Eng. Mfugale amemkwaza Rais?

Eng. Mfugale amemkwaza Rais?

Mpucha

JF-Expert Member
Joined
Jun 11, 2012
Posts
1,268
Reaction score
1,647
Wakuu,

Leo wakati mkuu wa nchi anakagua pale Ubungo interchange, ni dhahiri kabisa mkuu kuna kitu kimemuudhi, yule hisia zake hazifichiki, nadhani kuna kitu Mfugale amemkwaza Mh Rais.

Mimi binafsi sikupenda Mfugale alipokuwa anatoa maelezo kwa kutumia lile lifimbo lake la kutembelea kila mara analiinua juu, ule ni ukosefu wa nidhamu hasa unapoongea na mkuu wako, nadhani na yale majibu aliyomjibu Waziri Mkuu pia yamemkwaza Jiwe.
 
Nadhani Mh. Mfugale haikuwa vizuri kutokutekeleza maagizo ya waziri mkuu. Ingawa anaweza asitolewe kwa sababu ya uadilifu na misimamo yake, maana TANROAD ukiweka fisadi lazima panuke
 
Kwa walipotokea katika kile kiofisi pale posta wanakwenda kuchukuliana mihogo ya njano kule ferry na juisi ya supa dipu ili mchana upite, kusaidiana kwa shida na raha na kwa illegal na legal usitegemee baadhi ya watu waliokwepo TANROAD ile kuguswa.
 
Watajijua wenyewe
Ila ukitaka atumie nini kumwelewesha mkulu ??
Wakuu,

Leo wakati mkuu wa nchi anakagua pale Ubungo interchange, ni dhahiri kabisa mkuu kuna kitu kimemuudhi, yule hisia zake hazifichiki, nadhani kuna kitu Mfugale amemkwaza Mh Rais.

Mimi binafsi sikupenda Mfugale alipokuwa anatoa maelezo kwa kutumia lile lifimbo lake la kutembelea kila mara analiinua juu, ule ni ukosefu wa nidhamu hasa unapoongea na mkuu wako, nadhani na yale majibu aliyomjibu Waziri Mkuu pia yamemkwaza Jiwe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanafahamiana vizuri hao. Mfugale ndiyo mkusanya 10% kuanzia Jiwe akiwa Waziri wa Ujenzi. Ndiyo maana hata mwenyewe wala hajashtuka. Ondoa wasiwasi Jiwe hajakwazwa na Mfugale. Hao ni ndege wa rangi moja
Unajua saikolojia ya wezi huwa iko hivi, ukiwa mwizi unakuwa unajua kuwa kila mtu ni mwizi kama wewe ulivyo mwizi, wakati siyo!
 
Mbona hakuna shida yoyote.Mheshimiwa Rais anapenda uwajibikaji,muda mwingine watu wanamtamfsiri vibaya..
 
Mfugale na jpm ni ndege wawili wafananao wanaoruka pamoja
body language aliyoonyesha jpm leo ni kufunika maboya ili isionekane anambeba mfugale but in fact wanajuana
 
Halafu ukimuangalia kwa umakini inaonekana Mfugale kiafya hayupo vizuri.... Kwenye hiyo ziara ni kama amejilazimisha tu....
Nadhani Mh. Mfugale haikuwa vizuri kutokutekeleza maagizo ya waziri mkuu. Ingawa anaweza asitolewe kwa sababu ya uadilifu na misimamo yake, maana TANROAD ukiweka fisadi lazima panuke

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unajua saikolojia ya wezi huwa iko hivi, ukiwa mwizi unakuwa unajua kuwa kila mtu ni mwizi kama wewe ulivyo mwizi, wakati siyo!
Kama unajiita Makanyaga wewe mwenyewe nani atakuheshimu kama mwenyewe hujiheshimu.
 
Wanafahamiana vizuri hao. Mfugale ndiyo mkusanya 10% kuanzia Jiwe akiwa Waziri wa Ujenzi. Ndiyo maana hata mwenyewe wala hajashtuka. Ondoa wasiwasi Jiwe hajakwazwa na Mfugale. Hao ni ndege wa rangi moja
Ndiye anayetekeleza miradi ya chattle na ziwa na anaonekana amemshika mtu pabaya.
 
Ila pia naona mambo ya Mfugale yanaanza kwenda vibaya manake inaonekana jiwe hakupendezwa na namna yake asubuhi na hadi sasa kashampa onyo la mwisho huko Morogoro duh.
 
Back
Top Bottom