Kwahiyo sasa hivi nawe ni super star kama Mimi!!?Mtoa post unafikir sana,umenikumbusha nikiwa darasa la pili 1998,leo nimecheka sana leo baada ya kukumbuka nilivyokuwa miaka hyo na leo hii nimtu mashughuli sana ,asante mungu na mtoa post pia
Daaah!! hiyo hadi Leo huwa naifanya nikiwa mwenyewe bafuniilikuwa ukimwagiwa maji kichwani unapagusa kauso na mkono huku unapuliza maji ili upumue kwa amani kidogo.,, mie nlikuwa nkiogeshwa mikono naziba kwenye ofisi... Kimbembe ilikuwa kuchanwa nywele babuu kipilipili si mchezo..,
ikitokeo uneoga mwenyewe ukaguzi unasuguliwa mgongoni,tumboni, miguuni lazma kuna sehemu maji yasifike
Maisha bora....Haya mambo ya kusugua binadamu na mawe ndiyo leo nayasikia kwenu. Kwa mimi nijuavyo ni terrazzo tu ndizo husuguliwa na mawe!!
Huyo House girl Safi Sana, si una ona jinsi ulivyo mrembo, sasa bila kusuguliwa vizuri unadhani ungekuwa hivyo?.hii imenikumbusha mbali sana.....tulikuwa na housegirl mnoko sana....alikuwa ananisugua miguu na jiwe basi ananikwangua huyo......nilimchukia sana.......
Mimi siku nyweahwa maji1. Halafu unanyweshwa kidogo maji ya kuogea.......sijui maana yake
2.Mguuni unaguliwa na jiwe "laini" (siyaoni siku hizi)
3. Ole wako uwe na michubuko kwenye miguu kutokana na kucheza mpira halafu unakumbana na mama kauzu utakoma
4. Ukimaliza kuoga unakaushwa juani na kupakwa mafuta ya mamis na kuvishwa nguo ya mtumba