwanamke mmezoeana na hakuna uhusiano wa kimapenzi anaomba umkopeshe hela, ukimkopesha harudishi, wanaume wengine kudai mwanamke akurudishie fedha uliyomkopesha ni aibu
 
Mkuu. Hivi kweli deni la kukopeshwa na MTU halimfungi mdaiwa?
Je Kama kakopa TALA au benki?
 
Ukitaka kumkopesha mwanamke. Mkopeshe aliyekuzidi umri awe sawa na mama au shangazi yako. Ila ukimkopesha ambaye mpo rika moja. Imekula kwako
Nishaacha kukopesha watu na huwa sina mazoea ya kukopa pesa kwa mtu.
Kumbe wewe huwajui wamama wa mujini vizuri.
Huyo huyo unayemsema ana umri sawa na wa bi mkubwa anaweza kukufanyia kitu hutakaa usahau.
Kama ungekua umewahi kupanga kwenye nyumba ya singo maza sawa na bi mkubwa wakati wewe ni bachela usinge thubutu kukopesha hili kundi.
 
Kwa Dar nakubaliana na wewe ila huku mikoani wanaadabu.
Kumbe wewe huwajui wamama wa mujini vizuri.
Huyo huyo unayemsema ana umri sawa na wa bi mkubwa anaweza kukufanyia kitu hutakaa usahau.
Kama ungekua umewahi kupanga kwenye nyumba ya singo maza sawa na bi mkubwa wakati wewe ni bachela usinge thubutu kukopesha hili kundi.
 
Kinachofuata ni kupoteza urafiki/udugu na pesa zako pia. Mtu akitaka kukukopa ni bora umuelekeze kwenye taasisi za fedha akakopeshwe huko.
 
Ila hao matajiri wanakopeshana pesa pia.

Binafsi naona, tukopeshane tu pesa kwa sababu wengine tunakuwa tumetingwa na hatuna namna.

Binafsi naona ni bora kuwa na marafiki na ndugu wachache wenye tija, kuliko kuwa na marafiki na ndugu wengi wasio na tija.

Yaani nikiwa na shida usiponikopesha pesa wakati unazo, basi nakata mawasiliano na wewe kwa sababu hauna faida kwangu. Ukiugua siji kukuona, ukipata msiba siji, pesa zako zikusaidie!

Unaweza kuwa na pesa, ila unahitaji msaada wa wafu pia, mf, nguvu kazi ukiwa unashida.

Tukopeshane, kwa sababu tunategemeana. Mtu mmoja akikudhulumu isiwe kigezo cha kuacha kukopesha wengine waaminifu.
Acha kujipa umuhimu kwenye maisha ya watu....mtu kama ww sikupi hata mia nyie ndo hamlipagi madeni.
 
Back
Top Bottom