Ila hao matajiri wanakopeshana pesa pia.
Binafsi naona, tukopeshane tu pesa kwa sababu wengine tunakuwa tumetingwa na hatuna namna.
Binafsi naona ni bora kuwa na marafiki na ndugu wachache wenye tija, kuliko kuwa na marafiki na ndugu wengi wasio na tija.
Yaani nikiwa na shida usiponikopesha pesa wakati unazo, basi nakata mawasiliano na wewe kwa sababu hauna faida kwangu. Ukiugua siji kukuona, ukipata msiba siji, pesa zako zikusaidie!
Unaweza kuwa na pesa, ila unahitaji msaada wa wafu pia, mf, nguvu kazi ukiwa unashida.
Tukopeshane, kwa sababu tunategemeana. Mtu mmoja akikudhulumu isiwe kigezo cha kuacha kukopesha wengine waaminifu.