ENZI ZILE (Tukumbushane)

Nakumbuka nikiwa std 2 kulikuwa na vichongeo vya penseli vilivyokuwa na kioo juu, enzi hizo tulikuwa tunafundishwa na mwl wa kike ss huyo mwlm alikuwa anapenda kukaa kwenye dawat langu akisahihisha daftari ss nilikuwa naweka kile kichengoe chenye kioo chin katikat ya miguu yake bila yy kujua ss kile kioo kinadisplay v2 alivyovyaa ss yule ticha alikuwa ana chup mbili alizo kuwa anapendelea kuzivaa nyeupe na nyekundu bas nilikuwa nafurahia sn huo mchezo kwa bahat mbaya yule ticha alihamishwa tukapewa mwalim wa kiume nilimchukia huyo mwalim mpaka nilivyoingia sdt 3
 

Hakuana siku nimecheka kama leo tangu mwezi huu uanze jamani. Funza dume you are too much!
 


Dah! Ebwana kweli wewe kwenu lazima mlikuwa mambo safi, na wala sina haja ya kuuliza kama mlikuwa na ''kideo'' kwenu. Maana enzi hizo mkiwa na video kwenu (sio TV kwa kuwa kulikuwa hakuna mtambo wa TV) basi mtaa mzima heshima mbele!
 

We kweli kichaa!
 
Wewe ni mwanaume au mwanamke samahani kama nimekukwaza

Nguli kwani wanaume hawayarudi mauno..vip kina Fally Ipupa wanavyokwenda sambaba na jukwaa..Kina Nyoshi El Sadaat teteteteh mambo ya fani tu
 
kuna jamaa mmoja alikuwa house boy wa nyumba ya jirani alitokea Musoma, sasa akapata demu akaimbisha na kukubaliwa kipindi hicho ndio UKIMWI umeingia bado mpya na kondomu ndio hata kutumia watu hawajui basi yule jamaa siku hiyo anaenda kuchenga ilibidi avae kondomu toka nyumbani kwao halafu ndio akaenda kwa demu jamaa njia nzima anatembea na mpira halafu kufika kule walipoaidiana demu hakutokea
 
SI UNGEJITOKEZA TU MBELE YA WAZAZI WAKE HUKU UKIWA UMEVALIA SARE ZA SHULE, UKAMWOMBA BINTI AKUAZIME KITABU CHA '' WHERE AND WHEN CAN WE MEET''? LABDA binti ANGEKUJIBU HICHO SINA NILICHO NACHO NI ''WE CAN MEET AT.......''na wakati huohuo ukijiandaa kutimua mbio just in case wazazi wanakijua kimombo.
 
Kama mambo ya huku yanachekesha hivi wengine si tutafukuzwa kazi jamani?
 

funzadume na wewe umeanza kutupiga fikisi hapa hahhahahah
 
Kama mambo ya huku yanachekesha hivi wengine si tutafukuzwa kazi jamani?

dada wee cheka kwa afya bana, maisha yenyewe yako wapi?? ongeza uhai hapa my dear
 
Heri yangu mimi enzi hizo mnazosema nilikuwa bado kuzaliwa:target:
 
maswala ya domo zege enzi zile usipime!

Nikiwa std four nilimchunuku sana Flora; demu alikuwa bomba shule nzima; mtoto wa mwalimu nami mama ni mwalimu mkuu wa shule hiyo hiyo; sasa mbaya zaidi mama yangu na mama yake walikuwa wakitaniana na kuitana wakwe; wasijue mwenzao nafanya kweli kwa kupenda kitu; kazi ilkuwa kwnye kumwambia Flora; jamani nyie acheni tu hili swala la madem kuhongwa ama kubembelezwa kwa zawadi ni instinct zinazokuwepo aklini mwa wavulana tangu wkiwa wadogo mno kuliko tunavyofikiri! Mie kwa kuwa Mama ni mkuu hivyo nilikuwa na access na funguo ya stoo ya shule mara kwa mara na mzee ilkuwa sifanyi ajizia nikipata mwanya wa kuingia huko kama si daftari 2 ama 3 natoka na rangi za kuchorea ama hata kitabu kimoja cha hadithi na hivyo vitu lazima vifike kwa Flora; Mpelekaji alikua ni Binamu yangu. Basi nikiambiwa kavipokea mimi roho yangu kwatu! aah we acha tu.
Mkasa ulikuja kututokea puani siku binamu alipobambwa na Mama yake Flora; alihisiwa labda kamwibia Mama; kesi ikaletwa nyumbani ilikuwa pata shika ukaguzi ukafanyika chumbani kwangu! mchizi nikakutwa nimetengeneza hadi cheti cha ndoa yetu Flora (coppying my mother's of coz)
Yaani wakubwa wote waliishiwa hamu; nilichapwa sana na kulazimishwa kujiunga kutumikia kanisani mwaka mzima na mama! Shule nzima walijua lakini kwa kuwa nilikuwa mtoto wa ticha mkuu hakuna aliyethubutu kunitania!

lakini kazi yangu ilikuwa na malipo hatimaye nilipofika form one nilizawadiwa tunu na Flora! Namtakia maisha mema huko aliko!
 
mmmmh.
 
Haya mambo ya kutokuwa na mtandao wa simu nilikuwa nakwenda kumvizia demu mmoja kanisani. Sasa siku moja nikachelewa kuamka, kwa hiyo nikakuta misa imeshakwisha. Ikabidi niende mitaa ya kwao maana kusubiri tena mpaka Jumapili inayofuata ingekuwa mbali sana. Halafu sikuwa na uhakika wa nyumba anayoishi ila mtaa naujua.

Nikazunguka zunguka mtaani mwisho nikajitoa ufahamu na kuamua kugonga mlango kwenye nyumba mojawapo. Nikakaribishwa, kuingia ndani mzee mwenye nyumba ndiye kakaa sebuleni. Baada ya kumwamkia, akaniuliza shida yangu, nikamwambia nimesikia mtaa huu kuna nyumba wamechinja nguruwe kwa hiyo nimekuja kununua nyama ya nguruwe, je ni nyumba hii? Yule mzee akasema hapana sio hapa. Kwa kuwa hakuwa na taarifa za nguruwe kuchinjwa hapo mtaani ikabidi amwite binti yake amuulize! Binti kuja, kumbe ndiye yule yule ninayemtafuta kwa hiyo kama zali vile nikawa nimepatia nyumba! Kumuona tu mimi moyo wangu wote kwatu. Alipoulizwa akasema hakuna mahali wamechinja nguruwe mtaa ule labda nimechanganya mitaa. Basi nikaaga nikaondoka.

Siku nilipokuja kufanikiwa kumpata, akaniuliza...''Hivi ni kweli siku ile ulipokuja nyumbani kuulizia nyama ya nguruwe ilikuwa kweli umesikia wamechinja nguruwe au ilikuwa geresha tu?''...Nilicheka sana!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…