Enock Akeyo aliwashitaki Vodacom kwa kutangaza ofa hewa

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,016
9,885
Mteja wa Vodacom, Enock Akeyo alipokea ujumbe kutoka vodacom mwaka 2018 ukisema "Pesa ni Mpesa tunakupa MB 100 BURE kuperuzi intaneti kwa saa 24 ukiongeza salio la TZS 500 au zaidi kwa Mpesa leo."

Enock aliongeza salio na akapokea sms iliyoonesha amepewa MB100 za kuperuzi. Hata hivyo baada ya dk 8 akashangaa salio lake lote limeisha. Alipowapigia aliambiwa hakujiunga na kifurushi ndio sababu ya hela yake kutumika

Enock alienda Kamati ya Malalamiko ya TCRA ili kufikisha kesi hiyo na kudai fidia ya Tsh. 5,000,000 kwa sababu ya usumbufu na kupewa ahadi ya uongo wa ofa ya Mb.

Hata hivyo, vodacom walithibitisha kuwa mteja wao alipata MB100 lakini alizitumia kwa sekunde moja na zikaisha zote.Yaani aliwasha data majira ya saa mbili na dakika 22 na sekunde 51, na muda huohuo MB100 ziliisha.

Mbali na kuwa inaonesha ukakasi lakini kamati ya malalamiko ya TCRA ilikubali hoja za Vodacom hivyo Enock alishindwa kupata fidia mbali na kusema ilimletea shida.

Kwa maelezo ya Enock ni kuwa alipowasha data alisoma emails chache na kuingia JamiiForums kuperuzi akapata taarifa salio lake ni Tsh 0.00
IMG_4764.jpeg
IMG_4765.jpeg
IMG_4766.jpeg
IMG_4767.jpeg
IMG_4768.jpeg
IMG_4769.jpeg
IMG_4770.jpeg
IMG_4771.jpeg
IMG_4772.jpeg
 

Attachments

  • Uamuzi wa Kamati ya malalamiko ya Mamlaka Ya Mawasiliano Tanzania, Kati ya Enock Akeyo Vs Voda...pdf
    2.9 MB · Views: 1
Uwezi kuwashinda vigogo... Meneja wa Vodacom si ndio dada yake Nape, waziri wa hiyo hiyo wizara ya mawasiliano ni kaka... Dada ni mkuu Vodacom, Kaka ni waziri wa mawasiliano... Utashinda vipi kesi.... Wewe ni sawa na Nyumbu kwenye mahakama ya Fisi, na unaenda kumshitaki fisi... Unategemea ushinde
 
Uwezi kuwashinda vigogo... Meneja wa Vodacom si ndio dada yake Nape, waziri wa hiyo hiyo wizara ya mawasiliano ni kaka... Dada ni mkuu Vodacom, Kaka ni waziri wa mawasiliano... Utashinda vipi kesi.... Wewe ni sawa na Nyumbu kwenye mahakama ya Fisi, na unaenda kumshitaki fisi... Unategemea ushinde
Kwani 2019 Nape alikuwa waziri!?
 
Ipo siku tutawashitaki mitandao ya simu na wale kampuni za kubahatisha na sms zao fulani namba yako imechaguli mara imeshinda ...bra brah...

Tuma neno .....pate milioni ....
 
Wakati mwingine ni Bora kwenda mahakamani moja kwa moja huku ukiweka mawakili. Mashauri kupitia TCRA wakati mwingine yanaendeshwa kisiasa na yanachukua muda mrefu.
Kuna mwamba kawashitaki Vodacom mahakamani kwa kutoa taarifa zake bila idhini take na anadai fidia ya bilioni 10 na kesi bado inaendelea.
 
Back
Top Bottom