Enzi za Mwalimu - Tupia yako

Enzi za Mwalimu - Tupia yako

Rubi

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2009
Posts
1,615
Reaction score
332
Tupia yako unayokumbuka enzi za Mwalimu

enzi za mwalimu


















 
Rubi , enzi za mwalimu kuna mambo mengi sana. Nakumbuka juu ya maduka ya kaya. Kununua bidhaa kwa foleni. Bidhaa zenyewe adimu, hivyo ikipatikana lazima itunzwe na itumiwe kwa uangalifu. Nakumbuka siku moja wakati nikiwa mdogo baba yangu alinikuta nalamba sukari ambayo alisota sana mpaka kuipata. Nilichapwa viboko ambavyo navikumbuka mpaka leo, miaka mingi ikiwa imepita.
 
enzi za mwalimu
wananchi tulikuwa 15m tulisoma kutibiwa bureee na kupewa chakula hasa nyakati za matatizo kama ya njaa bureeee na serikali ilikuwa haina hata muwekezaji mmoja.
 
enzi za mwalimu
wananchi tulikuwa 15m tulisoma kutibiwa bureee na kupewa chakula hasa nyakati za matatizo kama ya njaa bureeee na serikali ilikuwa haina hata muwekezaji mmoja.
Pia kalamu, rula na madaftari 12 tulikuwa tunagawiwa shule siku mnapofungua shule pamoja na mikebe.

Na bado kulikuwa kuna zawadi za washindi wanaofanya vizuri kwenye mitihani yao ya mwisho.
- kulikuwa na ngoma za shule, mchakamchaka, gwaride la shule, somo la sayansikimu tulikuwa tunafanya kwa vitendo yaaani tunapika na kula shule.

- Tulikuwa tunakaguliwa nguo za ndani kila alhamisi kwa shuleni kwetu hasa darasa la kwanza mpaka la nne au la tano. enzi za mwalimu raha.
 
Enzi za mwalimu ukisikia Mwalimu (Rais) anakuja kwenye mkoa wenu siku hiyo ni kujipanga barabarani kuimba na kupiga makofi kila anapopita maana kazi zote zinasimama kwa muda mpaka apite.
 
  • Thanks
Reactions: awp
Mimi nakumbuka daftari likiisha teacher anakusignia unaenda kuchukua daftari lingine!
Zile zama achana nazo kabisa
 
wafanyakazi walifanya kazi kwa moyo na kwa bidii,pia askari alikua ni mtu tayari mda wote mkakamavu zaidi
 
Pia Watanzania tulikuwa tunapendana sana na kuaminiana kiasi kwamba ilikuwa sio shida kumkaribisha mtu aliyepotea kulala nyumbani kwako bila tatizo mpaka atakapompata mwenyeji wake.

Siku hizi mtu usiyemjua sio rahisi kumkaribisha nyumbani kwako maana si salama tena.
 
Enzi za mwalimu....Tulikua tunasimuliana kuwa askari wa kenya anaogopwa na raia kama ukoma huku kwetu ni askari ni ndugu,rafiki na msaada wa karibu ukipata shida. Siku hizi dah ulimwengu umepinduka kichwa chini miguu juu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom