Enzi zetu za shule

Umenikumbusha mbali sana, nilisoma Mwakaleli miaka ya 1995 (A Level) kuna mwalimu mmoja alikuwa mtaalamu wa Biology O - Level, hivyo vijana walimuita AMOEBA (Amiba) kwa jinsi alikuwa mtaalamu wa somo hilo lakini pia alivyokuwa rough.
 
wakati nasoma Songea Girls kuna mwalimu alikuwa na shingo fupi sana huyo tulikuwa tunamwita "tumchinjie wapi"
 
Mwalimu wetu wa Kiswahili form two alikuwa ndo kwaanza anatoka kozi; Topic yake ya kwanza ilikuwa ni Mofimu! Basi mpaka namaliza shule aliitwa mofimu!
 
Dah! kweli hii imenikumbusha mbali hata mimi, maana enzi hizo kwa wale waliosoma shule moja ya vipaji kaskazini mwa Tz wanaweza kuwakumbuka hawa.....
1. Mswahili (R.I.P) ------ Huyu ticha alikua mwalimu wa nidhamu alikua na vijisharubu hv na alikua akikubamba na soo tu neno la kwanza kumtoka ni "mswahili..."
2. Chifu ------- Huyu ni ticha mmoja wa kimasai alikua anapenda sana kuita watu chifu kwa mfano "chifu nitakukata vigongo" maana yake nitakupa stick. Jamaa alikua na misifa sana sijui kama hadi leo yupo.

3. Machakura (R.I.P) ----- machakura linatokana na neno chakula huyu ticha alikua ni Mkurya
4. Amanda ----- Jina hili lilitokana na tangazo la sabuni ya Amanda...nakumbuka huyu ticha alikua anafunisha geography
na wengineo wengi tu km Dudubaya, Rucockroach(Rumende)
 
Sijaona wadau wa Mzumbe Academic Village aka MAVI mpo kwenye JF?
Mara ya kwanza kutua Moro Mji kasoro bahari nilipendezwa sana na mazingira yake..ila nilipotua kwenye magofu ya mzumbe nikajua huku starehe yetu ni kitabu tuuu..Nawakumbuka sana mateacher kama
Anthony Wibonele aka Mkhomboti au alikuwa akijiita Tanzania One Physics (TOP) ..RIP
Msabila..(RIP) huyu nae alikuwa si haba kwenye Chemistry vijana walikuwa wanachezea mabanda tu kwenye NECTA...
Sifa moja ya wibonele alikuwa anafundisha Number na physics ilikuwa burudani tosha kwenye vipindi vyake..

Bila kumsahau Mkuu mwenye enzi hizo Thomas Dedemtula Msuka....
Wanamzumbe wanaweza kumalizia wimbo wa shule huu( ambao ulikuwa ukiimbwa J5 siku ya Ukaguzi wa Headmaster)
...Shule yetu Mzumbe sekondariiii ..Yasifika kote Tanzaniaa
..Malezi ya mzumbe..Elimu ya mzumbe....
( beti zimenipotea hapo..)
 
kuna mwalimu wangu mmoja wa primary tulimwita KENUA kutokana na tabia yake ya kukagua meno, so akikufikia anakwambia kenua, from there onwards ndo likawa jina lake
 
r.i.p trial balance wangu wa lugalo secondary iringa alifariki mwishoni mwa miaka ya tisini.

Bunsen burner.......huyu ni mwalimu wangu wa kemia form 1 na alinifanya nilipende somo kwa uhondo na namna alivyokuwa akilitamka jina la hicho kifaa cha maabara.

Sir ambi (sijui kama yupo hai) alikuwa mojawapo wa walimu ogopwa sana enzi hizo. Kutokana na u-seriousness wake watu walimpachika jina la sir

mheshimiwa comrade ...marehemu mwalimu materu ambaye aliwahi kututishia form one enzi hizo kwamba majina yetu yameandikwa kwa penseli kwenye rejista ya shule; hivyo kwake ilikuwa ni rahisi kutufuta! Akikuita lazima akwambie mheshimiwa comrade. Lakini wanafunzi ni wanafunzi; akiwa ni mwalimu wa somo la kilimo alikuwa ndiye msimamizi wetu wa orientation na orienatio enzi hizo ilikuwa ni kulima bustani (waliofika lugalo sekondari iringa wanalifahamu eneo husika linalimwa mboga mboga karibu mwaka mzima) vijana kwa kukwepa kazi tuliandikisha orodha ya majina kwa kuytaumia majina ya wachezaji wa yanga na simba wa enzi hizo! Tih tih ilikuwa patashika wakati wa gwaride la utambuzi mheshimiwa comrade alipokuwa anang'angania kumwadhibu a.k.a abedi mziba ama omari fungo na minziro wake!teh teh teh

headmaster wangu wa kwanza mwl mazengo aliwahi kuja shule kavaa raba enzi hizo zikiwa na jina maarufu la kuchumpa; ikawa soo kwani alimfuma mwanafunzi akiwaambia wenzie "headmaster kavaa la kuchumpa" yeye akatafsiri neno la kuchumpa ni kitu cha wizi! Ilikuwa mshike mshike na bahati mbaya sana alikuwa na kigugumizi!

Namshukuru mungu nilipata bahati ya kupita mikononi mwao pamoja na vituko vyote tulivyovifanya bado wao ndio ndio msingi wa mimi nilivyo sasa




jamani endelezeni safu!
umenikumbusha mbali sanaaaa.
 
kijenge primary school kulikuwa na mwalimu anaitwa HAITOSHI.
Kila alipokuwa anaingia darasani akisalimiwa anasema haitoshi ,hivyo wanafunzi marudia kumsalimia anasema haitoshi kwa hiyo mnarudia tena na tena alikuwa anaitwa Mwl.Mujwauzi ni miqaka kibao cjui leo hii yuko wapi?
 
Back
Top Bottom