Eneo kuzunguka kitovu linauma, ni nini hiki?

BABA TUPAC

JF-Expert Member
Sep 30, 2015
1,526
3,802
Hii hali hutokea mara moja moja sana, yaani naweza kuwa nimejilaza kitandani inatokea eneo linalozunguka kitovu linakuwa kama linavuta hivi kiasi kwamba siwezi kufanya chochote kwa wakati huo inabidi nitulie.

Hali hii haidumu kwa muda mrefu, huchukua kati ya sekunde thelathini mpaka dakika moja. Na hali hii huwezi kutokea mara moja kwa mwezi au nikakaa ndani ya miezi hata miwili isitokee lakini baada ya muda huja kujirudia tena. Ninachojiuliza hii hali husababishwa na nini? Je, ni tatizo la utumbo au ni kitu gani?

Kwa hapa Dar ni kuna clinic yoyote ile ya specialist wa maswala ya tumbo? ipo sehemu gani?

Note: Mimi ni mwanaume

Asanteni.
 
Hii hali hutokea mara moja moja sana, yaani naweza kuwa nimejilaza kitandani inatokea eneo linalozunguka kitovu linakuwa kama linavuta hivi kiasi kwamba siwezi kufanya chochote kwa wakati huo inabidi nitulie.

Hali hii haidumu kwa muda mrefu, huchukua kati ya sekunde thelathini mpaka dakika moja. Na hali hii huwezi kutokea mara moja kwa mwezi au nikakaa ndani ya miezi hata miwili isitokee lakini baada ya muda huja kujirudia tena. Ninachojiuliza hii hali husababishwa na nini? Je, ni tatizo la utumbo au ni kitu gani?

Kwa hapa Dar ni kuna clinic yoyote ile ya specialist wa maswala ya tumbo? ipo sehemu gani?

Note: Mimi ni mwanaume

Asanteni.
Mchango wenu ni muhimu wadau
 
Mkuu ebu ipeleke hii kule jf doctor ukapate ushauri wa wataalamu,kama wewe ni mgeni basi jua kuwa kuna jukwaa maalum linalohusu mambo ya tiba na afya linaitwa jf doctor" litafute halafu kaulize kule tatizo lako nazani utapewa ushauri wa kitaalam na experience za watu mbali mbali,hapa sio mahala pake
 
Jombaa,una minyoo ya gredi wewe,tafta dawa ya minyoo meza baada ya kila mezi tatu.Kama unawashwa pia kando na kuumwa hiyo sehemu ya kitovu ni hakikisho kuwa ni minyoo imezidi.Tafta ushauri wa daktari lakini maanake huu ni mtandao wa kijamii,si hospitali hii!
 
Jombaa,una minyoo ya gredi wewe,tafta dawa ya minyoo meza baada ya kila mezi tatu.Kama unawashwa pia kando na kuumwa hiyo sehemu ya kitovu ni hakikisho kuwa ni minyoo imezidi.Tafta ushauri wa daktari lakini maanake huu ni mtandao wa kijamii,si hospitali hii!
Acha kupotosha raia wasio na hatia
 
Acha kupotosha raia wasio na hatia
Wala sijampotosha atakapoenda kwa daktari ataambiwa hivo hivo,najua nachoongelea.Kama nimekosea kidogo bado mawaidha ya kunywa dawa ya minyoo baada ya miezi tatu ni sahihi kabisa.Nahisi wewe ni miongoni mwa wale watakaomshauri kuwa amerogwa kwa hivyo amtembelee mchawi!Sindio?
 
Hii hali hutokea mara moja moja sana, yaani naweza kuwa nimejilaza kitandani inatokea eneo linalozunguka kitovu linakuwa kama linavuta hivi kiasi kwamba siwezi kufanya chochote kwa wakati huo inabidi nitulie.

Hali hii haidumu kwa muda mrefu, huchukua kati ya sekunde thelathini mpaka dakika moja. Na hali hii huwezi kutokea mara moja kwa mwezi au nikakaa ndani ya miezi hata miwili isitokee lakini baada ya muda huja kujirudia tena. Ninachojiuliza hii hali husababishwa na nini? Je, ni tatizo la utumbo au ni kitu gani?

Kwa hapa Dar ni kuna clinic yoyote ile ya specialist wa maswala ya tumbo? ipo sehemu gani?

Note: Mimi ni mwanaume

Asanteni.
Hyo inaweza kuwa ni peri umbilical pain sasa saba zake nyingi sana inaweza kuwa ni appendicitis sasa wahi muone daktari mapema kabla hujazidiwa mm ningekusaidia ila nipo mbali sana
 
Hyo inaweza kuwa ni peri umbilical pain sasa saba zake nyingi sana inaweza kuwa ni appendicitis sasa wahi muone daktari mapema kabla hujazidiwa mm ningekusaidia ila nipo mbali sana
Nashukuru mkuu. Dawa ya appendix si ni operation? Dah, hapa sina amani tena
 
Nasikiaga kuna watu wana tatizo la utumbo kujifunga funga. Nenda hospitali ukapige x ray kuweza kupata majibu...
 
Hiyo ni umbilical hernia
Hii hali hutokea mara moja moja sana, yaani naweza kuwa nimejilaza kitandani inatokea eneo linalozunguka kitovu linakuwa kama linavuta hivi kiasi kwamba siwezi kufanya chochote kwa wakati huo inabidi nitulie. Hali hii haidumu kwa muda mrefu, huchukua kati ya sekunde thelathini mpaka dakika moja. Na hali hii huwezi kutokea mara moja kwa mwezi au nikakaa ndani ya miezi hata miwili isitokee lakini baada ya muda huja kujirudia tena. Ninachojiuliza hii hali husababishwa na nini? Je, ni tatizo la utumbo au ni kitu gani? Kwa hapa Dar ni kuna clinic yoyote ile ya specialist wa maswala ya tumbo? ipo sehemu gani? Note: Mimi ni mwanaume Asanteni.
 
kafanye check up inawezekana ikawa umb hernia au intestnal worms,appendicitis hvyo kukupa ni shida gan bla vpimo hatutakusaidia ipasavyo
 
Back
Top Bottom