Enziiii za Mwalimu

Enziiii za Mwalimu

Mwakumbuka Gurubiti za kijiti cha chelewa, Mabumunda je?? Good Good je? mwakumbuka tulikuwa twala mapera kwa wingi sana??

Nakumbuka hizo enzi nasoma Lake Primary School - Isamilo na Nyanza Primary pia nilisoma jamani kaaaaa sijui kama mwalimu Tumbo yupo mpaka leo

lol! yaani umenichekesha sana! umenikumbusha mbali kweli hasa Gulibiti!! haha haa na enzi zile pipi tulikuwa tunaita peremende na chewing gum ilikuwa bazoka!!

Du wale waliosoma Wilolesi Iringa kwa Kajiba, enzi hizo kila J3 na Alhamisi kuna parade, ilikuwa shule ya kikakamavu! du kulikuwa na adhabu za kulowekwa kwenye pipa!! mh nahisi angefanya hivyo kwa sasa wangemtia ndani Mwl. Kajiba! Lakini alikuwa ni mwl maalumu kwa kurekebisha tabia! Ukumbukwe mwl Kajiba popote ulipo nakupa heshima yako!

Nakumbuka asubuhi unawahi namba, mkononi una fagio la chelewa, kidumu cha maji, mbolea, maua and sometimes panga, fyekeo au jembe! du enzi zi la full Kayumba tulikomaje? sio sasa hivi watoto wetu hawajui lolote!!!!
 
Ukweli kabisa Mama Joe nakumbuka shuleni kwetu walifundisha mpaka ufundi, useremala, kutengeneza vigae vya kuezekea, na waliofanya vizuri walizawadiwa zana za kufanyia kazi!..SIPATI PICHA LEO TUNGEKUWA WAPI KAMA TUNGEKUWA NA MFUMO MZURI WA ELIMU!
sana I see yaani nimemaliza primary nikijua kukata na kushona nguo hata kama ilikuwa ni kwa kutumia mikono lakini ni elimu tosha, kulikuwa na cookery hadi secondary. Pia kulikuwa na hiyo useremala na bustani za nyanya mbogamboga hadi ufugaji kwa hiyo ulikuwa ukitoka shule unajua kilimo cha kisasa kwa kiasi Fulani unaweza anza kujitegemea kabisa. Mitaala imebadilishwa weee hata sijui tunaenda wapi?
 
Dah, hii thread ni yaukweli
EK: Elimu ya kijitegemea, lazima uwe na bustani ya nyanya au mchicha
Chezea sayansi kimu wewe, siku ya kupika shuleni hutamani kurudi home
Kabalagala, mbute,
I hate good good, nilizila sana nilipokuwa mwanza sec, leo cha moto nakiona kila siku kwa dr wa meno, sina hamu na ubishoo wa gud gud
Kila sikukuu ya chama na serikali wanafunzi kwenye maandamano hata kama ni jumapili
Mwalimu Tumbo alishafariki kitambo


Mwakumbuka Gurubiti za kijiti cha chelewa, Mabumunda je?? Good Good je? mwakumbuka tulikuwa twala mapera kwa wingi sana??

Nakumbuka hizo enzi nasoma Lake Primary School - Isamilo na Nyanza Primary pia nilisoma jamani kaaaaa sijui kama mwalimu Tumbo yupo mpaka leo
 
Jamani acheni yaani nimecheka hadi basi bila kusahau jiwe, nakumbuka shule yetu kulikuwa na mmomonyoko wa udongo, pamoja na hivyo ulivyovitaja lazima ubebe jiwe huku mfuko wa madaftari halafu hapo ni masika sasa huku mvua inawapiga, no mwavuli no nini lol!
Darasani hakuna dawati ni chini au unakalia jiwe, Kweli enzi za mwalimu....!


Nakumbuka asubuhi unawahi namba, mkononi una fagio la chelewa, kidumu cha maji, mbolea, maua and sometimes panga, fyekeo au jembe! du enzi zi la full Kayumba tulikomaje? sio sasa hivi watoto wetu hawajui lolote!!!!
 
sana I see yaani nimemaliza primary nikijua kukata na kushona nguo hata kama ilikuwa ni kwa kutumia mikono lakini ni elimu tosha, kulikuwa na cookery hadi secondary. Pia kulikuwa na hiyo useremala na bustani za nyanya mbogamboga hadi ufugaji kwa hiyo ulikuwa ukitoka shule unajua kilimo cha kisasa kwa kiasi Fulani unaweza anza kujitegemea kabisa. Mitaala imebadilishwa weee hata sijui tunaenda wapi?


Yaani kweli kabisa elimu ya sasa inawandaa watoto wetu wawe tegemezi kabisa! hawajui hata kushona, enzi zile lile somo la Sayansikimu lilitusaidia sana mpaka sasa tunaweza kufuma na kushoa, watoto wa sasa utawasikia nguo imechanika kumbe imefumuka hawawezi hata kuishona.

Tulijua kulima na kutunza bustani, yaani kama mimi shule niliyosoma nilijifunza hata kuponda kokoto! Wiloles + Kabiba oyeeee! Japo walimu walikuwa wakitutwisha mijideli ya icecream lakini on other way walikuwa wakitufunisha mahesabu na pia kujishughulisha na kazi zingine zinazowezakutuingizia vipato! leo mimi hata kibarua changu kiote nyasi sikosi cha kufanya na kutake care of my family.....

Hasa hizi international schools, japo ndo tunapeleka watoto wetu, lakini hawajui cha kufanya usafi wa darasa, choo, wala bustani, kushona nguo hata kupinda, hata alama za nguo zao waliopo boarding is issue..................
 
Ahahahahahhhh, dah yaani nimecheka kwa sauti hadi wenzangu wamenishanga, Hakyanani nimekumbuka mbali sana. Halafu kukariri tebo darasa la pili, nakumbuka mkimuona tu mwalimu ametoka ofisini darasa zima mnasimama mnaanza kuimba tebo, akiingia darasani wote mnanyamanza anaanza kuuliza mtu mmoja mmoja, ole wako ushindwe kujibu, utajuuuta kumfahamu mwl Samson lol!

Darasa la tano sitakuja kusahau hesabu za vipeuo, K.D.S na K.K.S wapi mwl Bunango, ulinichapa sana mama lakini ahsante ulinisaidia na kunifanya niwe hapa nilipo leo


Na ole wako usahau dada yake Juma anaitwa nani (Roza) kwenye Kiswahili kwenye vitabu vile 'Tujifunze Lugha Yetu' Kwenye English lazima ujue Mr & Mrs. Daud na watoto wao Musa na Neema wanaosoma Mtakuja Primary School. Those were the good old days!!!!
 
tukienda kwenye soka hatukusahau kushangilia kuwa Joshua! joshua! joshua! namna huyo! ukitoka nione!. mtu akimkata mtama unamjibu wewe, wewe usiniumizie!
mkuu nashukuru kwa kutukumbusha ya enzi zile!


Kumbe alifundisha watu jinsi ya kula KULAMBAKISHIE BABA siku hizi watu wanahomola kila kitu

Sent from my BlackBerry 9700 using Jamii Forums
 
Enzi hizo ukitoka shule bila kuchapwa unamshukuru Mungu
Mnatoka saa sita na nusu kwenda kula home, saa nane mnatakiwa mrudi shule, jua kali halafu unafika home unakua hakuna msosi, anambulia kunywa maji then unageuza

Sitasahau halaiki ya mwaka 1986 kuzima mwenge kitaifa mkoani mwanza, tulihenyeshwa balaaa
 
...Wamo humu wa Mfaranyaki Primary School, Songea LY Class ya 1974...Sijakosea, 1974 ???? 🙂🙂
 
Enzi hizo ukitoka shule bila kuchapwa unamshukuru Mungu
Mnatoka saa sita na nusu kwenda kula home, saa nane mnatakiwa mrudi shule, jua kali halafu unafika home unakua hakuna msosi, anambulia kunywa maji then unageuza

Sitasahau halaiki ya mwaka 1986 kuzima mwenge kitaifa mkoani mwanza, tulihenyeshwa balaaa
duh nilikuwa naogopa sana viboko, ajabu nilianzia shule ya Nyakahoja hapo Isamilo hawakuwa wanachapa kabisa ukikosa kuna kusimama nje ya staffroom hadi jioni....ajabu tulikuwa tunaogopa sana tunaita prison....mtu analia kweli na wote tunawaona wameadhibiwa kweli...kuja hama mkoa nikaenda kwa kayumba duh chamoto nilikiona! Kikubwa tulikuwa tunafundishwa kiasi huitaji tuition na unafaulu national exam ka kusoma tu mwenyewe nyumbani. Go tell this to my kids lol...
 
Umesahau kufagilishwa vyoo na kulimishwa mjini.
 
Umesahau kufagilishwa vyoo na kulimishwa mjini.
mmm kweli kulikuwa na kazi za ajabu...ila ukiwa mtii na msafi unapewa kazi ya kutunza ofisi za walimu au maktaba nashukuru niliponea maana vile vyoo unatoka na perfyum kali...
 
Ahahahahahhhh, dah yaani nimecheka kwa sauti hadi wenzangu wamenishanga, Hakyanani nimekumbuka mbali sana. Halafu kukariri tebo darasa la pili, nakumbuka mkimuona tu mwalimu ametoka ofisini darasa zima mnasimama mnaanza kuimba tebo, akiingia darasani wote mnanyamanza anaanza kuuliza mtu mmoja mmoja, ole wako ushindwe kujibu, utajuuuta kumfahamu mwl Samson lol!

Darasa la tano sitakuja kusahau hesabu za vipeuo, K.D.S na K.K.S wapi mwl Bunango, ulinichapa sana mama lakini ahsante ulinisaidia na kunifanya niwe hapa nilipo leo

Ram,
Huyo mwalimu Bunango alikufundisha wapi na miaka ipi? Halafu kulikuwa na hesabu ya kangaroo darasa la 5 (au la 6???)
 
Amenifundisha Mwenge shule ya msingi, mwanza
Alikuja mwenge 1988 nilimaliza nikamuacha, huwezi amini bado anafundisha hadi leo, nw anafundisha Nyanza shule ya msingi

Ram,
Huyo mwalimu Bunango alikufundisha wapi na miaka ipi? Halafu kulikuwa na hesabu ya kangaroo darasa la 5 (au la 6???)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom