Enzi za Kikwete vijana wa JKT walikuwa wanakimbia usaili wa Polisi, Zimamoto na Magereza

Kiboko ya Jiwe

JF-Expert Member
Apr 7, 2020
12,702
36,131
Nimekumbuka jambo, siku moja jeshi la polisi walikuja Ruvu JKT kuwasaili vijana ili wawaajiri. Vijana walijitokeza kama tu kujaribu zari lao huku wengine wakijisemea kuna la kesho na keshokutwa. Kuna vijana madoja wakubwa wa shamba ile siku walijipeleka shamba wenyewe ili tu wasifanye usaili wa Polisi.

Kule zamani kijana ukitokea mtaani unasema ikitokea kazi yoyote utakuwa tayari kufanya cha ajabu ukimaliza tu six week unaanza kuchagua kazi. Kazi kama ya Upolisi, Zimamoto na Magereza walikuwa wanaenda watu wenye vyeti vya kuungaunga, wenye miili yenye excuse au vijana wanaokaribia kumaliza mikataba yao ya miaka 2.

Siku hizi dunia iko kasi, hata mgambo wa Jiji wakienda Ruvu JKT kuhitaji nguvu kazi vijana watapigana vikumbo kugombea hizo nafasi.
 
2014 nilikata kuwa mwanajeshi zilitoka offer za wanafunzi form six waliosoma science ila saivi najuatia offer ile.

Sent from my TECNO LA7 using JamiiForums mobile app
Ulifanya umburula sana, ulijisemea niingie na degree. Kumbe ile six yako jeshini ni equivalent ya degree. Hiyo chance hupati tena, kwani jeshini maafisa wengi sasa ni form six then jeshi huwaendeleza wenyewe.
 
Ulifanya umburula sana, ulijisemea niingie na degree . Kumbe ile six yako jeshini ni equivalent ya degree. Hiyo chance hupati tena , kwani jeshini maafisa wengi sasa ni form six then jeshi huwaendeleza wenyewe.
Ni choice ambayo kwa kipindi kile ilikuwa sahihi kwangu kwanza sikuwa na exposure na jeshi kw namna yoyote ile kusema nilifanya umburulala siyo sawa!
 
Kweli
giphy.gif
 
Sasa hivi kubeti imekuwa ni mojawapo ya njia isiyo rasmi inayowaingizia vijana kipato cha mwezi.
Ha ha ha ha sana!na pool table kuna jama angu nilimaliza naye chuo akenda kusoma master ya public health saivi ni dereva bajaji jamaa yuko frustrated sana,familia inamuona kama hana muelekeo,bado jamii ina muandama kabaki kunywa vitoko tu.
 
Yeah mkuu ila kwenye maisha ni muhimu sana, kupata mentor kwenye maamuzi mengi sana ya maisha mimi kuanzai combinations niliyosoma advance,course niliyosoma chuo zote nilichagua kwa mihemuko!

Sent from my TECNO LA7 using JamiiForums mobile app
Mimi nilichagua chuo course ya kuweza kupata mkopo, na kweli nikapata 100% wakati wa Mkwele, kimbembe kimekuja wakati huu tunaotakiwa kuilipa hiyo pesa kwa mafisadi.
 
Back
Top Bottom